Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/98 uku. 3-6
  • Tuwe Wenye Matokeo Katika Huduma Yetu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuwe Wenye Matokeo Katika Huduma Yetu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Njia Mbalimbali za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Faida ya Kuwa na Eneo lako Mwenyewe
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Tumia Wakati Wako kwa Matokeo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Namna ya Kuwatendea Wengine Katika Mahubiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 11/98 uku. 3-6

Tuwe Wenye Matokeo Katika Huduma Yetu

1 Anga latiwa giza, sauti yenye kutia hofu yaongezeka na kugeuka ngurumo yenye kutia uziwi. Mawingu yaliyo kama moshi yashuka. Hilo ni nini? Jeshi la mamilioni ya nzige wanaokuja kufanya ukiwa kamili katika nchi! Tamasha hii inayoelezwa na nabii Yoeli inatimizwa leo katika kazi ya kuhubiri wanayofanya watumishi wa Mungu waliotiwa mafuta na wenzi wao, umati mkubwa.

2 Mnara wa Mlinzi wa Mei 1, 1998, ukurasa 11, fungu 19, ulitaarifu: “Jeshi la nzige wa Mungu wa siku ya kisasa wametoa ushahidi kamili katika ‘mji’ wa Jumuiya ya Wakristo. (Yoeli 2:9) . . . Wangali wanapanda vizuizi vyote na kuingia mamilioni ya makao, kuwafikia watu barabarani, kusema nao kwenye simu, na kuwafikia katika njia yoyote iwezekanayo, wajulishapo rasmi ujumbe wa Yehova.” Kushiriki katika kazi hiyo iliyoamuriwa na Mungu, je! hilo si pendeleo kubwa?

3 Kwa kutofautiana na nzige halisi, walio na kusudi tu la kujipatia chakula, sisi watumishi wa Yehova tunapendezwa vilevile na maisha ya wale tunaowahubiria. Tunapenda kusaidia wengine wajifunze kweli zuri mno zinazopatikana katika Neno la Mungu, kisha ziwasukume wapige hatua zitakazowaongoza kwenye wokovu wa milele. (Yn. 17:3; 1 Tim. 4:​16) Kwa hiyo, tunataka kuwa wenye matokeo katika mbinu tunazozitumia tutimize huduma yetu. Hata iweje njia ya kuhubiri tunayoitumia, tunapaswa kuangalia kama tunaitumia kwa namna na kwa wakati vinavyoweza kuzaa matunda bora. Kwa kuwa ‘mandhari (tamasha) ya ulimwengu huu inabadilika,’ tutafanya vema kufikiria njia tunazozitumia na utangulizi wetu ili tuhakikishe kwamba tumeshinda katika kupigania kuwa wenye kuzaa matunda mengi iwezekanavyo.​—1 Kor. 7:​31.

4 Ingawa tunajitahidi kufikia watu kwa nja nyingi, mahubiri ya nyumba kwa nyumba yanabaki nguzo ya huduma yetu. Je! umeona kwamba mara kwa mara watu hawapatikani nyumbani au ni wenye kulala unapowatembelea? Ni jambo la kukatisha tamaa kama nini, kwa kuwa hauwezi kushiriki ujumbe wa habari njema pamoja nao! Tunawezaje kushinda tatizo hilo?

5 Tuwe Wenye Kukubali Hali Mpya na Wenye Usawaziko wa Fikira: Katika Israeli ya karne ya kwanza, wavuvi walivua usiku. Kwa nini? Ingawa huo haukuwa wakati wenye kufaa zaidi kwao, ulikuwa wakati mzuri zaidi wa kunasa samaki wengi. Ulikuwa wakati wenye kuzaa matunda kuliko nyakati nyingine zote. Katika kueleza zoea hilo, Mnara wa Mlinzi wa Juni 15, 1992, ulisema: “Sisi pia twapaswa kuchunguza eneo letu ili twende kuvua, wakati ambao, kwa kweli, watu walio wengi wamo nyumbani na wangeitikia.” Kuchunguza kwa uangalifu mazoea ya watu wanaoishi pambizoni mwa miji mikuu na mitaa inayokaliwa kumeonyesha kwamba wengi labda hupatikana nyumbani kwao mapema Siku ya Posho au Siku ya Yenga asubuhi, lakini kwa kawaida hawako tayari kusikiliza wakati huo. Ikiwa hivyo ndivyo ilivyo katika eneo letu, je! hatuwezi kurekebisha wakati wa ziara zetu na kuzifanya mchana, au hata alasiri? Hiyo ni njia nzuri ya kufanya huduma yetu iwe yenye matokeo zaidi na kuwa wenye kufikiria jirani zetu, jambo ambalo ni alama ya upendo wa kweli wa Kikristo.​—Mt. 7:​12.

6 Kwenye Wafilipi 4:5, mtume Paulo atukumbusha kwamba tunapaswa kufanya ‘hali yetu ya kukubali sababu ijulikane kwa watu wote.’ Kwa kupatana na mwongozo huo uliopuliziwa na Mungu, tunaweza kuwa na usawaziko wa fikira katika njia tunazozitumia kadiri tunavyotimiza mgawo wetu wa kuhubiri kwa bidii na shauku. Hatutaki ‘tuepuke kufundisha hadharani na kutoka nyumba hadi nyumba,’ lakini tunataka kuhakikisha kwamba tunatimiza huduma yetu ya nyumba kwa nyumba kwa nyakati zenye kufaa na zenye kuzaa matunda. (Mdo. 20:20) Kama wale wavuvi katika Israeli ya karne ya kwanza, hatupendi ‘kuvua’ pa nyakati zinazoonekana zenye kufaa zaidi kwetu, bali, badala yake, pa nyakati ambapo twaweza kuwa wenye matokeo.

7 Ni marekebisho gani yangeweza kufanywa? Mara nyingi, mikutano kwa ajili ya utumishi wa shambani hufanywa pa saa 3:00 au saa 3:30 asubuhi Siku ya Posho au Siku ya Yenga; baadaye, kikundi hicho huanza papo hapo mahubiri ya nyumba kwa nyumba katika eneo. Kwa kuwa mambo yako hivyo, mabaraza fulani ya wazee yamefanya mipango ili kikundi hicho kishiriki katika aina nyingine za huduma, kama vile mahubiri ya barabarani, eneo la biashara, au ziara za kurudia, kabla ya kwenda nyumba kwa nyumba katika maeneo yanayokaliwa. Makutaniko mengine yamepanga nyakati za mikutano kwa ajili ya utumishi wa shambani mchana​—saa 4:00, saa 5:00, au saa 6:00. Baadaye, kikundi hicho huenda moja kwa moja katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba na kubaki katika utumishi hadi kwenye mwanzo wa alasiri. Katika maeneo fulani, mwanzo wa alasiri, si asubuhi, waweza kuwa wakati bora zaidi wa kukutana kwa ajili ya utumishi wa shambani. Marekebisho kama hayo yaweza kuchangia sana kuongeza matokeo katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba.

8 Tuwe Wenye Utambuzi na Wenye Busara: uniquement Français Watu tunaokutana nao kutoka nyumba hadi nyumba huitikia ujumbe wetu kwa njia tofauti-tofauti. Baadhi yao ni wasikivu, wengine ni wasiojali, na wachache huenda ni wabishi au wagomvi. Kuhusu hao wa mwisho, kitabu Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko, kwenye ukurasa 7, chatukumbusha kwamba “hatutaki kupata ushindi kwa kubishana na watu wasioonyesha staha kuelekea ukweli.” Ikiwa msikilizaji anapinga, ni vizuri kuondoka. Hatupaswi hata kidogo kushindana na watu kwa kusisitiza ili wazungumze nasi au kukubali maoni yetu. Sisi hatuwatolei watu ujumbe kwa nguvu. Hilo halingekuwa jambo la akili na lingeweza kuleta matatizo kwa Mashahidi wengine, au hata kuletea kazi yetu matatizo kwa ujumla.

9 Kabla ya kutembelea eneo, ni jambo la busara kuangalia ikiwa katika mfuko mna maandishi yanayoonyesha anwani ya wenyeji walioomba tusiwatembelee. Ikiwa ipo, tutajulisha kila mhubiri anayehubiri katika barabara hiyo. Hakuna mtu ambaye angepaswa kuchukua hatua ya kukutana na watu hao bila ruhusa ya mwangalizi wa utumishi.​—ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1994. Majibu kwa Maulizo Yenu.

10 Tunaweza kuwa wenye matokeo zaidi ikiwa tunatenda kwa utambuzi tunapohubiri nyumba kwa nyumba. Tuwe wachunguzi tunapokaribia nyumba. Je! madirisha yote na pazia zote ni vyenye kufungwa? Je! hakuna kelele? Je! wakaaji labda ni wenye kulala? Inawezekana kwamba tutakuwa na mazungumzo yenye matokeo wakati ujao. Labda ni vema, kwa sasa, kuacha nyumba hiyo na kuandika namba yake. Tutaweza kurudi kabla ya kuondoka katika eneo au kuandika kwamba inafaa kurudi wakati ujao.

11 Hata hivyo, inaweza kufika kwamba tunaamsha au tunaudhi mtu fulani bila kukusudia. Inaelekea mtu huyo atakasirika. Tutafanya nini? Mezali 17:​27 (UV) lashauri: “Mwenye roho ya utulivu ana [utambuzi].” Hatuombi radhi kwa kuwa tunatimiza huduma yetu, lakini inafaa tuombe radhi kwa kuwa tumepita pa wakati usiofaa. Tunaweza kuuliza kwa adabu ikiwa ingewezekana kurudi pa wakati wenye kufaa zaidi. Meneno ya wema yanayosemwa kwa sauti ya upole hutuliza mara nyingi wasikilizaji wa aina hiyo. (Mez. 15:1) Ikiwa msikilizaji anatuambia kwamba yeye hutumika hadi usiku, tungeweza kuonyesha jambo hilo kwenye maandishi tutakayoacha pamoja na kadi ya eneo, ili atembelewe pa wakati wenye kumfaa katika siku zijazo.

12 Ili kutembelea eneo kikamili, ni jambo la lazima pia kuwa mwenye utambuzi. Kwa kuwa watu wengi hawapatikani nyumbani kwao tunapopita mara ya kwanza, tunapaswa kufanya jitihada za ziada ili kuwatolea ujumbe wa wokovu. (Rom. 10:13) Wakati mwingine inatukia kwamba wahubiri hujaribu mara nyingi katika mchana uleule kukuta watu nyumbani kwao. Jambo hilo huonwa na majirani, ambao wanaweza hivyo kuwa na maoni mabaya kwamba Mashahidi wa Yehova huwa ‘kila wakati kwenye milango ya watu’ mitaani mwao. Tunawezaje kuepuka jambo hilo?

13 Inafaa kuwa wenye utambuzi. tunaporudi kwenye mlango wa mtu asiyekuwako, je! jambo fulani lafanya tufikiri kwamba mwenye nyumba amerudi? Ikiwa barua au vikaratasi vingine vimejaa na kutoka nje katika kisanduku cha barua (ikiwa kipo), ni kusema kwamba labda hakujafika mtu, na lingekuwa jambo lisilofaa kupiga tena kwenye mlango. Ikiwa hatukumkuta mtu huyo baada ya majaribio mengi yaliyofanywa pa nyakati tofauti-tofauti za mchana, kutia ndani jioni, tutaweza kumpigia simu. Ikiwa haiwezekani, tuache kwa siri trakti au kikaratasi cha mwaliko kwenye mlango, zaidi ikiwa ni eneo linalotembelewa mara nyingi. Inawezekana kumkuta mtu huyo wakati ujao eneo hilo litakapotembelewa.

14 Tungepaswa kuepuka kuzungumza sana kwenye mlango wa nyumba ikiwa jambo hilo linamfanya msikilizaji apatwe na baridi. Tunapoalikwa kuingia, tuwe waangalifu tusichafue sakafu. Tuwe wenye akili wakati mbwa anapobweka kwa sababu yetu. Ikiwa tunahubiri katika jengo kubwa, tuseme kwa sauti ndogo na tuepuke kufanya makelele, jambo ambalo lingeudhi wakaaji na kuwajulisha kuwako kwetu.

15 Tuwe Wenye Utaratibu na Wenye Kuheshimika: Kupitia upangaji mzuri wa mambo, inawezekana kuepuka kufanya vikundi vikubwa vinavyoonekana wazi katika eneo. Watu wangeweza kuwa wenye mashaka kwa kuona magari mengi yakiegeshwa mbele ya nyumba zao na kikundi kikubwa cha wahubiri kikikusanyika hapo. Tunataka kuepuka kufanya watu wafikiri kwamba “tunashambulia” mitaa wanamokaa. Ni vizuri zaidi kujipanga kwenye Jumba la Ufalme, wakati wa mkutano kwa ajili ya mahubiri. Vikundi vidogo-vidogo vya wahubiri, vyenye ukubwa wa familia, haviogopeshi sana wakaaji wa eneo na ni vyepesi zaidi kupanga upya kadiri eneo linavyotembelewa.

16 Utaratibu mzuri waomba wazazi waangalie kwa makini mwenendo wa watoto katika mahubiri. Wanaposindikiza watu wenye umri mkubwa katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba, watoto wangepaswa kuonyesha kwamba wamelelewa vizuri. Hatupaswi kuruhusu watoto wadogo wacheze au kutembea hapa na pale, wakivuta isivyofaa uangalifu wa watu wa mtaa na wa wapita-njia.

17 Inafaa vilevile kuwa na usawaziko kuhusu mapumziko. Ajouté + citation Huduma Yetu ya Ufalme ya Desemba 1995, ukurasa 5, inasema: “Tunaposhiriki katika mahubiri, tunapoteza labda wakati wenye thamani kwa kukatiza ili kupumzika. Hata hivyo, hali ya majira inapokuwa ngumu, pumziko hutuwezesha kupata nguvu mpya na kuendelea na utendaji wetu. Wahubiri wengi hupendelea hata hivyo kuhubiri na hawatumii wakati waliopangia mahubiri kwa kupumzika wakiwa pamoja na ndugu na dada wengine.” Igawa hilo ni swali linalohusu kila mtu binafsi, inaonekana kwamba vikundi vya akina ndugu na dada hukutana kwenye mkahawa. Licha ya wakati unaopitishwa kwa kungoja kuhudumiwa, kuwako kwa kikundi kikubwa kwaweza kuudhi wateja wengine. Wakati mwingine, akina ndugu hueleza kwa sauti kubwa mambo waliyoyafanya katika mahubiri asubuhi, jambo linaloharibu heshima na matokeo ya huduma yetu. Kwa kuonyesha utambuzi, wahubiri wataepuka kusongamana kwa wingi katika nyumba fulani na kupoteza wakati katika mahubiri.

18 Wengi hupata matokeo mazuri kwa kuzungumza na watu mahali pote wanapopatikana: barabarani, kwenye maegesho ya magari na mahali penginepo penye watu wengi. Hapo pia, tunapenda kutoa ushahidi mzuri, si katika maneno tu, bali pia kwa kuwa na usawaziko wa fikira. Wahubiri wa kila kutaniko wanapaswa kuheshimu mipaka ya eneo lao, kusudi wasiudhi watu katika maeneo ya biashara na katika miingilio ya barabara za ardhini, au wafanyakazi wa biashara zenye kufunguliwa mchana na usiku, kama vile vituo vya mafuta ya motokaa. Ili kuhakikisha kwamba tunatimiza huduma yetu kwa utaratibu na heshima, hatutapita mipaka ya eneo letu, isipokuwa mipango ya pekee imefanywa na halmashauri ya utumishi ya kutaniko linalohitaji msaada.​—Ona 2 Wakorintho 10:13-15.

19 Makutaniko mengine yanayo mitaa mingi ambapo inawezekana kutoa ushahidi wa vivi hivi. Hivyo, makutaniko hayo yamekata-kata mitaa hiyo na kuifanya kuwa maeneo. Kadi ya eneo hutolewa kwa mhubiri mmoja au kwa kikundi, jambo linalofanya iwezekane kulitembelea kwa matokeo zaidi na kuepusha wahubiri wengi sana kuhubiri mahali pamoja kwa wakati uleule, kwa kupatana na kanuni inayoonyeshwa kwenye 1 Wakorintho 14:40: “Acheni mambo yote yatukie kwa adabu na kwa mpango.”

20 Kuonekana kwetu kwa nje kunapaswa kuwa sikuzote kwenye kuheshimika na kuonyesha wahudumu wanaochukua jina la Yehova. Jambo hilo liko hivyo pia kuhusu vifaa vyetu. Mifuko mikuukuu na Biblia zenye kuchakaa au zilizo na pembe zenye kukunjama huvunjia heshima ujumbe wa Ufalme. Mtu fulani alisema kwamba mavazi yetu na kujipamba kwetu “huwapa mara moja watu wanaotuzunguka alama ya utambulisho wetu, sifa yetu na nafasi yetu katika utaratibu wa mambo.” Kwa hiyo, mavazi yetu hayapaswi kuwa ya ovyo ovyo wala ya kuchekesha, lakini yawe sikuzote “yenye kustahili habari njema.”​—Ona 1 Timotheo 2:9, 10.

21 Kwenye 1 Wakorintho 9:26, mtume Paulo alisema: “Jinsi ninavyokimbia si bila uhakika; jinsi ninavyoelekeza ngumi zangu ni ili nisiwe nikipiga hewa.” Kwa kuiga Paulo, sisi tunaazimia kuwa wenye matokeo, wenye kuzaa matunda katika huduma yetu. Tukiwa wenye kuhubiri kwa bidii miongoni mwa “jeshi la nzige” la Yehova, na tutoe ujumbe wa wokovu kwa jirani yetu huku tukiwa wenye usawaziko katika fikira na kuwa wenye utambuzi!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine