Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/03 uku. 3-6
  • Iweni Wenye Bidii kwa Lililo Jema!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Iweni Wenye Bidii kwa Lililo Jema!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Hubiri Neno la Mungu Kikamili’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • ‘Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Endeleeni Kutangaza Kazi za Ajabu za Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Je, tunaweza kufanya Aprili 2000 kuwa mwezi wetu bora kuliko yote?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 3/03 uku. 3-6

Iweni Wenye Bidii kwa Lililo Jema!

1 Tunapoanza majira ya Ukumbusho ya mwaka wa 2003, tuna sababu nyingi za kuwa “wenye bidii kwa lililo jema.” (1 Pet. 3:13) Ya kwanza kabisa kati ya sababu hizo ni ile dhabihu ya ukombozi ya Yesu Kristo. (Mt. 20:28; Yn. 3:16) Kuhusu hiyo, mtume Petro aliandika: “Haikuwa kwa vitu vyenye kuharibika, kwa fedha au dhahabu, kwamba mlikombolewa kutoka kwenye namna ya mwenendo usio na matunda. . . . Bali ilikuwa kwa damu yenye bei, kama ile ya mwana-kondoo asiye na waa na asiye na doa, naam, ya Kristo.” (1 Pet. 1:18, 19) Shukrani kwa wonyesho huo wa ajabu wa upendo zinatulazimisha kujishughulisha katika kufanya lililo jema, tukijua kwamba Yesu ‘alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu ili apate kutukomboa sisi kutoka kwenye kila namna ya uasi-sheria na kujisafishia mwenyewe watu walio wake mwenyewe pekee, wenye bidii kwa kazi zilizo bora.’—Tito 2:14; 2 Kor. 5:14, 15.

2 Tunapofanya yale yanayopendeza machoni pa Mungu, tunafurahia uhusiano mzuri pamoja naye na kuja chini ya ulinzi wake wenye upendo. Petro aliendelea kusema: “Yeye ambaye angependa uhai na kuona siku zilizo njema, . . . acheni ageuke mbali kutoka lililo baya na kufanya lililo jema; acheni atafute sana amani na kuifuatia. Kwa maana macho ya Yehova yako juu ya waadilifu, na masikio yake yaelekea dua zao.” (1 Pet. 3:10-12) Katika nyakati hizi zenye hatari, ni baraka kama nini kujua kwamba Yehova ni mwenye kutulinda na yuko tayari kutenda kwa ajili yetu, ‘akitulinda kama mboni ya jicho lake.’—Kumb. 32:10; 2 Sik. 16:9.

3 Ijapokuwa walipambana na majaribu, Wakristo wa mapema ambao Petro aliandikia walichochewa na bidii ambayo haingeweza kuzimwa, na walitangaza habari njema kwa kiasi kikubwa zaidi iwezekanavyo. (1 Pet. 1:6; 4:12) Jambo hilohilo ni kweli kuhusu watu wa Mungu leo. Ijapokuwa tunaishi “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo,” shukrani kwa wema wa Yehova zinatuchochea kufanya mapenzi ya Mungu kwa bidii. (2 Tim. 3:1; Zab. 145:7) Acheni tuchunguze kazi fulani zilizo jema tutakazojishughulisha nazo mnamo majira haya ya Ukumbusho.

4 Tualike Wengine Kwenye Ukumbusho: Njia moja ambayo kwa hiyo tunaweza kuonyesha shukrani zetu kwa zawadi ya ajabu ya ukombozi ni kuwapo kwa ajili ya ukumbusho wa kifo cha Yesu unaofanywa kila mwaka, ambao mwaka huu utaadhimishwa Siku ya Tatu, Aprili 16, baada ya jua kutua. (Luka 22:19, 20) Mwaka uliopita, makutaniko 94,600 ulimwenguni pote yaliripoti jumla kubwa ya watu 15,597,746 waliohudhuria! Hiyo ni hesabu ya zaidi ya watu 220,000 wa ziada kwa kulinganisha na hudhurio la mwaka uliopita.

5 Ni watu wangapi watakaohudhuria mwaka huu? Mengi yatategemea jitihada zetu zenye bidii za kutia wengine moyo wakusanyike pamoja nasi. Anza kwa kufanya orodha ya wale wote ambao ungependa kualika. Familia yako ya karibu ndiyo inayopaswa kuwa kwenye nafasi ya kwanza. Ikiwa una mwenzi asiyeamini, mwambie kwamba unatamani kwa moyo wote ahudhurie pamoja nawe. Mume mmoja asiyeamini alisema kwamba alihudhuria Ukumbusho mwaka uliopita kwa kuwa aliona kwamba kuwapo kwake kulikuwa na maana kubwa kwa mke wake. Unaweza kutia kwenye nafasi ya pili ya orodha yako watu wa jamaa, majirani, wafanyakazi wenzako, au wanashule wenzako. Uwe hakika kwamba unaalika wanafunzi wako wa Biblia.

6 Baada ya kufanya orodha yako, panga wakati wa kutoa mwaliko wa kibinafsi kwa kila mmoja. Tumia vikaratasi vilivyochapishwa kwa ajili ya Ukumbusho. Ili kusaidia watu wakumbuke wakati na mahali ambapo mwadhimisho utafanyikia, andika kwa mashine au chapa vizuri wakati na mahali pa Ukumbusho kwenye sehemu ya chini ya kikaratasi cha mwaliko. Tarehe ya Aprili 16 inapokaribia, kumbusha wale wanaopatikana kwenye orodha yako, ukiwatembelea kibinafsi au kwa njia ya simu. Acheni tusaidie wengi zaidi iwezekanavyo wawepo kwa ajili ya tukio hilo takatifu sana.

7 Tusaidie Wale Wanaohudhuria Ukumbusho: Kwa kawaida, usiku wa Ukumbusho ni pindi yenye kusisimua. Tuna nafasi ya kukaribisha watu ambao kwa kawaida hawahudhurii mikutano yetu. Chukua mipango ili ufike mapema na kubaki hadi nyuma, ikiwa hali za kwenu zinaruhusu. Chukua hatua ya kufahamiana na wapya waliohudhuria. Uwe mwenye shauku na mkaribishaji-wageni.—Rom. 12:13.

8 Je, watu fulani wanaohudhuria Ukumbusho wanaweza kusaidiwa wafanye maendeleo makubwa zaidi ya kiroho kupitia funzo la Biblia la nyumbani? Jitahidi kupata majina na anwani za wageni wowote ambao hawatembelewi kwa sasa ili kuendelea kuwasaidia. Ikiwa wanasaidiwa kwa upendo, wengine kati ya hao wanaweza kufanya maendeleo kufikia kustahili kuwa wahubiri wasiobatizwa kabla ya Ukumbusho wa mwaka ujao. Unapofanya ziara za kurudia kwa wale waliohudhuria Ukumbusho, waalike kwenye hotuba ya pekee itakayotolewa mnamo Aprili 27.

9 Je, Unaweza Kuwa Painia Msaidizi Mnamo Machi na Aprili? Kila mwaka bidii yetu kwa ajili ya Yehova inatuchochea kujitoa kikamili katika huduma mnamo ile miezi ya utendaji wa pekee. Jitihada zenye umoja za kutaniko nzima ili kuhubiri habari njema kwa bidii mnamo majira ya Ukumbusho zinaweza kutoa matokeo mazuri.

10 Kutaniko moja lenye wahubiri 107 na mapainia wa kawaida 9 liliripoti kwamba walikuwa na “mwezi wenye kutokeza” mnamo Aprili mwaka jana, kukiwa na wahubiri 53 waliotumika wakiwa mapainia wasaidizi, kutia ndani wazee na watumishi wa huduma wote. Wazee waliongezaje shauku kwa ajili ya utumishi wa painia msaidizi mwezi huo? Walianza mapema, wakitia moyo wengi zaidi iwezekanavyo ili wajiandikishe. Mikutano kwa ajili ya utumishi wa shambani ilifanywa pa wakati tofauti-tofauti katika siku ili ipatane na programu ya wote katika kutaniko. Mkazo wa pekee ulitiwa juu ya kutoa ushahidi kwa njia ya simu, zaidi sana kwa walio wadhaifu.

11 Dada mmoja mwenye umri wa miaka 86, ambaye hawezi kutembea kwa sababu ya matatizo ya afya, alijaza ombi ili kuwa painia msaidizi. Akianza asubuhi, angefanya saa mbili hivi akitoa ushahidi kwa njia ya simu alipokuwa akiketi kwenye meza ya jikoni; kisha, baada ya kupumzika kwa saa chache, angerudi na kutoa ushahidi zaidi kwa njia ya simu. Mtu mmoja aliyezungumza naye alikuwa amepoteza mume wake na wana wawili mnamo miaka miwili iliyotangulia, naye hakuelewa kwa nini Mungu aliruhusu mambo mabaya kama hayo yatukie. Ushahidi mzuri ulitolewa, na funzo la Biblia likaanzishwa. Kutoa ushahidi kwa njia ya simu jioni na wakati mwingine ni njia yenye matokeo ya kuzungumza na watu wanaoishi katika majengo makubwa-makubwa au maeneo ambayo si rahisi kuyafikia. Kunawezesha pia wahubiri wazungumze na watu ambao hawako nyumbani wakati wa mchana.

12 Wazee walimalizia ripoti yao kwa kusema: “Tulikuwa na wakati bora na tunathamini mapendeleo na baraka ambazo Yehova amewezesha kila mmoja wetu kuzifurahia.” Kwa kupanga mambo ifaavyo, kutaniko lenu pia linaweza kufurahia baraka kama hizo.

13 Tujitahidi Ili Sisi Sote Tushiriki Katika Huduma: Upendo wetu kwa Mungu na jirani unatuchochea kununua wakati kila mwezi ili kushiriki habari njema na wengine. (Mt. 22:37-39) Waangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko na wasaidizi wao wanapaswa kujitahidi kusaidia wale walio katika kikundi chao washiriki katika huduma kila mwezi. Njia nzuri ya kufanya hivyo ni kwa kuchukua mipango kimbele ili kuhubiri na watu fulani hasa katika kikundi. Kuliko kungoja mpaka mwisho wa mwezi ili kufanya hivyo, anzeni mapema. Hilo litawatolea nyinyi nafasi zaidi ili kutoa msaada wenye upendo.

14 Je, kikundi chenu cha funzo la kitabu kina wahubiri wadhaifu kimwili ambao wana matatizo makubwa ya kushiriki katika huduma? Ikiwa wengine kati yao wako katika makao ya matunzo au hawawezi kutoka nyumbani kwao, inaeleweka kwamba nafasi zao za kutoa ushahidi zitakuwa ndogo. Lakini kwa kutumia nafasi zao ndogo za kuacha nuru yao ing’ae, wanaweza kuchochea wale wanaoona kazi zao nzuri wapendezwe kabisa na kweli. (Mt. 5:16) Waangalizi wa funzo la kitabu wanapaswa kuhakikisha kwamba wahubiri hao wanajua kwamba wanaweza kuripoti utumishi wa shambani kwa vipindi vya wakati vya dakika 15. Kuweza kuripoti wakati wanaopitisha wakitoa ushahidi kunatia wahubiri hao waaminifu moyo, na kunawaletea furaha na kutosheka. Kunasaidia pia kuhakikisha kwamba ripoti ya utendaji ya watu wa Mungu ulimwenguni pote ni sahihi.

15 Vijana Wenye Shughuli Katika Kufanya Lililo Jema! Ni jambo lenye kuburudisha kama nini kuona vijana Wakristo wakitumia nguvu na nishati zao katika utumishi wa Yehova! (Mez. 20:29) Ikiwa wewe ni kijana, unawezaje kuonyesha bidii yako kwa ajili ya Yehova mnamo miezi hii ya pekee ya utendaji?

16 Kama haujakuwa bado mhubiri asiyebatizwa katika kutaniko, je, unaweza kujitahidi kufikia pendeleo hilo? Jiulize maulizo yafuatayo: ‘Je, nina ujuzi wa msingi kuhusu kweli ya Biblia? Je, ninataka kushiriki katika utumishi wa Ufalme? Je, mimi ni mfano mzuri katika mwenendo wangu? Je, mimi binafsi ninaweza kuonyesha imani yangu kwa kusema na wengine kuhusu habari njema? Je, ninachochewa na moyo wangu kufanya hivyo?’ Ikiwa unaweza kujibu ndiyo kwa maulizo hayo, basi zungumza na wazazi wako kuhusu tamaa yako ya kuwa mhubiri. Wazazi wako wanaweza kumwendea mmoja wa wazee wa halmashauri ya utumishi.

17 Ikiwa tayari wewe ni mhubiri wa habari njema, je, unaweza kutumia wakati wa mapumziko mnayopewa kutoka shuleni ili kushiriki zaidi katika huduma? Kwa kuwa na programu nzuri na kwa msaada wa wazazi na wengine, vijana wengi waliobatizwa wameweza kuwa mapainia wasaidizi. Ikiwa jambo hilo haliwezekani, basi azimia kushiriki zaidi katika huduma ya shambani. Jiwekee mradi. Zaidi ya mradi wa saa, jiwekee mradi mwingine kuhusiana na ubora wa huduma yako. Labda unaweza kujitahidi kusomea mtu andiko kwenye kila mlango, kuboresha ziara zako za kurudia, kuanzisha funzo la Biblia, au kupanua huduma yako ili kutia ndani kutoa ushahidi kwa njia ya simu au sehemu nyingine ya utumishi. Namna gani kuhusu mradi wa kuwa na jirani, mwanashule mwenzako, au mtu wa jamaa akiambatana nawe kwenye Ukumbusho mwaka huu? Kushiriki kikamili katika shughuli za kitheokrasi kutathawabisha na bila shaka kutatia wengine moyo katika kutaniko.—1 Thes. 5:11.

18 Tusaidie Wapya Wafanye Maendeleo: Mnamo mwaka wa utumishi uliopita, wastani wa mafunzo ya Biblia 224,318 yaliongozwa kila mwezi katika Congo-Kinshasa, na wastani ya mafunzo ya Biblia 14,192 katika Congo-Brazzaville. Baada ya wakati fulani, wengi wa wanafunzi hao watafanya maendeleo kufikia kujiweka wakfu na kubatizwa. Lakini, kabla hawajafikia mradi huo, tunapaswa kuwasaidia wastahili kuwa wahubiri wa habari njema. Hiyo ni hatua ya maana katika kufundisha wapya kuwa wafuasi wa Yesu Kristo. (Mt. 9:9; Luka 6:40) Je, una mwanafunzi wa Biblia aliye tayari kuchukua hatua hiyo?

19 Ikiwa hauna hakika kuhusu maendeleo ya mwanafunzi wako, tafuta msaada kutoka kwa mwangalizi wako wa funzo la kitabu au mwangalizi wa utumishi. Labda unaweza kumwalika ahudhurie funzo. Ndugu hao wana uzoefu wenye thamani unaoweza kutumiwa ili kukadiria maendeleo ya kiroho ya mwanafunzi. Wanaweza kuwa na madokezo ambayo yatasaidia mwanafunzi azidi kufanya maendeleo ya kiroho.

20 Wakati mwanafunzi wako anapoonyesha kwamba anapenda kuwa mhubiri asiyebatizwa, na ikiwa unahisi kwamba anastahili, zungumza na mwangalizi-msimamizi. Yeye atachukua mipango ili wazee wawili wakutane nawe na mwanafunzi ili waone ikiwa anastahili; watatumia habari kwenye ukurasa wa 98-9 wa kitabu Huduma Yetu. (Ona Mnara wa Mlinzi wa Novemba 15, 1988, ukurasa wa 17.) Ikiwa mwanafunzi anakubaliwa kuwa mhubiri, unapaswa kuanza kumzoeza papo hapo. Anapotoa ripoti ya utumishi wa shambani, kutaniko litajulisha kwamba mwanafunzi huyo ni mhubiri asiyebatizwa. Tunatumaini kwamba maelfu ya wahubiri wapya, vijana na wazee, wanaweza kufikia hatua hiyo ya maana mnamo miezi hii ya pekee ya utendaji.  

21 Kupanga Mambo Kunasaidia Kutimiza Mema Mengi Zaidi: Kupanga mambo kimbele kutachangia kufanikisha utendaji wetu mbalimbali wa kitheokrasi mnamo majira haya ya Ukumbusho. (Mez. 21:5) Kuna mambo mengi yanayohitaji uangalifu kwa upande wa wazee.

22 Ili kusaidia kutaniko lifanye mengi zaidi katika huduma ya shambani, wazee wanapaswa kuchukua mipango yenye kufaa ili kufanya mikutano kwa ajili ya utumishi wa shambani kila siku ya juma na kwenye mwisho-juma. Mwangalizi wa utumishi anapaswa kuchukua uongozi katika kufanya mipango hiyo. Je, mikutano ya ziada inaweza kupangwa mapema asubuhi, au jioni inapokaribia? Kutaniko linapaswa kujulishwa kuhusu mipango hiyo. Litakuwa jambo lenye kusaidia ikiwa programu inatiwa kwenye ubao wa matangazo.

23 Wazee wanapaswa kuhakikisha kwamba wamechukua mipango kwa ajili ya Ukumbusho kabla ya Aprili 16. Hiyo inatia ndani kusikilizana na makutaniko mengine kuhusu jinsi ya kutumia Jumba la Ufalme ikiwa makutaniko hayo yatakusanyikia hapo, kusafisha Jumba la Ufalme, kuchagua wakaribishaji na wahudumiaji, na kupata mifano. Kutaniko linapaswa kujulishwa kuhusu wakati na mahali pa Ukumbusho na kuhusu marekebisho mengine yoyote katika programu ya mikutano ya juma. Kushughulikia mambo hayo kwa bidii kutafanya mwadhimisho ‘utukie kwa adabu na kwa mpango.’—1 Kor. 14:40.

24 Labda vichwa vya familia watapenda kutumia sehemu ya funzo lao la familia ili kuzungumzia jinsi familia inavyoweza kushiriki katika utendaji wenye kuongezeka mnamo majira ya Ukumbusho. Je, familia yenu nzima inaweza kufanya utumishi wa painia msaidizi? Au, je, familia inaweza kutegemeza mshiriki mmoja au wengi katika kufanya hivyo? Ikiwa hilo haliwezekani, jiwekeeni miradi halisi mkiwa familia ili kupitisha wakati mwingi zaidi katika huduma. Je, kuna mtoto katika familia ambaye, kwa kutiwa moyo na kusaidiwa kidogo, anaweza kustahili kuwa mhubiri asiyebatizwa? Ni watu wangapi ambao familia yenu inaweza kualika kwenye Ukumbusho mwaka huu? Kupanga mambo vizuri kutaletea familia yenu baraka na furaha nyingi.

25 Tutumie Kikamili Wakati Unaobaki: Alipoandikia Wakristo wa karne ya kwanza, mtume Petro aliwakumbusha kwamba wakati uliomba kutenda haraka kwa kuwa mwisho wa mfumo wa mambo wa Kiyahudi ulikuwa umekaribia. (1 Pet. 4:7) Leo, mambo ya hakika yanaonyesha kwamba mwisho wa mfumo wa mambo wa sasa na wa ulimwenguni pote unakaribia. Siku kwa siku, maisha yetu yanapaswa kuonyesha kwamba tunasadiki jambo hilo. Tukiwa watumishi wa Yehova wenye bidii, tunapaswa kukaza fikira juu ya ile kazi ya haraka ya kutangaza habari njema.—Tito 2:13, 14.

26 Huu ni wakati wa kutenda kwa bidii! Tafakari juu ya yale ambayo Yehova amefanya kwa ajili yako, kwa ajili ya familia yako, na kwa ajili ya kutaniko. Ijapokuwa hatuwezi kamwe kumlipa kwa zile njia nyingi ambazo katika hizo ametufaidi, tunaweza kutolea Yehova ibada ya nafsi yote. (Zab. 116:12-14) Jitihada zetu zenye bidii zitathawabishwa kutoka juu. (Mez. 10:22) Sisi sote na tuwe “wenye bidii kwa lililo jema” mnamo wakati huu wa pekee wa utendaji wenye kuongezeka, “ili katika mambo yote Mungu apate kutukuzwa kupitia Yesu Kristo.”—1 Pet. 3:13; 4:11.

[Picture on page 3]

Hudhurio la Ulimwenguni Pote Kwenye Ukumbusho

199914,088,751

200014,872,086

200115,374,986

200215,597,746

[Picture on page 4]

Ni Nani Utakayealika Kwenye Ukumbusho?

□✔ Familia ya karibu na watu wa jamaa

□✔ Majirani na watu unaojuana nao

□✔ Wafanyakazi na wanashule wenzako

□✔ Ziara za kurudia na mafunzo ya Biblia

[Picture on page 5]

Saidia Wale Wanaohudhuria Ukumbusho

□✔ Wakaribishe kwa shauku

□✔ Watembelee baadaye

□✔ Watolee funzo la Biblia

□✔ Waalike kwenye hotuba ya pekee

[Picture on page 6]

Una Mradi Gani kwa Ajili ya Majira ya Ukumbusho?

□✔ Saidia mtu fulani uliyemwalika ahudhurie Ukumbusho

□✔ Timiza sifa za kuwa mhubiri wa habari njema

□✔ Pitisha hesabu fulani ya saa katika huduma

□✔ Boresha sehemu fulani ya huduma

□✔ Tumika ukiwa painia msaidizi

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine