Kufaidika Kabisa na Mikutano kwa Ajili ya Mahubiri
1 Mikutano yenye kufaa kwa ajili ya mahubiri inatutolea vitia moyo na pia maagizo yenye kufaa mbele ya kwenda katika mahubiri. Inatuwezesha kuhubiri pamoja na wengine ili tuungane mkono na kuzoezana. (Met. 27:17; Mhu. 4:9, 10) Tunaweza kufanya nini ili tufaidike kabisa kutokana na mikutano hiyo?
2 Mwenye Kuongoza: Hakuna karatasi (plan) yenye kuonyesha kimbele habari za kuzungumzia kwenye mikutano hiyo. Kwa hiyo, inaomba kujitayarisha vizuri ili kuongoza mkutano huo. Usiwe na zoezi la kuchunguza andiko la siku kila mara unapoongoza mkutano huo, hata hivyo unaweza kuamua kuzungumzia andiko la siku ikiwa linahusiana moja kwa moja na kazi ya kuhubiri. Fikiria mambo yanayoweza kusaidia wale ambao watahubiri siku hiyo. Kwa mfano, unaweza kuzungumzia au kufanya onyesho la namna fulani ya kuhubiri. Unaweza kurudilia habari fulani katika kitabu Kutoa Sababu, kitabu cha Shule ya Huduma au sehemu fulani ya Mkutano wa Utumishi wa hivi karibuni. Nyakati nyingine, unaweza kuzungumzia jinsi ya kushinda upinzani fulani unaoweza kutokea katika eneo lenu, au unaweza kuzungumzia pia jinsi ya kuamsha kupendezwa na kuanzisha mafunzo ya Biblia, zaidi ikiwa wahubiri wengi watarudilia watu. Kuhusu jambo lolote lile utachagua kuzungumzia, jikaze kuwa mchangamfu na mwenye kutia moyo.
3 Anza mkutano pa wakati hata ikiwa unajua kwamba watu fulani watachelewa. Tumia akili nzuri unapogawa watu na uwapatie eneo wale wanaolihitaji. Mkutano huo unapaswa kuchukua dakika 10 mpaka 15 na hata kufupishwa ikiwa unafanywa kisha mkutano wa kutaniko. Mbele ya kumaliza mkutano huo, kila mtu anapaswa kujua mtu ambaye atatumika naye na eneo ambalo watahubiri. Mkutano unapaswa kumalizwa kwa sala.
4 Munaweza Kusaidia: Kama ilivyo kuhusu mikutano ya kutaniko, tunaonyesha kwamba tunamheshimu Yehova na kufikiria watu wengine kwa kufika pa wakati. Shiriki katika mazungumzo. Unaweza kuacha mwenye kuongoza akupatie mtu fulani wa kuhubiri naye au unaweza kufanya mipango na mtu mwingine mbele ya kuanza mkutano kwa ajili ya kuhubiri. Ikiwa unataka kufanya mipango yako mwenyewe, jikaze ‘kupanuka’ kwa kutumika na wahubiri mbalimbali kuliko kuhubiri kila mara na marafiki zako. (2 Kor. 6:11-13) Mkutano unapomalizika, epukeni kubadili mipango iliyochukuliwa na kiongozi, na muondoke mara moja ili kujielekeza kwenye eneo.
5 Mikutano kwa ajili ya mahubiri ina kusudi lilelile kama mikutano mingine ya kutaniko. Inapangwa ili tuweze ‘kufikiriana na kuchocheana katika upendo na matendo mazuri.’ (Ebr. 10:24, 25) Ikiwa tunajikaza ili kufaidika na mikutano hiyo, itatusaidia kutimiza kazi yetu ya kuhubiri, iliyo ‘kazi nzuri’ kweli kweli!
[Maulizo ya Funzo]
1. Namna gani mikutano kwa ajili ya mahubiri inaweza kutusaidia?
2. Ni mambo gani fulani ambayo mwenye kuongoza mkutano kwa ajili ya mahubiri anaweza kuzungumzia?
3. Mkutano kwa ajili ya mahubiri unapaswa kuchukua dakika ngapi, na ni mambo gani yanayopaswa kufanywa munamo dakika hizo?
4. Ni nini kitakachosaidia wote wafaidike na mikutano kwa ajili ya mahubiri?
5. Mikutano kwa ajili ya mahubiri ina kusudi gani?