Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/04 uku. 3-5
  • Endeleeni Kutangaza Kazi za Ajabu za Yehova

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Endeleeni Kutangaza Kazi za Ajabu za Yehova
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • ‘Hubiri Neno la Mungu Kikamili’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Tangazeni Mahali Pote Sifa Bora za Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Tutafute Mapainia Wasaidizi 100,000
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 2/04 uku. 3-5

Endeleeni Kutangaza Kazi za Ajabu za Yehova

1 Hakuna mtu yeyote anayeweza kujilinganisha na Mungu wetu mkuu, Yehova! Daudi aliandika: “Wewe mwenyewe umefanya mambo mengi, Ee Yehova Mungu wangu, naam, kazi zako za ajabu na mawazo yako kutuelekea; hakuna wa kulinganishwa nawe.” (Zab. 40:5) Kazi za ajabu za Yehova zinatia ndani uumbaji wa ulimwengu wote mzima, Ufalme wa Kimesiya, matendo ya fadhili-upendo kuelekea watu wake, na kampeni ya kuhubiri ulimwenguni pote. (Zab. 17:7, 8; 139:14; Dan. 2:44; Mt. 24:14) Upendo kwa Yehova na shukrani kwa yote ambayo amefanya hutuchochea kuwaambia wengine mambo yanayomhusu. (Zab. 145:5-7) Mnamo Machi, Aprili, na Mei, tutakuwa na nafasi ya kufanya hivyo kwa ukamili zaidi.

2 Kuwa Painia Msaidizi: Je, unaweza kupanga programu yako ili kutumia saa 50 katika huduma mwezi mmoja au zaidi mnamo miezi hii ya utendaji wa pekee? Bila shaka, marekebisho yoyote utakayofanya katika kawaida yako yatakuwa ya lazima. (Efe. 5:16) Wengi wametambua kwamba kufanya utumishi wa painia msaidizi kunawasaidia kuboresha huduma yao. Wanakuwa wenye kutulia zaidi kwenye mlango, na kufanya hivyo kunawatolea nafasi ya kutumia sana Biblia. Kutumia wakati zaidi katika huduma kunafanya iwe rahisi kurudilia wale walioonyesha kupendezwa kokote ili kuwasaidia, na wengine ambao hawakuongoza funzo la Biblia hapo zamani wameanzisha funzo moja walipofanya utumishi wa painia msaidizi. Kwa kuwa kufanya utumishi wa painia msaidizi kunaomba kujitahidi ili kusaidia wengine, ni utendaji wenye kuleta shangwe.—Mdo. 20:35.

3 Usiwe haraka kusema kwamba hali zako hazikuruhusu ushiriki utumishi wa painia msaidizi. Mzee mmoja aliyekuwa painia msaidizi mwaka uliopita anao watoto wawili na kazi ya kimwili ya wakati wote. Ndugu huyo mwenye shughuli nyingi alifanyaje hivyo? Kwa kuwa anatumika mnamo juma, alipanga kutumika sana katika utumishi kwenye miisho-juma, akianza na ushahidi wa barabarani Siku za Posho pa saa 1:00 ya asubuhi. Wengi katika kutaniko hilo waliokuwa na hali zenye kufanana na hizo walifanya pia utumishi wa painia msaidizi, na walitegemezana na kutiana moyo. Katika kutaniko lingine, dada mwenye umri wa miaka 99 aliamua kupainia katika Mei baada ya kualikwa na binti wake kukaa naye. Wengine katika kutaniko walimsaidia dada huyo mzeemzee kwenda nyumba kwa nyumba na kuongoza mafunzo ya Biblia wakisukuma kiti chake chenye magurudumu. Alishiriki pia katika kutoa ushahidi kwa njia ya simu, ushahidi wa barabarani, na kwa njia ya barua. Anaamini kwamba hilo lilifanywa, si kwa nguvu yake mwenyewe, lakini kwa msaada tu wa Yehova.—Isa. 40:29-31.

4 Jaribu kufanya programu inayolingana vizuri zaidi na hali zako. Programu za kielelezo zinazopatikana katika toleo hili zinaweza kusaidia. Je, una kazi ya kimwili ya wakati wote au unakwenda shuleni? Programu inayotumia zaidi miisho-juma inaweza kuwa yenye kufaa zaidi kwako. Ikiwa una matatizo ya afya na nguvu yako haikuruhusu kutumika sana katika huduma, programu inayoomba kutumia wakati mdogo kila siku inaweza kuwa bora zaidi. Ongea na wengine kuhusu tamaa yako ya kuwa painia msaidizi. Labda wao pia watafanya hilo liwe mradi wao.

