Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/01 uku. 3
  • Kisanduku Cha Maulizo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kisanduku Cha Maulizo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mukutano kwa Ajili ya Mahubiri Wenye Kutimiza Kusudi Lake
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Kufaidika Kabisa na Mikutano kwa Ajili ya Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Mikutano kwa Ajili ya Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Andiko la Siku Halitachunguzwa Tena Kwenye Mikutano kwa Ajili ya Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 9/01 uku. 3

Kisanduku Cha Maulizo

◼ Ni habari gani zinazopaswa kutolewa kwenye mkutano kwa ajili ya utumishi wa shambani?

Kusudi la mkutano kwa ajili ya utumishi wa shambani ni kutusaidia tukaze uangalifu juu ya utendaji unaofuata​​—huduma. Kwa hiyo, kiongozi anapaswa kujitayarisha vizuri na kuwa tayari kutoa kitu fulani chenye kutia moyo, kilicho wazi, na chenye kutumika. Ikiwa andiko la siku linazungumzia mahubiri moja kwa moja, hilo linaweza kusomwa na kuzungumziwa. Hata hivyo, mkutano unapaswa kukaza uangalifu kwanza juu ya huduma, ukisaidia wote watakaotoka kwenda katika kazi ya kutoa ushahidi wawe tayari zaidi ili kutimiza huduma siku hiyo.​​—2 Tim. 4:5.

Nukta zinazofaa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme zinaweza kuzungumziwa ili kufanya wote wajue toleo la sasa na jinsi ya kulitoa. Siku ya Magazeti, utoaji fulani kutoka katika kisanduku “Tuseme Nini Kuhusu Magazeti” unaweza kufanyiwa onyesho. Kwa ajili ya kampeni nyinginezo, utangulizi mmoja au mawili yanayofaa kwa eneo la kutaniko yanaweza kukaziwa kutoka katika kitabu Kutoa Sababu. Sehemu fulani ya huduma inaweza kuzungumziwa au kufanyiwa onyesho, kama vile jinsi ya kutumia Biblia kwenye mlango, jinsi ya kushughulikia kizuia-mazungumzo kinachoweza kutokea, jinsi ya kutolea mtu funzo la Biblia, au jinsi ya kufuatia kupendezwa.

Mikutano kwa ajili ya utumishi haipaswi kuzidi dakika 10 mpaka 15, kutia ndani kupanga wahubiri, kugawa eneo, na kutoa sala. Wakati wanaporuhusiwa kwenda, kila mmoja aliyeko anapaswa kujua mahali na mtu ambaye atatumika naye, na wanapaswa kwenda hapohapo katika eneo. Kwa kuwa mkutano ni mfupi, ni jambo la maana kwamba wote wafike pa wakati. Mkutano kwa ajili ya utumishi unapaswa kuwa mfupi zaidi wakati unapofuata mkutano wa kutaniko, kama vile Funzo la Mnara wa Mlinzi. Si lazima kuzungumzia andiko la siku, kwa kuwa mazungumzo mazuri ya Kimaandiko yamekwisha kufurahiwa.

Ndugu wenye kustahili na wenye kubatizwa wanapaswa kupewa kimbele mgawo wa kuongoza kila mkutano kwa ajili ya utumishi. Ikiwa hakuna ndugu mwenye kustahili na mwenye kubatizwa anayepatikana ili kuchukua uongozi siku fulani hasa, wazee wanapaswa kuchagua akina dada wenye kubatizwa wanaoweza kufanya hivyo wakati uhitaji unapotokea. Dada aliyechaguliwa anaweza kuanzisha mazungumzo ya kikundi ya andiko la siku au nukta zingine zinazohusiana na utumishi wa shambani, akibaki mwenye kukaa na akifanya maneno yake yawe mafupi. Atavaa kitambaa cha kufunika kichwa.

Mikutano kwa ajili ya utumishi wa shambani ni nafasi bora za kutiwa moyo na kutolewa vifaa ili kushiriki katika huduma. Ikiwa kiongozi anajitayarisha vizuri, wote watafaidika zaidi.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine