Tutoe Utumishi Mtakatifu Mchana Na Usiku
1 Tunalo pendeleo lisilo na kifani: lile la kuwa Mashahidi wa Yehova. Sisi tumo katika tengenezo la ulimwenguni pote la waevanjelisti ambao Yehova anatumia ili kutimiza kazi iliyo kubwa ya utangazaji wa Ufalme wa nyakati zote. (Mk. 13:10) Kwa kuwa tunaishi kipindi kigumu, je! tunajitoa kabisa katika utendaji huo kwa kadiri ya uwezo wetu?
2 Hatujui ni watu wangapi wataguswa moyo na mahubiri yetu. Yehova unatutolea uhakikisho wa kwamba kutakuwako “mkutano mkubwa” ambao washiriki wao wanajitofautisha kwa ‘utumishi mtakatifu wanaotoa mchana na usiku.’ (Ufu. 7:9, 15) Zaidi ya milioni tano ya Mashahidi wa Yehova wanaoshughulika leo katika utumishi wa Mungu hawako tu wasikiaji wanaoonyesha kupendezwa fulani, wala watu wanaoridhika tu kwa kuhudhuria kwenye mikutano. Ni watu wanaotimiza kazi fulani, wanaotangaza habari njema ulimwenguni pote.
3 Kila siku tunazo nafasi za kumsifu Yehova, iwe kwa njia ya mahubiri yanayotayarishwa au kwa namna ya vivihivi. Tufikirie ukubwa wa ushuhuda ambao ungeweza kutolewa ikiwa kila mmoja wetu angechukua uamuzi wa kutangaza ukweli iwe tu kwa mtu mmoja kila siku. Shukrani yetu kwa Yehova ingepaswa kutusukuma kusema juu yake kwa namna ya shauku.—Zab. 92:1, 2.
4 Tuwasaidie Wengine Kutoa Utumishi Mtakatifu: Yehova anaendelea kutubariki kwa kututolea ongezeko. (Hag. 2:7) Wastani ya mafunzo ya Biblia yaliyoongozwa Burundi, Congo na Zaïre, mnamo mwaka wa utumishi wa nyuma, ilikuwa ya 3,278, 11,138 na 180,017. Tunapojifunza na watu, kusudi letu ni kuwasaidia kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo. (Mt. 28:19, 20) Wengi wao wamekwisha kufanya maendeleo makubwa na wanahudhuria kikawaida kwenye mikutano. Waliisha kuanza kusema kwa marafiki zao juu ya “mambo yenye fahari ya Mungu” ambayo walijifunza. (Mdo. 2:11, NW) Je! tunaweza kwa sasa kuwaalika kushiriki katika huduma ya peupe?
5 Mnamo mwezi wa Mei, tutafanya bidii ya pekee ili kualika wanafunzi wanaotimiza matakwa yanayoombwa kujiunga nasi katika mahubiri. Je! mtu unayejifunza naye ameonyesha tamaa hiyo? Ikiwa ni hivyo, je! anatimiza matakwa yanayoombwa na Maandiko? (Ona kitabu Huduma Yetu, kurasa 97-99.) Wakati mwanafunzi anatamani kushiriki katika mahubiri, eleza nia yake kwa mwangalizi-msimamizi, ambaye atachukua mipango ili kwamba wazee wawili wachunguze swala hilo. Ikiwa anatimiza matakwa ili kuwa mhubiri asiyebatizwa, alikeni mwanafunzi awasindikize katika mahubiri. Mwangalizi wa utumishi na viongozi kwenye funzo la kitabu watakuwa hasa waangalifu kuwasaidia wale ambao wangeweza kutimiza matakwa yanayoombwa ili kuanza kuhubiri katika Mei.
6 Ingekuwa vizuri kwamba wazazi wachunguze ikiwa watoto wao wanaweza kuwa wahubiri wasiobatizwa. (Zab. 148:12, 13) Ikiwa mtoto wenu anatamani kusema katika utumishi wa Ufalme na ikiwa ana mwenendo mzuri, mnaweza kuzungumza na mzee fulani aliye mshiriki wa halmashauri ya utumishi. Kisha kukusanyika nanyi na mtoto, wazee wawili watahakikisha ikiwa anaweza kuhesabiwa kati ya wahubiri. Ni jambo lenye kufurahisha hasa kwamba watoto wamsifu Mungu pembeni nasi!
7 Yehova peke yake ndiye anayestahili kwamba tumtolee utumishi mtakatifu. (Lk. 4:8) Basi sote na tuweze kufaidika na pendeleo la ajabu tulilo nalo la kumsifu “sana”!—Zab. 109:30; 113:3.