Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 5/11 uku. 4
  • Matangazo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2011
Huduma Yetu ya Ufalme—2011
km 5/11 uku. 4

Matangazo

◼ Vichapo vya kutolea watu katika mwezi wa 5: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Tunaporudilia watu wenye kupendezwa, kutia ndani wale waliohuzuria Ukumbusho ao matukio mengine ya kitheokrasi lakini hawajiunge sana na kutaniko, tujikaze kuanzisha mafunzo ya Biblia kwa kutumia kitabu Biblia Inafundisha. Mwezi wa 6: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa msikilizaji amekwisha kupata kitabu hicho, mhubiri anaweza kumtolea kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa mbele ya mwaka wa 1995.

◼ Utumishi wa Betheli: Biro ya Tawi inapenda kuwatia moyo ndugu na dada walio na sifa nzuri za kiroho na wenye miaka kati ya 19 na 35 wanaojua kazi zinazotajwa hapa chini wahuzurie mkutano utakaofanywa kwenye Mkusanyiko wa Wilaya kwa ajili ya wale wanaotaka kutumika kwenye Betheli na kisha wajaze ombi kwa ajili ya utumishi wa Betheli: ndugu wanaojua kutengeneza gari ndogo-ndogo na kubwa-kubwa (mécaniciens); ndugu wanaojua kutembeza gari kubwa-kubwa; ndugu wanaojua mambo ya elektroniki (électromécaniciens); ndugu walio na ufundi mbalimbali (mécaniciens-ajusteurs: tour, fraiseuse, rectifieuse); na walio na ufundi wa vyombo vya kusambaza joto, hewa, na kupoleza hewa (frigoristes).

◼ Tafazali, jueni kwamba nyongeza imetayarishwa ili kuonyesha mambo yenye kupendeza kuhusu Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Lingala. Nyongeza hiyo inapatikana katika Lingala na Kifaransa. Ikiwa kutaniko lenu linahitaji nyongeza fulani, munaweza kuziomba kwa kutumia fomu S-14 na kutia alama km11 05-LI ao km11 05-F.

◼ Azimio: Katika mkutano wa utumishi wa juma tokea tarehe 9 mwezi wa 5, mzee mmoja atasoma tena barua ya tarehe 7 mwezi wa 12, 2009 ili kuchunguza tena ‘azimio lenu kwa ajili ya Jumba la Ufalme.’ Katika mkutano wa utumishi wa juma tokea tarehe 16 mwezi wa 5, mratibu wa baraza la wazee atapendekeza azimio jipya kwa kutaniko. Kisha, atatuma kopi ya azimio hilo jipya kwenye biro ya tawi.

◼ Karibuni tutatuma mahali mbalimbali ambapo mikusanyiko ya wilaya itafanywa, bahasha (enveloppe) ya kila kutaniko iliyo na fomu kwa ajili ya mwaka wa 2012. Kila mwandishi wa kutaniko atahakikisha kwamba kutaniko lao limepata bahasha hiyo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine