Mukutano kwa Ajili ya Mahubiri Wenye Kutimiza Kusudi Lake
1. Mukutano kwa ajili ya mahubiri una kusudi gani?
1 Siku moja, Yesu alifanya mukutano pamoja na wanafunzi wake 70 mbele waende katika mahubiri. (Luka 10:1-11) Aliwatia moyo kwa kuwakumbusha kwamba hawatakuwa peke yao, lakini wataongozwa na Yehova, “Bwana wa mavuno.” Aliwatolea pia maagizo ili kuwazoeza, na aliwapanga “wawili-wawili.” Leo pia, mukutano wenye tunafanya mbele ya kuenda katika mahubiri una kusudi ileile—unatutia moyo, unatuzoeza, na kutupanga kwa ajili ya mahubiri.
2. Mukutano kwa ajili ya mahubiri unapaswa kuchukua dakika ngapi?
2 Mupaka sasa, mukutano kwa ajili ya mahubiri unachukua dakika 10 mupaka 15; dakika hizo zinatumiwa pia ili kupanga wahubiri, kugawa eneo, na kusali. Sasa, mupango huo umebadilishwa. Kuanzia Mwezi wa 4, mukutano kwa ajili ya mahubiri utachukua tu dakika 5 mupaka 7. Lakini, kama unafanywa kisha mukutano mwingine wa kutaniko, mukutano kwa ajili ya mahubiri unapaswa kuwa mufupi zaidi, kwa sababu tayari wahubiri wametoka kufurahia mazungumuzo mazuri ya Maandiko. Mukutano mufupi kwa ajili ya mahubiri utawezesha wahubiri wote kupitisha wakati zaidi katika mahubiri. Tena, kama mapainia ao wahubiri fulani walianza kuhubiri mbele ya mukutano kwa ajili ya mahubiri, watahitaji kukatisha mahubiri kwa dakika chache tu.
3. Namna gani mukutano kwa ajili ya mahubiri unapaswa kupangwa ili wahubiri wafaidike sana?
3 Mukutano kwa ajili ya mahubiri unapaswa kupangwa ili wahubiri wafaidike sana. Katika makutaniko mengi, ni muzuri kwa vikundi vya mahubiri kukutana nafasi mbalimbali kuliko kukutana nafasi moja. Hilo linaweza kufanya iwe mwepesi kwa wahubiri kuenda kwenye mukutano kwa ajili ya mahubiri na pengine katika eneo la mahubiri. Linasaidia pia waangalizi wa vikundi wapange mbiombio wahubiri wa vikundi vyao na wawahangaikie sana. Baraza la wazee linaweza kuamua jambo la kufanya kulingana na hali ya eneo la kutaniko. Mbele ya kumaliza mukutano huo kwa sala fupi, kila muhubiri anapaswa kujua atahubiri wapi na atahubiri na nani.
4. Sababu gani mukutano kwa ajili ya mahubiri haupaswe kuonwa kuwa wa maana kidogo kuliko mikutano mingine ya kutaniko?
4 Mukutano Huo Ni wa Maana Kama Vile Mikutano Mingine ya Kutaniko: Kwa sababu mukutano kwa ajili ya mahubiri unafanywa kwa faida ya wahubiri wenye wataenda katika mahubiri, si lazima kutaniko nzima likuwe katika mukutano huo. Hata hivyo, hilo halimaanishe kama tunapaswa kuuzarau ao kuuona kuwa wa maana kidogo kuliko mikutano mingine ya kutaniko. Kama vile mikutano mingine, mukutano kwa ajili ya mahubiri ni mupango wa Yehova wenye unatusaidia kuchocheana katika upendo na matendo mazuri. (Ebr. 10:24, 25) Kwa hiyo, kiongozi anapaswa kujitayarisha muzuri ili mazungumuzo yamutukuze Yehova na wahubiri wafaidike. Ikiwezekana, wahubiri wenye wataenda katika mahubiri wanapaswa kujikaza kuwa katika mukutano huo.
Hatupaswe kuzarau mukutano kwa ajili ya mahubiri ao kuuona kuwa wa maana kidogo kuliko mikutano mingine ya kutaniko
5. (a) Namna gani mwangalizi wa utumishi anapaswa kupanga mukutano kwa ajili ya mahubiri? (b) Wakati gani na namna gani dada anaweza kuongoza mukutano kwa ajili ya mahubiri?
5 Namna Kiongozi Anapaswa Kujitayarisha: Ili ndugu ao dada fulani ajitayarishe muzuri kwa ajili ya mugawo fulani kwenye mukutano wa kutaniko, anapaswa kupewa mugawo huo mbele ya wakati. Ni vile pia kuhusu mikutano kwa ajili ya mahubiri. Ni kweli kwamba, wakati vikundi vya mahubiri vinakutana nafasi tofauti-tofauti, ni waangalizi wa vikundi vya mahubiri ao wasaidizi wao ndio wanaongoza mukutano wa kikundi chao. Lakini, wakati kutaniko nzima linakutana pamoja kwa ajili ya mahubiri, mwangalizi wa utumishi atachagua ndugu fulani aongoze mukutano huo. Waangalizi fulani wa utumishi wanafanya programu ya kuongoza mukutano kwa ajili ya mahubiri, wanaletea kila kiongozi kopi ya programu hiyo na kuweka kopi ingine kwenye ubao wa matangazo. Mwangalizi wa utumishi atatumia akili nzuri wakati anawachagua viongozi; asisahau kwamba uzuri wa mukutano huo unategemea ufundi wa kufundisha na wa kupanga mambo wa viongozi hao. Kama hakuna muzee, mutumishi wa huduma ao ndugu mwengine aliyebatizwa mwenye iko tayari kuongoza siku fulani, mwangalizi wa utumishi atapatia mugawo huo dada mwenye kubatizwa na mwenye kustahili.—Soma habari “Wakati Dada Ndiye Ataongoza.”
6. Sababu gani ni jambo la maana mwenye amepewa mugawo wa kuongoza mukutano wa mahubiri ajitayarishe muzuri?
6 Wakati tunapewa mugawo kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi ao Mukutano wa Utumishi, tunachukua mugawo huo kwa uzito na tunautayarisha muzuri. Hatutangoja wakati wa kuenda kwenye mikutano uenee ili tuanze kuwaza mambo yenye tutasema. Ni vile tunapaswa kuona pia mugawo wa kuongoza mukutano kwa ajili ya mahubiri. Kwa kuwa sasa mukutano kwa ajili ya mahubiri utakuwa mufupi, inaomba kutayarisha muzuri mukutano huo ili wahubiri wafaidike nao na uishe kwa wakati. Kujitayarisha muzuri kunamaanisha pia kupata eneo mbele ya wakati.
7. Kiongozi anaweza kuzungumuzia mambo gani?
7 Mambo ya Kuzungumuzia: Kwa kuwa hali za eneo zinatofautiana, mutumwa mwaminifu hakutayarisha plan ya kila mukutano kwa ajili ya mahubiri. Kisanduku chenye kichwa “Wakati wa Mukutano kwa Ajili ya Mahubiri, Munaweza Kuzungumuzia” kinatoa mapendekezo fulani. Kwa kawaida, mukutano huo utafanywa kama mazungumuzo. Wakati fulani, munaweza kufanya pia onyesho lenye kutayarishwa muzuri ao kuona video fulani yenye kufaa kutoka jw.org. Wakati kiongozi anatayarisha mukutano kwa ajili ya mahubiri, anapaswa kufikiria mambo yenye yanaweza kuwatia moyo na kuwatayarisha wenye wataenda katika mahubiri siku hiyo.
Wakati kiongozi anatayarisha mukutano kwa ajili ya mahubiri, anapaswa kufikiria mambo yenye yanaweza kuwatia moyo na kuwatayarisha wenye wataenda katika mahubiri siku hiyo
8. Inaweza kuwa muzuri sana kuzungumuzia mambo gani kwenye mukutano kwa ajili ya mahubiri Siku ya Posho na Siku ya Yenga?
8 Kwa mufano, Siku ya Posho, wahubiri wengi wanawatolea watu Munara wa Mulinzi na Amuka! Wahubiri wengi wenye kuhubiri Siku ya Posho hawahubiri katikati ya juma, kwa hiyo wanaweza kuwa wamesahau mapendekezo kuhusu namna ya kuwatolea watu magazeti yenye walifanyia mazoezi kwenye Ibada yao ya Familia ya mangaribi. Ili kuwasaidia, kiongozi anaweza kurudilia moja ya namna mbalimbali za kuanzisha mazungumuzo kwenye ukurasa wa mwisho wa Huduma Yetu ya Ufalme. Anaweza pia kuzungumuzia namna ya kuwatolea watu magazeti kwa kutumia habari mbalimbali zenye kuzungumuziwa katika eneo, ao sikukuu fulani; ao anaweza tena kuzungumuzia namna ya kutayarisha musikilizaji kwa ajili ya kumurudilia kama anakubali magazeti. Kama wahubiri fulani wamekwisha kutolea watu magazeti fulani ya mwezi, kiongozi anaweza kuwaomba waeleze kwa kifupi namna gani walifanya na matokeo gani mazuri walipata. Siku ya Yenga, kiongozi anaweza kuamua kufanya hivyo kuhusu vichapo vya kuwatolea watu katika mwezi. Kwa sababu vichapo vya funzo kama vile broshua Habari Njema na Umusikilize Mungu na kitabu Biblia Inafundisha vinaweza kutolewa kila siku, kiongozi wa mukutano kwa ajili ya mahubiri anaweza kuzungumuzia kwa kifupi namna ya kuwatolea watu vichapo hivyo.
9. Kama kutaniko linafanya kampanye fulani ya pekee, kiongozi anaweza kuzungumuzia mambo gani Siku ya Posho na Siku ya Yenga?
9 Kama kutaniko linafanya kampanye fulani ya pekee, Siku ya Posho na Siku ya Yenga kiongozi anaweza kuzungumuzia namna ya kuwatolea watu magazeti ya sasa pamoja na mwaliko ao trakte ya kampanye, ao anaweza kuzungumuzia jambo la kufanya kama musikilizaji anapendezwa. Anaweza pia kuzungumuzia mambo yenye wahubiri fulani walikutana nayo yenye kuonyesha faida ya kampanye kama hiyo.
10, 11. Sababu gani ni lazima wahubiri wajitayarishe ili mukutano kwa ajili ya mahuriri ufanyike muzuri?
10 Namna Wahubiri Wanapaswa Kujitayarisha: Wahubiri pia wana jambo la kufanya ili mukutano kwa ajili ya mahubiri ufanyike muzuri. Kama wanajitayarisha mbele ya wakati, kwa mufano kwenye ibada yao ya familia, watakuwa na mambo ya kusaidia nayo wahubiri wengine. Kujitayarisha muzuri kunamaanisha pia kupata magazeti na vichapo vya kutumia mbele ya kuja kwenye mukutano kwa ajili ya mahubiri ili kisha mukutano wahubiri waende katika eneo bila kuchelewa.
11 Ni jambo la maana pia kupanga kufika kwenye mukutano kwa ajili ya mahubiri dakika fulani mbele uanze. Ni kweli kwamba tunajikaza kufika kwa wakati kwenye mikutano yote ya kutaniko. Hata hivyo, tunaweza kuvuruga mambo kama tunachelewa zaidi sana kwenye mukutano kwa ajili ya mahubiri. Namna gani? Kiongozi wa mukutano huo anafikiria mambo fulani mbele awapange wahubiri. Kama wahubiri wachache tu ndio wanafika, anaweza kuamua kuwatuma wote katika eneo lenye limehubiriwa kidogo. Kama wahubiri fulani walikuja kwa miguu, na kama eneo liko mbali, kiongozi anaweza kuwapanga wahubiri hao pamoja na wenye kuwa na motokari. Kama eneo lenye litahubiriwa halina usalama, kiongozi anaweza kupanga ndugu wahubiri pamoja na dada ao karibu-karibu nao. Wahubiri wenye ulemavu wanapaswa kupewa eneo lenye kuwa na barabara za muzuri ao zenye kuwa na nyumba zenye hazina vipandio (escaliers) vingi. Wahubiri wapya wanaweza kupangwa na wahubiri wenye uzoefu zaidi. Lakini, kama wahubiri wanachelewa, kiongozi atalazimika kupanga tena watu ili wenye kuchelewa wapate watu wa kustahili kuhubiri nao. Ni kweli kwamba, hali fulani zinaweza kutulazimisha kuchelewa kwenye mukutano kwa ajili ya mahubiri. Lakini, kama tunazoea kuchelewa, inaweza kuwa alama ya kuonyesha kama hatuone mikutano kwa ajili ya mahubiri kuwa ya maana sana ao kama tunashindwa kupanga mambo yetu mbele ya wakati.
12. Kama unazoea kupanga kuhubiri na marafiki zako, ni muzuri ufanye nini?
12 Inawezekana wahubiri wakuje kwenye mukutano kwa ajili ya mahubiri wakiwa tayari wamepanga kuhubiri pamoja, ao muhubiri fulani anaweza kuwa amepewa mutu wa kuhubiri naye. Kama unazoea kujitafutia mutu wa kuhubiri naye, ni muzuri ‘upanuke’ kwa kuhubiri na wahubiri mbalimbali kuliko kuhubiri na marafiki zako kila wakati. (2 Kor. 6:11-13) Ni muzuri wakati fulani kupanga kuhubiri na muhubiri mupya ili umusaidie kukomalisha ufundi wake wa kuhubiri. (1 Kor. 10:24; 1 Tim. 4:13, 15) Sikiliza muzuri maagizo yenye munapewa na maagizo kuhusu nafasi mutaanzia kuhubiri. Wakati mukutano kwa ajili ya mahubiri unaisha, tafazali usibadilishe mutu mwenye walikupatia ili kuhubiri naye na muende katika eneo bila kuchelewa.
13. Mukutano kwa ajili ya mahubiri utatuletea faida gani kama kila mutu anatimiza muzuri sehemu yake?
13 Kisha kuhubiri, wanafunzi 70 wenye Yesu alituma katika mahubiri walirudia na furaha. (Luka 10:17) Bila shaka, mukutano wenye Yesu alifanya pamoja nao mbele waende uliwasaidia sana kupata matokeo mazuri. Leo pia, mikutano kwa ajili ya mahubiri inaweza kuwa na matokeo kama hayo. Kama kila mutu anatimiza muzuri sehemu yake, mukutano kwa ajili ya mahubiri utatutia moyo, utatutayarisha, na utatupanga ili tutimize kazi yetu ya kutoa “ushahidi kwa mataifa yote.”—Mat. 24:14.