“Ninaweza Kuripoti Saa Hizo?”
Je, umekwisha kujiuliza ulizo hilo? Maagizo kuhusu kuripoti saa yanapatikana katika kitabu Tengenezo ukurasa wa 86-87. Maagizo mengine yanatolewa mara kwa mara, kwa mfano Kisanduku cha Maulizo katika Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 9, 2008. Kwa kuwa hali zinabadilika, hatukupewa sheria nyingi kuhusu jambo hilo. Kwa hiyo, si jambo lenye kufaa wazee waweke sheria ya zaidi kuhusu jambo hilo.
Ikiwa kunatokea ulizo fulani kuhusu jambo hilo na kwamba hakuna kichapo kinachotoa mwongozo, kila mhubiri anaweza kufikiria maulizo haya: Je, nilitumia wakati huo katika mahubiri? Ao je, nilitumia wakati huo katika mambo fulani mengine yasiyopatana na kazi ya kuhubiri? Zile saa tunazoandika kwenye ripoti ya utumishi wa shambani kila mwezi zinapaswa kutuletea furaha, hazipaswi kufanya zamiri yetu isumbuliwe. (Mdo. 23:1) Kwa kweli, jambo tunalohangaikia zaidi si jinsi ya kuhesabu wakati, lakini jinsi ya kutumia wakati wetu kwa hekima kwa kutumika kwa bidii tunapokuwa katika kazi ya kuhubiri.—Ebr. 6:11.