Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/09 uku. 6-7
  • Mikutano kwa Ajili ya Mahubiri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mikutano kwa Ajili ya Mahubiri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mukutano kwa Ajili ya Mahubiri Wenye Kutimiza Kusudi Lake
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Kufaidika Kabisa na Mikutano kwa Ajili ya Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Namna ya Kufaidika na Kikundi Chenu cha Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Kisanduku Cha Maulizo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2009
km 8/09 uku. 6-7

Mikutano kwa Ajili ya Mahubiri

1. Kwa nini jambo la kuhubiri kwa utaratibu linatuhusu?

1 Yesu alituwekea mfano mzuri ili kufanya kazi ya kuhubiri Ufalme kwa utaratibu na kwa njia yenye matokeo. Leo pia, wale walio na daraka la kuongoza kazi ya kuhubiri Ufalme ulimwenguni pote wanapenda kuona kazi hiyo ikifanywa kwa utaratibu na kwa njia yenye matokeo. Vivyo hivyo, makutaniko ulimwenguni pote yanajikaza kutumia mikutano kwa ajili ya mahubiri kuwa njia ya kutayarisha vikundi vya wahubiri wa Ufalme ili kufanya mahubiri kwa utaratibu.—Mt. 24:45-47; 25:21; Luka 10:1-7.

2. Mikutano kwa ajili ya mahubiri itafanywa namna gani?

2 Mupange Mambo Vizuri: Mikutano kwa ajili ya mahubiri inawatolea wale wanaojitayarisha kuhubiri vitia-moyo, maagizo kuhusu namna ya kuhubiri, na mwongozo wa kufuata. Andiko la siku linaweza kuzungumziwa kwa kifupi ikiwa linapatana na kazi ya kuhubiri. Nyakati nyingine, mawazo kutoka Huduma Yetu ya Ufalme, kitabu Kutoa Sababu ao labda kitabu Shule ya Huduma, yanaweza kutumiwa ili kuwatayarisha wote watakaohubiri siku hiyo. Munaweza kufanya onyesho fupi kuhusu kichapo kinachotumiwa kuwa toleo la mwezi. Mbele ya kutoa sala, kila mutu anapaswa kujua atatumika na nani katika mahubiri na ni wapi eneo atakalotumikia linapatikana. Kisha tu kumaliza mkutano huo ambao hautapitisha dakika 15, wote watajielekeza kwenye eneo.

3. Ni nani walio na daraka la kuchukua mipango kuhusu mikutano kwa ajili ya mahubiri?

3 Mikutano Hiyo Inapangwa Namna Gani? Mwangalizi wa utumishi, ndiye ana daraka la kuchukua mipango kuhusu mikutano kwa ajili ya mahubiri. Waangalizi wa vikundi ao wasaidizi wao, wana daraka la kuhubiri pamoja na vikundi vyao vya mahubiri Siku ya Posho na Siku ya Yenga. Wazee na watumishi wa huduma wengine wanaweza kuongoza vikundi vya mahubiri katikati ya juma. Waangalizi wa vikundi watashirikiana na mwangalizi wa utumishi ili kupata maeneo ya kutosha ya kuhubiria nyumba kwa nyumba Siku ya Posho na Siku ya Yenga. Katika juma, mwangalizi wa utumishi atahakikisha kwamba mipango iliyochukuliwa kuhusu wale watakaoongoza vikundi katika mahubiri inafuatwa.

4-6. (a) Mikutano kwa ajili ya mahubiri ina kusudi gani kuhusiana na eneo la kutaniko? (b) Ni mambo gani yanayopaswa kufikiriwa ili kujua mambo yanayohitajiwa kuhusiana na mikutano kwa ajili ya mahubiri?

4 Mikutano kwa Ajili ya Mahubiri Itaongozwa Wapi na Wakati Gani? Kuliko kutaniko nzima kukutana nafasi moja, kwa kawaida, itakuwa vizuri mikutano kwa ajili ya mahubiri ifanywe mahali mbalimbali katika eneo lote, kwa kawaida katika nyumba za ndugu, ili kuhubiria watu wa eneo kwa matokeo. Mikutano hiyo inaweza kufanywa pia katika Majumba ya Ufalme. Makutaniko mengi yanafanya mkutano kwa ajili ya mahubiri katika Jumba la Ufalme Siku ya Yenga kisha tu hotuba ya watu wote na funzo la Mnara wa Mlinzi. Tujikaze ili mikutano hiyo isifanywe mbali na eneo. Kwa hiyo, mara kwa mara, uchunguzi unapaswa kufanywa kuhusu mahali ambapo mikutano hiyo itafanywa na kuhakikisha kwamba mahali hapo panafaa kabisa ili kuhubiri eneo kwa ukamili na kwa njia yenye matokeo.

5 Ili kujua wakati unaofaa zaidi kwa ajili ya mikutano hiyo, na ikiwa itafanywa mara ngapi kwa juma ao mara ngapi kwa siku, hilo litatokana na hali ya eneo. Maulizo yafuatayo yanaweza kuwasaidia kujua wapi na wakati gani mikutano hiyo inaweza kufanywa kwa njia inayofaa zaidi.

6 Ni eneo gani linalopaswa kuhubiriwa zaidi? Ni wakati gani unaofaa zaidi kuhubiri nyumba kwa nyumba? Je, mnaweza kupanga kuhubiri nyumba kwa nyumba ao kurudilia watu wakati wa magaribi? Mipango yote inayohusu mikutano kwa ajili ya mahubiri inapaswa kuwekwa kwenye ubao wa matangazo. Nia ya kila mhubiri wa Ufalme inapaswa kuwa kuhubiri eneo lote alilogawiwa hivi kwamba anaweza pia kusema kama mtume Paulo: “Sina tena eneo lisiloguswa.”—Rom. 15:23.

7. Yule atakayeongoza mkutano kwa ajili ya mahubiri ana daraka gani?

7 Namna ya Kuongoza Mikutano kwa Ajili ya Mahubiri: Yule atakayeongoza mkutano kwa ajili ya mahubiri ataonyesha kwamba anaheshimu kabisa mpango huu wa kitheokrasi kwa kujitayarisha vizuri. Mikutano hiyo itaanza pa wakati na itakuwa yenye kujenga na fupi, ikichukua dakika 10 ao 15. Mbele ya kufanya mkutano, mwenye kuongoza anapaswa kujua eneo litakalohubiriwa. Hata ikiwa si lazima kungojea wale wanaochelewa, mbele ya kuondoka ni vizuri kuacha habari ili wajue mahali ambapo kikundi kitahubiri, jambo hilo linaweza kuwasaidia. Kisha tu mkutano huo, wote watajielekeza mara moja kwenye eneo walilogawiwa bila kuchelewa. Bila shaka, mkutano unaopangwa vizuri na wenye kujenga, utawatolea wale waliohuzuria muongozo unaofaa ili kutimiza utumishi wao siku hiyo.—Met. 11:14.

8. Ni katika njia gani wale wanaohuzuria mikutano kwa ajili ya mahubiri wanaweza kuunga mkono wale wanaoongoza?

8 Kuhuzuria Mikutano kwa Ajili ya Mahubiri: Ni jambo la lazima kuungana mkono. (Ebr. 13:17) Inapohitajiwa, ndugu anayeongoza kikundi atasaidia kila mutu apate yule atakayehubiri naye. Ni vizuri wahubiri wenye uzoefu wawe hapo ili wawasaidie wapya na wale wasio na uzoefu. Wale wanaohubiri mara kwa mara na mhubiri tofauti, wanaweza kutimiza kazi nzuri kabisa. (Met. 27:17; Rom. 15: 1, 2) Kila mutu atajikaza kufika pa wakati. Kwa kuheshimu mpango huo wa kitheokrasi na kufikiria ndugu na dada zetu, hilo litatuchochea kufanya mabadiliko yanayohitajiwa ili kuhuzuria mikutano hiyo.—2 Kor. 6:3, 4; Flp. 2:4.

9. Ni katika njia gani ya maana mapainia wanaweza kuunga mkono mikutano kwa ajili ya mahubiri?

9 Msaada wa Mapainia: Mapainia wanapohuzuria mikutano kwa ajili ya mahubiri, hilo linapendeza sana na kutia wote moyo. Kwa kweli, mapainia wana kazi nyingi. Zaidi ya kuongoza mafunzo ya Biblia, kurudilia watu, programu yao ya kila siku inaweza kutia ndani kushugulikia familia na kazi zao za kimwili. Kwa hiyo, mapainia hawaombwi kabisa kuhuzuria kila mkutano kwa ajili ya mahubiri unaopangwa na kutaniko, hasa ikiwa mkutano huo unafanywa kila siku. Lakini, labda itawezekana mapainia wahuzurie mikutano fulani kwa ajili ya mahubiri kila juma. Kwa kiasi fulani, mikutano kwa ajili ya mahubiri ni nafasi ya kuzoeza washiriki wa kutaniko; na kwa kuwa mapainia wana ujuzi wa Biblia na uzoefu katika mahubiri, wanaweza kuwasaidia wengine kabisa. Kushiriki kwa ukawaida katika mahubiri kumewasaidia wawe na uzoefu mwingi katika mahubiri. Hivyo wanaweza kuwasaidia wengine. Kwa kuwa wanahubiri kwa bidii na kuhuzuria kwa ukawaida mikutano kwa ajili ya mahubiri, wao ni mfano mzuri wa kufuata. Inapendeza sana kuwaona wakishiriki katika mikutano kwa ajili ya mahubiri.

10. Kwa nini ni jambo lenye kufaa kila mhubiri ajikaze kabisa kuhuzuria mikutano kwa ajili ya mahubiri?

10 Kama ilivyokuwa wakati wa Yesu na wanafunzi wake, sehemu kubwa ya kazi yetu ya kuhubiri Ufalme inatimizwa kwa kuhubiri nyumba kwa nyumba. Mikutano kwa ajili ya mahubiri inatutolea nafasi ya kutiana moyo na inatusaidia tupate matokeo mazuri tunaposhiriki katika kazi hiyo. Kila mhubiri wa habari njema anapaswa kuunga mkono mipango hiyo ya kitheokrasi kulingana na uwezo wake. (Mdo. 5:42; 20:20) Basi, kila mmoja wetu na ajikaze kufanya mabadiliko anayohitaji ili kuhuzuria mikutano kwa ajili ya mahubiri. Kwa kufanya hivyo, hakika Yehova atatubariki na tunaweza kufurahisha moyo wa kiongozi wetu Yesu Kristo, tunapohubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu.—Mt. 25:34-40; 28:19, 20.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine