Tumia Wakati Wako kwa Matokeo
1 Kila mmoja anacho kiwango kile kile cha wakati kila juma. Sehemu tunayotoa kwa kueneza habari njema ni yenye thamani ya pekee kwa kuwa huo ni wakati unaopitishwa katika kazi ya kuokoa uhai. (Rom. 1:16) Tunaonyesha kwamba tunathamini jambo hilo kwa kujitayarisha vema kwa ajili ya utumishi uliopangwa, kwa kufika pa wakati kwenye mikutano kwa ajili ya utumishi, na kwa kuondoka ili kwenda katika eneo bila kukawia. Tungepaswa kuwa wenye kuhubiri badala ya kukawia kwenye mkutano kwa ajili ya utumishi. Kwa kuwa Yehova ametufundisha kwamba “kwa kila kitu kuna majira yake,” tunahitaji kutumia kwa matokeo kweli kweli wakati tulioweka kando kwa ajili ya huduma.—Mhu. 3:1.
2 Panga Wakati Wako kwa Hekima: Baraka nyingi zinatujia wakati tunaposhikamana kwa uthabiti na programu inayofanya iwezekane kwetu kushiriki kikawaida katika huduma ya shambani. Kwa kawaida, matokeo mazuri tunayoyapata katika huduma yangepaswa kulingana na kiasi cha wakati tunachopitisha katika utumishi. Kwa kufanya marekebisho madogo kwenye programu yetu, je! tungeweza kutoa wakati zaidi katika utumishi wa shambani? Kwa mfano, baada ya utendaji wa kugawa magazeti Siku ya Posho, je! tungeweza kuchukua wakati fulani wa ziada ili kufanya ziara za kurudia? Ikiwa tumekuwa katika huduma ya shambani kwa wakati fulani Siku ya Yenga, je! tungeweza kupitisha wakati fulani pia kwa kufanya ziara za kurudia na kuongoza funzo la Biblia? Je! ingewezekana kuongeza ushahidi fulani wa barabarani kwenye utendaji wa nyumba kwa nyumba? Katika njia hizo au nyinginezo, tungeweza kufanya utumishi wetu uwe bora zaidi.
3 Tunapokuwa katika huduma, tunaweza kupoteza wakati wenye thamani ikiwa sisi si waangalifu. Bila shaka, hali za hewa zinapokuwa mbaya, pumziko fupi litatuburudisha na kutusaidia tuendelee. Hata hivyo, iweni wenye usawaziko, kwa kuwa mapumziko kama hayo huenda yasiwe ya lazima kila wakati.
4 Katika miaka ya juzijuzi, imekuwa vigumu zaidi na zaidi kuwakuta watu nyumbani. Ili kushindana na hali hiyo, wahubiri wengi hutoa ushahidi wa nyumba kwa nyumba pa wakati tofauti-tofauti wa siku. Kwa nini usijaribu kutoa ushahidi nyuma kisha saa nane ya mchana au mwanzoni mwa jioni?
5 Ingekuwa vizuri zaidi ikiwa hatuongei-ongei tunapofanya kazi ya barabarani. Badala yake, iweni kila mmoja mbali na mwenzake, na karibieni watu ili kuanzisha mazungumzo pamoja nao. Hivyo, wakati utapangwa kwa matokeo zaidi na furaha kubwa itatokana na kazi.
6 Chukua Nafasi Zote ili Kutoa Ushahidi: Wakati mwanamke mwenye nyumba aliposema kwamba hakuwa mwenye kupendezwa, Shahidi mmoja alimwuliza ikiwa kulikuwa mtu mwingine katika nyumba ambaye angeweza kuongea naye. Hilo liliongoza kwenye mazungumzo pamoja na mwanamume mwenye nyumba, ambaye alikuwa amekuwa mgonjwa kwa miaka mingi na alifungwa sana kwenye kitanda. Tumaini linaloonyeshwa katika Neno la Mungu lilifanya upya kupendezwa kwake na maisha. Bado kidogo yeye alipona, akawa mwenye kuhudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme na kushiriki na wengine tumaini lake alilotoka kupata!
7 Dada mmoja tineja alitumia dokezo la kujitoa katika utumishi wa shambani muda wa saa inayotangulia Funzo la Kitabu la Kutaniko. Kwenye mlango wake wa kwanza, yeye alikuta binti mwenye umri wa miaka 13 ambaye alisikiliza kwa makini na kuchukua vichapo. Yule dada mchanga alimkuta binti yule yule kwenye shule siku iliyofuata. Upesi baadaye, dada alipendekeza kujifunza Biblia pamoja naye, na binti yule alikubali.
8 Fanya Huo Uwe Wakati Bora: Kushiriki kikawaida katika utumishi wa shambani hutusaidia tusitawishe ustadi wetu katika kutoa habari njema. Je! unaweza kufanya uwezo wako wa kuanzisha mazungumzo kwenye mlango uwe bora kwa kutumia utangulizi wenye matokeo zaidi? Je! ungeweza kuwa mwalimu mwenye ustadi zaidi unapoongoza funzo la Biblia la nyumbani? Kwa kufanya hivyo, unaweza kutumia kwa matokeo kweli kweli wakati wako katika utumishi na kufanya huduma yako iwe yenye kuzaa matunda zaidi na zaidi.—1 Tim. 4:16.
9 Kwa kuwa “wakati ubakio umepunguzwa,” maisha yetu yangepaswa kujazwa kazi za Kikristo. (1 Kor. 7:29) Kutoa wakati kwa ajili ya utendaji wa kuhubiri kungepaswa kuwa ndilo jambo letu kubwa la kutanguliza mbele. Acheni tushiriki kwa kiasi kikubwa na kwa bidii katika huduma. Wakati ni mali ya ajabu ambayo Yehova ametutolea. Utumieni sikuzote kwa hekima na kwa matokeo.
[Box on page 4]
Fikiria Madokezo Yafuatayo:
◼ Fikeni pa wakati kwenye mikutano kwa ajili ya utumishi.
◼ Kwa akili, fanyeni vikundi vyenye kutoa ushahidi viwe vidogo-vidogo.
◼ Epukeni kukawia mnapokwenda katika eneo.
◼ Fanyeni kazi katika eneo wakati ambapo watu wengi zaidi hupatikana nyumbani.
◼ Mara kwa mara, tumikeni wenyewe ikiwa ni salama kufanya hivyo.
◼ Fanyeni ziara za kurudia karibu zaidi na eneo la mahubiri ya nyumba kwa nyumba.
◼ Endeleeni kuwa na shughuli katika utumishi wakati wengine wanapochelewa kwenye mlango.
◼ Ikiwa inawezekana, kulingana na hali, bakieni katika mahubiri kwa zaidi ya saa mmoja.