Matangazo
◼ Vichapo vya kutolea watu katika Mwezi wa 1: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa msikilizaji amekwisha kupata kitabu hicho, mhubiri anaweza kumtolea kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa mbele ya mwaka wa 1995. Mwezi wa 2: Je, Kuna Muumba Anayekujali?, Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Mwezi wa 3: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Mujikaze sana ili kuanzisha mafunzo ya Biblia. Mwezi wa 4 na wa 5: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Munaporudilia watu wenye kupendezwa, kutia ndani wale waliohuzuria Ukumbusho ao matukio mengine ya kitheokrasi lakini hawajiunge sana na kutaniko, mujikaze kuwatolea kitabu Biblia Inafundisha. Mwezi wa 6: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa msikilizaji amekwisha kupata kitabu hicho, mhubiri anaweza kumtolea kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa mbele ya mwaka wa 1995.
◼ Kuanzia Mwezi wa 2, waangalizi wa mzunguko watatoa hotuba ya watu wote yenye kichwa “Kweli Ina Matokeo Gani Katika Maisha Yako?”