Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • od sura 8 uku. 71-86
  • Wahubiri wa Habari Njema

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wahubiri wa Habari Njema
  • Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • WAHUBIRI WAPYA
  • MAMBO YENYE KUOMBWA ILI KUWA MUHUBIRI
  • NAMNA YA KUSAIDIA VIJANA
  • KUJITOA KWA MUNGU KATIKA SALA NA KUBATIZWA
  • RIPOTI ZENYE KUONYESHA MAENDELEO YA KAZI YA KUHUBIRI
  • RIPOTI YAKO YA MAHUBIRI
  • FISHE YA MUHUBIRI YA KUTANIKO
  • JUU YA NINI TUNATOAKA RIPOTI YA MAHUBIRI?
  • KUJIWEKEA MIRADI
  • Tutoe Utumishi Mtakatifu Mchana Na Usiku
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Majibu kwa Maulizo Yenu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Iweni Wenye Bidii kwa Lililo Jema!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Aprili—wakati wa ‘kufanya kazi kwa bidii na kujitahidi’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
Ona Habari Zaidi
Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
od sura 8 uku. 71-86

SURA YA 8

Wahubiri wa Habari Njema

YEHOVA alitupatia mufano mukamilifu wa kufuata. Ule mufano ni Mwana wake Yesu Kristo. (1 Pe. 2:21) Wakati mutu anakuwa mufuasi wa Yesu na anaanza kuhubiri habari njema, anakuwa mutumishi wa Mungu. Ili kuonyesha kama ile ni kazi ya kufurahisha, Yesu alisema hivi: “Mukuje kwangu, ninyi wote wenye kuteseka na wenye kulemewa na mizigo, na mimi nitawapumuzisha. Mubebe nira yangu na mujifunze kupitia mimi, kwa maana mimi ni mwenye tabia ya upole na munyenyekevu katika moyo, na mutapata pumuziko kwa ajili yenu.” (Mt. 11:28, 29) Wote wenye kuitika ile mualiko wako najionea vile ahadi ya Yesu iko natimia kabisa!

2 Juu yeye njo Mutumishi Mukubwa zaidi wa Mungu, alialika watu wengine wakuwe wafuasi wake. (Mt. 9:9; Yoh. 1:43) Aliwapatia mazoezi juu ya namna ya kuhubiri na aliwatuma ili wafanye kazi sawa ile yenye alikuwa anafanya. (Mt. 10:1–11:1; 20:28; Lu. 4:43) Kisha, alituma wengine 70 ili wahubiri habari njema juu ya Ufalme wa Mungu. (Lu. 10:1, 8-11) Wakati Yesu aliwatuma, aliwaambia hivi: “Kila mutu mwenye anawasikiliza ninyi ananisikiliza mimi pia. Na kila mutu mwenye anawazarau ninyi ananizarau mimi pia. Zaidi ya hayo, kila mutu mwenye ananizarau mimi, anazarau pia Ule mwenye alinituma.” (Lu. 10:16) Kwa kusema vile, Yesu alionyesha kama daraka yenye alipatia wanafunzi wake ilikuwa nzito. Walikuwa wajumbe wake na wa Mungu Mwenye Kuwa Juu Zaidi! Ni vile pia leo kwa wote wenye kuitika hii mualiko ya Yesu: “Ukuje ukuwe mufuasi wangu.” (Lu. 18:22; 2 Ko. 2:17) Wote wenye kuitika ile mualiko wanatumwa na Mungu ili kuhubiri habari njema ya Ufalme na kufanya wanafunzi.​—Mt. 24:14; 28:19, 20.

3 Vile tuliitika mualiko wa Yesu wa kumufuata, tuko wenye kubarikiwa sana juu ‘tunafikia kumujua’ Yehova Mungu na Yesu Kristo. (Yoh. 17:3) Tulishajifunza mambo yenye Yehova anapenda. Yehova alishatusaidia kufanya upya akili yetu, kuvala utu mupya ao kubadilika kabisa, na kuishi kulingana na kanuni zake za haki. (Ro. 12:1, 2; Efe. 4:22-24; Kol. 3:9, 10) Tuko wenye shukrani sana kwa Yehova juu ya ile mambo yote; na ile njo ilitusukuma tujitoe kwake katika sala. Kisha tulionyesha ile kwa kubatizwa mu maji. Kuanzia pale tukakuwa watumishi wake wenye kukubaliwa.

4 Kila siku tukumbuke kama, tunapaswa kuwa na moyo safi na mikono yenye haina kosa wakati tuko namutumikia Mungu. (Zb. 24:3, 4; Isa. 52:11; 2 Ko. 6:14–7:1) Tuko na zamiri safi juu tunamuamini Yesu. (Ebr. 10:19-23, 35, 36; Ufu. 7:9, 10, 14) Mutume Paulo alishauri Wakristo wafanye mambo yote kwa utukufu wa Mungu ili wasikwaze wengine. Pia mutume Petro alionyesha kama mwenendo muzuri unaweza kuchochea watu wenye hawako Mashahidi wapende ile kweli. (1 Ko. 10:31, 33; 1 Pe. 3:1) Tunaweza kufanya nini juu ya kusaidia mutu fulani afikie kuwa muhubiri wa habari njema?

WAHUBIRI WAPYA

5 Wakati tu unaanza kujifunza Biblia na mutu mwenye kupendezwa, umutie moyo aanze kuelezea wengine mambo yenye iko najifunza. Wakati anapata nafasi, anaweza kuelezea watu wa jamaa yake, marafiki, wafanyakazi wenzake na watu wengine. Ile ni hatua ya maana ili kuwafundisha wapya wakuwe wafuasi wa Yesu Kristo, ni kusema, wahubiri wa habari njema. (Mt. 9:9; Lu. 6:40) Kusema kweli, kadiri mwanafunzi anakomala kiroho na anazoea kuhubiria watu kila wakati nafasi ikijitokeza, ile itamusukuma aanze kupenda kuhubiri pamoya na kutaniko.

MAMBO YENYE KUOMBWA ILI KUWA MUHUBIRI

6 Mbele ya kuambia mutu fulani aanze kuhubiri nyumba kwa nyumba kwa mara ya kwanza, unapaswa kuhakikisha kama alishatimiza mambo fulani yenye inaombwa. Mutu akipenda kuenda na siye mu mahubiri, maana yake anajitambulisha mbele ya watu wote kama yeye ni Shahidi wa Yehova. Kwa hiyo, anapaswa kuwa mutu mwenye alishaanza kuishi kulingana na kanuni za Yehova za haki, na tayari anaweza kuwa muhubiri mwenye hayabatizwa.

7 Kwa kawaida, wakati uko najifunza na mutu na kuzungumuzia kanuni za Biblia pamoya naye, unaweza kujua hali yake. Pengine utatambua kama alishaanza kuishi kulingana na mambo yenye iko najifunza. Lakini kuko mambo fulani juu ya maisha yake yenye wazee watapenda kwanza kujua. Kwa hiyo, watazungumuza na nyie wote wawili, ni kusema weye na mwanafunzi wako.

8 Muratibu wa baraza ya wazee atafanya mipango ili wazee wawili (mumoya kati yao anapaswa kuwa mu halmashauri ya utumishi ya kutaniko) wazungumuze na nyie. Mu makutaniko mwenye hamuna wazee wengi, muzee moya na mutumishi wa huduma mwenye kustahili wanaweza kufanya ile kazi. Wale ndugu wanapaswa kujikaza kufanya ile mazungumuzo bila kuchelewa. Kama muko ku mukutano, na kule njo wazee wanapata habari kama mwanafunzi wako wa Biblia anapenda kuwa muhubiri, wanaweza kufanya mipango ili wazungumuze na nyie kisha tu ile mukutano. Ni muzuri kufanya ile mazungumuzo mu hali ya urafiki. Mbele mwanafunzi akubaliwe kuwa muhubiri mwenye hayabatizwa, inaomba kuhakikisha ikiwa:

  1. (1) Anaamini kwamba Biblia ni Neno ya Mungu yenye iliongozwa na roho yake.​—2 Ti. 3:16.

  2. (2) Anajua na anaamini mafundisho ya musingi ya Biblia, juu wakati ataulizwa maulizo fulani, asijibie kulingana na mafundisho ya uongo ao kulingana na mawazo yake, lakini ajibie kulingana na Biblia.​—Mt. 7:21-23; 2 Ti. 2:15.

  3. (3) Iko natii amri yenye kuwa mu Biblia ya kukusanyika na watu wa Yehova ku mikutano ya kutaniko kama hali yake inaruhusu.​—Zb. 122:1; Ebr. 10:24, 25.

  4. (4) Anajua mambo yenye Biblia inafundisha juu ya uasherati, uzinifu, kuoa wanamuke wengi, mwanaume kulala na mwanaume ao mwanamuke kulala na mwanamuke, na iko naishi kulingana na ile mafundisho. Kama ni mwanaume mwenye kuishi pamoya na mwanamuke, ao ni mwanamuke mwenye kuishi pamoya na mwanaume, na ule mutu haiko wa jamaa yake, lazima wakuwe wenye kuoana kulingana na sheria.​—Mt. 19:9; 1 Ko. 6:9, 10; 1 Ti. 3:2, 12; Ebr. 13:4.

  5. (5) Iko natii mashauri yenye kuwa mu Biblia, yenye inakataza ulevi na kutumia dawa za kulewesha, kama tu haiko kwa sababu ya matunzo.​—2 Ko. 7:1; Efe. 5:18; 1 Pe. 4:3, 4.

  6. (6) Iko naona ulazima wa kuepuka marafiki wabaya.​—1 Ko. 15:33.

  7. (7) Alishaachana kabisa na dini ya uongo, kama njo mule alikuwaka zamani. Alishaacha kukusanyika nao na kuwategemeza mu mambo yenye wako nafanya.​—2 Ko. 6:14-18; Ufu. 18:4.

  8. (8) Alishaacha kabisa kujiingiza mu mambo ya politike ya mu hii dunia.​—Yoh. 6:15; 15:19; Yak. 1:27.

  9. (9) Anaamini na iko naishi kupatana na maneno yenye kuwa mu andiko ya Isaya 2:4, yenye inazungumuzia ugomvi kati ya mataifa.

  10. (10) Anapenda kabisa kuwa Shahidi wa Yehova.​—Zb. 110:3.

9 Kama wazee hawako hakika na mawazo ya mwanafunzi juu ya jambo fulani kati ya ile mambo, watamuuliza maulizo fulani, pengine kwa kutumikisha maandiko yenye kuonyeshwa. Ni lazima mwanafunzi aelewe kama wale wenye wanahubiri na Mashahidi wa Yehova wanapaswa kutumikisha mu maisha yao zile kanuni zenye kuwa mu Biblia. Majibu ya mwanafunzi itasaidia wazee watambue kama anajua mambo yenye inaomba afanye, ao kama iko naitimiza kwa kiasi fulani ili aanze kuhubiri na kutaniko.

10 Wazee wanapaswa kumujulisha palepale kama anastahili kuwa muhubiri ao hapana. Mara mingi, wanaweza kufanya vile kisha tu ile mazungumuzo. Kama anastahili, wazee watamujulisha na watamukaribisha kwa furaha mu kutaniko. (Ro. 15:7) Wanapaswa kumutia moyo aanze kuhubiri na kutaniko bila kukawia na kutoa ripoti yake ya mahubiri ku mwisho ya mwezi. Wazee watamufasiria kama, wakati mwanafunzi wa Biblia anakuwa muhubiri na anatoa ripoti yake ya kwanza ya mahubiri, Fishe ya Muhubiri ya Kutaniko inafanywa, na kunatiwa jina yake, kisha inawekwa mu dosye ya kutaniko. Kama wahubiri wanaombwa waambie wazee habari zao za kipekee, ni kwa kusudi ya kusaidia tengenezo ya Mashahidi wa Yehova iweze kusimamia muzuri kazi za kidini mu dunia yote; tena ni juu ya kusaidia wahubiri wafanye muzuri kazi yao ya kidini na watiwe moyo kiroho. Zaidi ya ile, wazee wanaweza kukumbusha wahubiri wapya kama, habari yoyote ya kipekee inashugulikiwa kulingana na Kanuni za mu Dunia Yote za Kulinda Habari za Mashahidi wa Yehova. Zile kanuni zinapatikana ku jw.org.

11 Kujikaza kumujua muzuri muhubiri mupya na kuonyesha kwamba tunapendezwa na mambo yenye alishafanya, kunaweza kuwa na matokeo ya muzuri juu yake. Ile inaweza kumusukuma akuwe natoa ripoti ya utumishi kwa ukawaida kila mwezi na ajikaze sana kumutumikia Yehova.​—Flp. 2:4; Ebr. 13:2.

12 Wakati wazee wanaamua kama mwanafunzi wa Biblia anastahili kuanza kuhubiri na kutaniko, watamupatia kitabu Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova. Wakati mwanafunzi atatoa ripoti yake ya kwanza, kutaniko itatangaziwa kwa kifupi kama ule mwanafunzi anakuwa muhubiri mwenye hayabatizwa.

NAMNA YA KUSAIDIA VIJANA

13 Hata watoto wadogo wanaweza kuwa wahubiri wa habari njema. Yesu aliwakaribisha watoto wadogo na aliwabariki. (Mt. 19:13-15; 21:15, 16) Hata kama ni wazazi kwanza njo wako na daraka ya kusaidia watoto wao, ndugu na dada wengine mu kutaniko wanaweza pia kufurahia kusaidia vijana wenye kuonyesha kabisa kama wanapenda kuwa wahubiri wa habari njema ya Ufalme. Kama uko muzazi, mufano wako muzuri mu kazi ya kuhubiri utatia watoto wako moyo ili wamutumikie Mungu kwa bidii. Kama mutoto iko na mwenendo ya muzuri, na anapenda kabisa kutangaza imani yake mbele ya wengine, inaomba kufanya nini juu ya kumusaidia zaidi?

14 Ni muzuri muzazi wake azungumuze na muzee moya kati ya wazee wa Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko ili wachunguze ikiwa ule mutoto anastahili kuwa muhubiri. Muratibu wa baraza ya wazee atafanya mipango ili wazee wawili (mumoya kati yao anapaswa kuwa mu halmashauri ya utumishi ya kutaniko) wazungumuze na ule mutoto pamoya na wazazi wake Mashahidi ao mutu mwenye kumuchunga, kama naye ni Shahidi. Kama mutoto alishajua mafundisho ya musingi ya Biblia na anaonyesha kama anapenda kuwa muhubiri, ile inaonyesha kama alishafanya maendeleo. Kisha kuchunguza ile mambo na mambo ingine yenye inaombwa kwa wakubwa, wale wazee wawili wataamua ikiwa mutoto anaweza kukubaliwa kuwa muhubiri mwenye hayabatizwa ao hapana. (Lu. 6:45; Ro. 10:10) Wakati wazee wanazungumuza na mutoto, haitakuwa lazima kuzungumuzia mambo yenye haimuhusu kabisa, ni kusema, mambo yenye kwa kawaida inaangalia tu wakubwa.

15 Wakati ya mazungumuzo, wazee wanapaswa kumupongeza ule mutoto juu ya maendeleo yake na kumutia moyo ajiwekee muradi ya kubatizwa. Ni muzuri pia kupongeza wazazi juu wao njo walitumika sana ili kuingiza kweli mu moyo ya mutoto yao. Ili wazazi waweze kusaidia muzuri mutoto yao, wazee wanapaswa kuwatia moyo wachunguze habari yenye kuwa ku ukurasa wa 179-181, yenye kichwa “Barua kwa Wazazi Wakristo.”

KUJITOA KWA MUNGU KATIKA SALA NA KUBATIZWA

16 Vile ulishamujua Yehova na kumupenda, na vile ulishatimiza mambo fulani yenye anaomba, na tayari ulishaanza kuhubiri habari njema, inaomba sasa ufanye urafiki wako na Yehova ukuwe nguvu. Utafanya vile namna gani? Inaomba ujitoe kwa Yehova katika sala na uonyeshe kama ulishajitoa kwa kubatizwa mu maji.​—Mt. 28:19, 20.

17 Kujitoa kwa Yehova, maana yake kuwekwa pembeni kwa ajili ya kusudi takatifu. Ni kusema, kumukaribia Mungu katika sala, na kumutolea ahadi ya kama utamutumikia maisha yako yote, na kumuambia kama utaishi kulingana na kanuni zake. Maana yake unajitoa kwake tu, hapana kwa wakati kidogo, lakini milele. (Kum. 5:9) Ile ni jambo ya kufanya weye peke. Hakuna mutu mwenye anaweza kujitoa pa fasi yako.

18 Lakini, haiko tu kumuambia Yehova kwa siri kama unapenda kuwa mali yake. Inaomba pia kuonyesha mbele ya wengine kama ulishajitoa kwake. Unaonyesha wengine vile, wakati unabatizwa mu maji sawa vile Yesu alifanya. (1 Pe. 2:21; 3:21) Kama ulishaamua kumutumikia Yehova na unapenda kubatizwa, unapaswa kufanya nini? Umuambie muratibu wa baraza ya wazee. Atafanya mipango ili wazee fulani wazungumuze na weye, ili waone kama unatimiza mambo yenye Mungu anaomba wale wenye wanapenda kubatizwa wafanye. Ili ujue mambo mingi zaidi, tafazali soma habari yenye kusema: “Barua kwa Muhubiri Mwenye Hayabatizwa,” ku ukurasa wa 182-184 wa hii kitabu, na “Maulizo kwa Ajili ya Wale Wenye Kupenda Kubatizwa,” ku ukurasa wa 185-207.

RIPOTI ZENYE KUONYESHA MAENDELEO YA KAZI YA KUHUBIRI

19 Kwa miaka mingi, ripoti zenye kuonyesha maendeleo ya ibada safi mu dunia yote zinatiaka moyo watu wa Yehova. Tangu wakati Yesu Kristo aliambia wanafunzi wake kama habari njema inapaswa kuhubiriwa mu dunia yote, Wakristo wa kweli wanapendaka sana kujua namna gani ile kazi itafanywa.​—Mt. 28:19, 20; Mk. 13:10; Mdo. 1:8.

20 Wafuasi wa kwanza wa Yesu walifurahia kusikia ripoti za matokeo ya muzuri juu ya kazi ya kuhubiri. (Mk. 6:30) Kitabu ya Matendo inatuambia kama, kulikuwa watu 120 hivi wakati roho takatifu ilimwangwa juu ya wanafunzi kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33 K.K.Y. Kisha tu wakati mufupi, hesabu ya wanafunzi iliongezeka na kuwa watu 3 000 hivi, na kisha ilifikia kuwa watu 5 000 hivi. Ripoti yenye ilitolewa, ilionyesha kama ‘Yehova aliendelea kuwaongezea kila siku watu wenye walikuwa wanaokolewa’ na kwamba ‘makuhani wengi sana wakaanza kutii imani.’ (Mdo. 1:15; 2:5-11, 41, 47; 4:4; 6:7) Bila shaka, zile habari juu ya ongezeko ziliwatia moyo wanafunzi! Tena ziliwasukuma waendelee kufanya kazi yenye Mungu aliwapatia, hata kama viongozi wa dini ya Wayahudi walianzisha mateso makali juu yao.

21 Mu barua yenye aliandikia Wakristo Wakolosai, mu mwaka wa 60 na 61 K.K.Y., mutume Paulo alitoa ripoti ya kwamba habari njema ilikuwa “inazaa matunda na kuongezeka katika ulimwengu wote” na kwamba “ilihubiriwa katika uumbaji wote chini ya mbingu.” (Kol. 1:5, 6, 23) Wakristo wa kwanza walikuwa wanatii Neno, na roho takatifu iliwapatia nguvu ya kufanya kazi kubwa ya kuhubiri mbele ya mwisho yenye iliwafikia Wayahudi mu mwaka wa 70 K.K.Y. Kusema kweli, wale Wakristo waaminifu walitiwa moyo sana kusikia ripoti ya kazi yenye ilikuwa inafanyika ile wakati!

Unafurahia kabisa kuona vile kazi ya kuhubiri iko nafanywa mbele mwisho ifike?

22 Vilevile, leo tengenezo ya Yehova inajikazaka kuandika ripoti ya kazi yenye kufanywa; ni kusema, kazi yenye kutimiza andiko ya Matayo 24:14, yenye kusema hivi: “Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho utakuja.” Juu tuko watumishi wenye walishajitoa kwa Mungu, tuko na kazi ya haraka yenye tunapaswa kufanya. Ni lazima tufanye yetu yote juu ile kazi ya kuhubiri ifanywe muzuri kabisa mbele mwisho ifike. Yehova atahakikisha kama ile kazi imeisha. Na kama tunajikaza kuifanya, tutafurahisha moyo wake.​—Eze. 3:18-21.

RIPOTI YAKO YA MAHUBIRI

23 Ni nini tunapaswa kuripoti? Karatasi ya Ripoti ya Mahubiri yenye kuchapishwa na tengenezo inaonyesha mambo yenye tunapaswa kuripoti. Lakini, maelezo yenye kufuata inaweza kutusaidia sana.

24 Mu sehemu “Vichapo Vyenye Uliachia Watu (na vya Kielektronike),” utaandika hesabu ya vichapo vyote, ikuwe vya kieletronike ao vya kuchapishwa vyenye uliachia watu wenye hawako Mashahidi wa Yehova wenye kubatizwa. Mu sehemu “Video Zenye Ulionyesha,” andika ni mara ngapi ulionyesha video mbalimbali.

25 Mu sehemu “Marudio,” andika ni mara ngapi ulirudilia watu fulani wenye kupendezwa wenye bado hawayajitoa kwa Yehova na kubatizwa. Unaweza kuhesabia rudio kama unamutembelea mutu na kuzungumuza naye tena, ao wakati unamuandikia barua, kumuita ku telefone, kumuandikia habari fulani ya Biblia kupitia telefone ao kupitia Enternete, ao kwa kumutumia vichapo fulani. Kila mara ukiongoza funzo ya Biblia, utahesabia pia rudio. Kila juma, kama muzazi anaongoza ibada ya familia, na mu ile ibada muko mutoto mwenye hayabatizwa, anaweza kuhesabia rudio moya.

26 Kwa kawaida, funzo ya Biblia inaongozwaka kila juma. Lakini hata kama ulijifunza na mutu fulani mara ngapi, ku mwisho ya mwezi utaripoti tu funzo moya. Muhubiri anapaswa kuandika hesabu ya mafunzo mbalimbali ya Biblia yenye aliongoza mu mwezi. Mafunzo ya Biblia yenye muhubiri anaweza kuripoti, inatia ndani watu wenye hawayajitoa kwa Yehova na kubatizwa. Unaweza pia kuripoti funzo, kama muzee fulani mwenye kuwa mu halmashauri ya utumishi ya kutaniko anakuomba ujifunze Biblia na ndugu ao dada fulani mwenye hatende tena, ao kama uko najifunza na ndugu ao dada mwenye kubatizwa, lakini hayamaliza kitabu Furahia Maisha Milele!.

27 Inaomba kuripoti “Saa” za kweli za mahubiri. Ni kusema, saa zenye unapitisha mu mahubiri ya nyumba kwa nyumba, kuwarudilia watu wenye kupendezwa, kuongoza mafunzo ya Biblia, ao kuhubiri hata kama haukupanga kufanya vile ao wakati unazungumuza na watu wenye hawako Mashahidi wa Yehova wenye kubatizwa. Kama wahubiri wawili wanatumika pamoya, wote wanaweza kuripoti saa za mahubiri, lakini ni mumoya tu njo atahesabia marudio na mafunzo yake ya Biblia yenye waliongoza. Wazazi wawili wenye kufundisha pamoya watoto wao wakati wa Ibada ya Familia ya mangaribi wanaweza kuhesabia saa moya kila juma. Ndugu wanaweza kuhesabia wakati yenye walitumia ili kufanya hotuba ya watu wote. Muhubiri mwenye kutafsiri hotuba ya watu wote anaweza pia kuhesabia ile wakati yenye atafanya. Hatutahesabia wakati yenye tunaweza kupitisha mu mambo ingine ya lazima, sawa vile kujitayarisha kwa ajili ya mahubiri, kuhuzuria mukutano kwa ajili ya mahubiri, kufanya matembezi fulani na mambo ingine.

28 Kila muhubiri anapaswa kufuata zamiri yake yenye kuzoezwa na Biblia wakati iko nasali ili kuamua ni saa ngapi za mahubiri zenye anaweza kuhesabia. Wahubiri fulani wanahubiri mu maeneo yenye kuwa na watu wengi sana, lakini wengine wanahubiri mu maeneo yenye kuwa na watu kidogo, na inaomba kufanya safari ya murefu juu ya kuwapata. Maeneo, na mawazo ya wahubiri juu ya kazi yao ya kuhubiri iko tofauti. Baraza Yenye Kuongoza hailazimishe kila Shahidi mu makutaniko yenye kuwa mu dunia yote afuate zamiri yao juu ya namna ya kuhesabia saa za mahubiri, wala hakuna mutu mwenye alishawekwa ili kuamulia wengine juu ya ile jambo.​—Mt. 6:1; 7:1; 1 Ti. 1:5.

29 Wakati unatoa ripoti ya saa za mahubiri, hautaweka ndani dakika. Lakini ni tofauti na muhubiri mwenye iko na mipaka fulani juu ya uzee, mwenye haitawezekana atoke mu nyumba, mwenye iko mu nyumba ya kuchungia wazee, ao mwenye hana uwezo kwa sababu ya hali ingine ya nguvu. Muhubiri mwenye kuwa mu hali za vile anaweza kuandika hata vipande-vipande vya dakika 15. Hata kama alihubiri tu dakika 15 mu mwezi, anapaswa kuziripoti, na atahesabiwa kati ya wahubiri wa Ufalme wenye kuhubiri kwa ukawaida. Ile mupango inatumiwa pia kwa muhubiri fulani mwenye anakuwa muzaifu kwa wakati fulani, pengine mwenye hawezi kutembea mu mwezi muzima ao zaidi juu anagonjwa sana ao aliumia sana. Ni mupango yenye inahusu tu wahubiri wenye kuwa na mipaka kabisa. Ni halmashauri ya utumishi ya kutaniko njo itaamua ni wahubiri gani wenye wanahusika mu hii mupango.

FISHE YA MUHUBIRI YA KUTANIKO

30 Ripoti yako ya mahubiri ya kila mwezi inaandikwa ku Fishe ya Muhubiri ya Kutaniko. Ile fishe haiko yako, ni ya kutaniko. Kwa hiyo, wakati unapanga kuhamia mu kutaniko ingine, usikose kujulisha wazee wa kutaniko yako. Mwandishi wa kutaniko yako atatuma fishe yako ya mahubiri mu ile kutaniko unahamia. Ile itasaidia wazee wa mu kutaniko yako ya sasa wakukaribishe na kuwa tayari kukupatia musaada ya kiroho yenye uko nayo lazima. Kama unaenda fasi ingine, na unaanza kukusanyika kule, lakini hautafanya zaidi ya miezi tatu, tafazali, uendelee tu kutuma ripoti yako ya mahubiri ku kutaniko kwenye ulitoka, ni kusema ku kutaniko yako.

JUU YA NINI TUNATOAKA RIPOTI YA MAHUBIRI?

31 Ilishakakufikia siku fulani unasahau kutoa ripoti yako ya mahubiri? Bila shaka, siye wote tunakuwaka na lazima ya kukumbushwa mara kwa mara. Lakini, kama tunaendelea kuwa na mawazo ya muzuri juu ya kutoa ripoti ya mahubiri, na kama tunaelewa juu ya nini kufanya vile ni jambo ya lazima, itakuwa mwepesi kwetu kukumbuka kuitoa.

32 Wahubiri fulani wanajiuliza: “Vile Yehova anajua muzuri mambo yenye niko nafanya mu kazi ya kuhubiri, juu ya nini tena nitoe ripoti mu kutaniko?” Ni kweli Yehova anajua muzuri ile tuko nafanya, na anajua muzuri ikiwa tuko namutumikia kwa nafsi yetu yote ao kama tuko nafanya kidogo kuliko vile tunaweza kufanya kabisa. Lakini, kumbuka kama Yehova aliandikisha hesabu ya siku zenye Noa alifanya mu safina na miaka yenye Waisraeli walitembea mu jangwa. Mungu aliandikisha hesabu ya watu wenye walikuwa waaminifu kwake na wale wenye walikosa kumutii. Aliandikisha habari kuhusu namna Waisraeli walikamata inchi ya Kanaani hatua kwa hatua, na mambo yenye waamuzi Waisraeli wenye walikuwa waaminifu walifanya. Ndiyo, Yehova aliandikisha mambo mingi juu ya kazi mbalimbali zenye watumishi wake walifanya. Alitumia roho yake takatifu juu mambo yenye ilifanyika zamani iandikwe. Alifanya vile juu ya kutuonyesha kama anaona kuandika na kuchunga ripoti kuwa jambo ya lazima.

33 Mambo yenye ilitokea yenye kuandikwa mu Biblia, inaonyesha kama ripoti na habari mbalimbali zenye watu wa Yehova waliandika ni za kweli. Mu hali mingi, ingekuwa nguvu kuelewa muzuri habari fulani kama hesabu kamili haingeandikwa. Angalia mifano yenye kupatikana mu hii maandiko: Mwanzo 46:27; Kutoka 12:37; Waamuzi 7:7; 2 Wafalme 19:35; 2 Mambo ya Nyakati 14:9-13; Yohana 6:10; 21:11; Matendo 2:41; 19:19.

34 Hata kama ku ripoti yetu hatuonyeshake mambo yote yenye tuko nafanya mu ibada yetu kwa Yehova, ile ripoti ni ya lazima mu tengenezo ya Yehova. Zamani, kisha mitume kufanya kazi ya kuhubiri, walirudia na kumupatia Yesu ripoti ya “mambo yote yenye walikuwa wamefanya na kufundisha.” (Mk. 6:30) Wakati fulani, ripoti zinaweza kutusaidia kujua ni mambo gani tunapaswa kukazia sana uangalifu kuhusu kazi yetu ya kuhubiri. Zile hesabu zinaweza kuonyesha kwamba tulifanya maendeleo mu mambo fulani mu kazi yetu ya kuhubiri, lakini mu mambo ingine munaweza kuwa shida, ni kusema, pengine hesabu ya wahubiri haiongezeke ao iko naongezeka polepole sana. Pengine wahubiri wako na lazima ya kutiwa moyo ao kuko magumu fulani yenye inaomba kushugulikiwa. Waangalizi wako na kazi ya kuchunguza ripoti za mahubiri na kujikaza kutengeneza mambo fulani, yenye pengine iko nazuia maendeleo ya wahubiri fulani ao ya kutaniko yote.

35 Tena, ripoti zinasaidia tengenezo ya Yehova kujua ni wapi kuko lazima kubwa ya wahubiri. Ni maeneo gani mwenye muko maendeleo zaidi? Ni mu maeneo gani mwenye maendeleo iko chini? Ni vichapo gani vitasaidia watu wajifunze kweli? Ripoti zinasaidia tengenezo kujua na kufanya mipango juu ya vichapo vyenye itaomba kutumikisha mu mahubiri, mu sehemu mbalimbali za dunia.

36 Mara mingi, ripoti zinatiaka watu wengi moyo. Tunafurahi kabisa wakati tunasikia mambo yenye ndugu na dada zetu wako natimiza mu kazi ya kuhubiri habari njema mu dunia yote, haiko vile? Ripoti juu ya ongezeko zinatusaidiaka kuelewa muzuri namna tengenezo ya Yehova iko naendelea kupanuka. Mambo yenye wahubiri walikutana nayo mu mahubiri inatufurahishaka sana na kufanya tukuwe na bidii zaidi; tena, inatusukumaka tufanye mingi zaidi mu kazi ya kuhubiri habari njema. (Mdo. 15:3) Kuunga mukono mupango ya kutoa ripoti ya kazi ya kuhubiri ni jambo ya lazima sana, na ile inaonyesha kama tuko nahangaikia ndugu na dada zetu mu dunia yote. Kufanya ile sehemu yenye inaweza kuonekana sawa vile ya kidogo, ni njia ya kuonyesha kama tuko natii mipango yenye tengenezo ya Yehova iko nakamata.​—Lu. 16:10; Ebr. 13:17.

KUJIWEKEA MIRADI

37 Hatupaswe kulinganisha ripoti yetu ya mahubiri na ripoti ya muhubiri mwingine. (Gal. 5:26; 6:4) Hali za watu ziko tofauti. Kuliko kufanya vile, tunaweza kupima maendeleo yetu mu kazi yetu ya kuhubiri kwa kujiwekea miradi yenye tunaweza kufikia. Kufikia ile miradi njo itafanya tukuwe na furaha na tupate faida kabisa.

38 Ni wazi kwamba Yehova iko nakusanya haraka watu wenye atalinda wakati wa “taabu kubwa.” Leo tuko najionea kutimizwa kwa hii unabii ya Isaya: “Mudogo atakuwa elfu na mutu wa hali ya chini atakuwa taifa lenye nguvu. Mimi mwenyewe, Yehova, nitaharakisha jambo hilo kwa wakati wake.” (Ufu. 7:9, 14; Isa. 60:22) Ni pendeleo kubwa sana kuwa wahubiri wa habari njema mu hii kipindi ya siku za mwisho!​—Mt. 24:14.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine