Kujikumbusha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maulizo yanayofuata yatatumiwa kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi katika juma tokea tarehe 27 mwezi wa 6, 2011. Kwa muda wa dakika 20, mwangalizi wa shule ataongoza kujikumbusha kunakotegemea habari zilizozungumziwa tokea tarehe 2 mwezi wa 5 mpaka tarehe 27 mwezi wa 6, 2011.
1. Tunaweza kujifunza nini kutokana na jinsi Yehova alivyomwomba Ayubu asali kwa ajili ya wale waliomkosea? (Ayu. 42:8) [w98 8/15 uku. 30 fu. 5]
2. ‘Zabihu za uadilifu’ ambazo Wakristo wanatoa leo ni nini? (Zab. 4:5) [w06 5/15 uku. 18 fu. 9]
3. Namna gani figo za Daudi zilimurekebisha? (Zab. 16:7) [w04 12/1 uku. 14 fu. 9]
4. Namna gani “mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu”? (Zab. 19:1) [w04 10/1 uku. 10 fu. 8]
5. Zaburi 27:14 inaonyesha uhusiano gani kati ya tumaini na uhodari? [w06 10/1 uku. 26-27 fu. 3, 6]
6. Namna gani Zaburi 37:21 inatusaidia tujue jinsi tunavyoweza kuwatendea ndugu zetu? [w88 8/15 uku. 17 fu. 8]
7. Kuhusu kupendezwa na ibada, tunaweza kujifunza nini kutokana na vile Mlawi aliyekuwa uhamishoni alivyojisikia? (Zab. 42:1-3) [w06 6/1 uku. 9 fu. 3]
8. Ni nini kinachoweza kutusaidia kupenda uadilifu na kuchukia uovu? (Zab. 45:7) [cf uku. 58-59 fu. 8-10]
9. Daudi aliomba ategemezwe kwa “roho ya kupenda” ya nani? (Zab. 51:12) [w06 6/1 uku. 9 fu. 10]
10. Namna gani tunaweza kuwa kama mzeituni katika nyumba ya Mungu? (Zab. 52:8) [w00 5/15 uku. 29 fu. 6]