5 Jinsi Vijana Wanavyoweza Kushiriki: Yehova ni mwenye kupendezwa wakati vijana wanaposema kuhusu kazi zake za ajabu. (Zab. 71:17; Mt. 21:16) Ikiwa wewe ni kijana aliyebatizwa, labda unaweza kuwa painia msaidizi mnamo mwezi mmoja wa wakati wa mapumziko ya shule. Ikiwa hauwezi kutumika ukiwa painia msaidizi, je, unaweza kujiwekea miradi kamili ili kuongeza ushirika wako na kuboresha huduma yako mnamo miezi hiyo? Ikiwa umekuwa mwenye kushiriki katika huduma pamoja na wazazi wako lakini haujakuwa mhubiri asiyebatizwa, sasa huu ndio wakati unaofaa wa kujaribu kuwa na sifa ya kustahili. Si lazima kufikiri kwamba unapaswa kuwa fundi katika kujibu maulizo ya Kibliblia au kwamba unapaswa kujua mambo mengi kadiri ambavyo watu wenye kubatizwa wenye umri mkuu wanavyojua. Je, unaelewa mafundisho ya msingi ya Biblia? Je, unashikamana sana na viwango vya maadili vya Biblia? Je, unapenda kujulikana kuwa Shahidi wa Yehova? Hivyo basi, ongea pamoja na wazazi wako kuhusu jambo hilo. Wanaweza kufanya mpango ili kukutana na wazee pamoja nawe kuona ikiwa unatimiza matakwa.—Ona kitabu Huduma Yetu, ukurasa 98-9.

6 Tusaidie Wengine Kuhubiri: Wanafunzi wa Biblia wenye kufanya maendeleo wanaweza kustahili ili kujiunga nasi wakiwa wahubiri mnamo miezi ijayo ya utendaji wa pekee. Ikiwa una mwanafunzi wa Biblia anayefanya maendeleo mazuri, tafuta msaada wa mwangalizi wako wa funzo la kitabu au wa mwangalizi wa utumishi. Mmoja wao anaweza kwenda nawe kwenye funzo hilo ili kukadiria maendeleo ya mwanafunzi. Ikiwa mwanafunzi huyo anastahili na ana tamaa ya kuwa mhubiri, mwangalizi msimamizi anaweza kupanga ili wazee wawili wakutane nawe pamoja na mwanafunzi huyo. (Ona Mnara wa Mlinzi, Novemba 15, 1988, ukurasa wa 17.) Mara tu mwanafunzi atakapokubaliwa, anza papohapo kumzoeza katika huduma.

7 Waangalizi wa funzo la kitabu wanapaswa kutoa uangalifu wa pekee kwa yeyote asiyetenda au asiye kawaida katika kikundi chao. Watolee mwaliko wa kipekee ili kutumika pamoja nawe katika huduma. Ikiwa wamekuwa wasiotenda kwa muda mrefu, ni jambo la hekima kwamba wazee wawili waongee nao kwanza kuona ikiwa wanastahili. (Ona Kisanduku cha Maulizo katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 2000.) Bidii ya kutaniko mnamo miezi hiyo ya utendaji wa pekee inaweza kuwachochea washiriki kwa ukawaida katika huduma mara nyingine tena.

8 Jitayarisheni Sasa kwa Ajili ya Utendaji Wenye Kuongezeka: Wazee, anzeni tangu sasa kusitawisha shauku katika kutaniko kuhusu utumishi wa painia msaidizi. Mnaweza kufanya mengi kupitia maelezo yenu yenye kutia moyo na mfano mzuri. (1 Pet. 5:3) Ni nini kilichokuwa kilele cha mapainia wasaidizi cha kutaniko lenu mwaka uliopita? Je, kinaweza kuwa juu mwaka huu? Waangalizi wa funzo la kitabu na wasaidizi wao wanapaswa kutafuta njia za kutia moyo wote katika kikundi waongeze utendaji wao. Waangalizi wa utumishi wanaweza kupanga mikutano ya ziada kwa ajili ya utumishi wa shambani. Julisheni kutaniko kimbele yale yanayopangwa. Hakikisheni kwamba wahubiri wenye kustahili wanapewa mgawo wa kuongoza mikutano hiyo na kwamba mikutano kwa ajili ya utumishi inaanza na kumalizika pa wakati. (Ona Kisanduku cha Maulizo katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 2001.) Mwangalizi wa utumishi anapaswa kuchukua mipango ili kuwe na maeneo, magazeti, na vichapo vya kutosha.

9 Mwaka uliopita wazee wa kutaniko moja walianza kimbele na kwa shauku kutia moyo wengine wafanye utumishi wa painia msaidizi, wengi wao walijaza fomu. Walipanga mikutano ya ziada kwa ajili ya utumishi wa shambani—mkutano moja pa saa 11:30 za asubuhi kwa kufanya ushahidi wa barabarani, mkutano mwingine pa saa 9:00 kisha mchana-kati kwa ajili ya wale wanaotoka shuleni, na mkutano wa tatu pa saa 12:00 kisha mchana-kati kwa ajili ya wale wanaotoka kazini. Kwa kuongezea, mikutano mitatu kwa ajili ya utumishi wa shambani ilipangwa Siku za Posho. Washiriki wa kutaniko waliitikia, wahubiri 66 walikuwa mapainia wasaidizi mnamo Aprili!

10 Kwa nini msiweke pembeni wakati, mtakapokuwa na funzo lenu la familia, ili mzungumzie namna ya kujiwekea miradi halisi kwa ajili ya miezi ijayo? Mkipanga mambo na kushirikiana vizuri, wengine au wote katika familia wanaweza kuwa mapainia wasaidizi. Ikiwa hilo haliwezekani, jiwekeeni miradi ya kuongeza utendaji wenu kwa kurefusha wakati wenu wa utumishi mnaozoea kufanya au kwa kuhubiri kwenye pindi nyingine. Msali kwa ajili ya jambo hilo mkiwa familia. Mnaweza kuwa hakika kwamba Yehova atabariki jitihada zenu.—1 Yoh. 3:22.

11 Kazi ya Ajabu Sana ya Mungu: Onyesho kubwa zaidi la upendo wa Yehova ni zawadi ya Mwana wake kuwa fidia kwa ajili yetu. (1 Yoh. 4:9, 10) Dhabihu ya fidia ni msingi halali ili kukomboa wanadamu kutoka dhambi na kifo. (Rom. 3:23, 24) Damu ya Yesu iliyomwagika ili kuhalalisha lile agano jipya, ilifanya iwezekane kwa wanadamu wasiokamilika wafanywe kuwa wana wa Mungu wakiwa na tazamio la kutawala katika Ufalme wa kimbinguni. (Yer. 31:31-34; Marko 14:24) Jambo la maana zaidi ni kwamba mwenendo mkamilifu wa Yesu wenye utii ulitakasa jina la Yehova. (Kum. 32:4; Met. 27:11) Siku ya Yenga, Aprili 4, kisha kutua kwa jua, Ukumbusho wa Kifo cha Yesu utaadhimishwa ulimwenguni pote.

12 Mwadhimisho wa Mlo wa Jioni wa Bwana unatukuza kazi za ajabu za Yehova. Hotuba hiyo inakuza shukrani na uelewevu wetu kuhusu yale Yehova alifanya katika kuandaa fidia. Wale wanaopendezwa watakaohudhuria wataweza kutazama kazi zingine za ajabu za Mungu. Wataweza kuona umoja na upendo wenye shauku ambao Yehova amefundisha watu wake kuonyesha. (Efe. 4:16, 22-24; Yak. 3:17, 18) Kuhudhuria tukio hili lenye maana kunaweza kuwa na uvutano kabisa juu ya namna mtu anavyofikiri, kwa hiyo tunataka tuwe wengi iwezekanavyo—2 Kor. 5:14, 15.

13 Tualike Wengine Kuhudhuria: Anza kujitayarisha sasa kwa kufanya orodha ya wale utakaoalika. Orodha yako inapaswa kutia ndani washiriki wa familia wasioamini, majirani, watu unaojuana nao kazini au shuleni, watu uliojifunza nao Biblia zamani na wale unaojifunza nao sasa, na watu wote unaorudilia. Waangalizi wa funzo la kitabu wanapaswa kutia ndani kwenye orodha yao wahubiri wote wasiotenda.

14 Tumia vikaratasi vya mialiko vilivyochapishwa kwa ajili ya Ukumbusho, na andika kwa mashine au uandike vizuri kwa kalamu wakati na mahali ambapo Ukumbusho utaadhimishwa. Au huenda utataka kutumia mwaliko unaopatikana kwenye ukurasa wa mwisho wa Mnara wa Mlinzi toleo la Machi 15, 2004, au Amkeni! toleo la Machi 22, 2004. Kwa kuwa Aprili 4 inakaribia, kumbusha wale wanaopatikana kwenye orodha yako; fanya hivyo kwa kuwatembelea ama kwa njia ya simu.

15 Kwenye Ukumbusho: Jaribu kufika mapema jioni hiyo ya Ukumbusho. Onyesha ukaribishaji kwa kusalimia kwa shauku wale walio wapya. (Rom. 12:13) Unalo daraka la pekee kuelekea wageni ambao umealika. Wafanye wajisikie kuwa wenye kukaribishwa, na uwaonyeshe kwa washiriki wengine wa kutaniko. Labda unaweza kuwasaidia wakae pembeni yako. Na ikiwa hana au hawana Biblia au kitabu cha nyimbo, fanya mpango ili afuate au wafuate katika Biblia au kitabu cha nyimbo pamoja nawe au na ndugu mwingine. Baada ya mwadhimisho, uwe tayari kujibu maulizo yote wanayoweza kuwa nayo. Ikiwa kwa wengine ni mara ya kwanza kuhudhuria, waulize ikiwa watapenda kujifunza mengi zaidi kuhusu Neno la Mungu na kusudi lake. Wapendekeze funzo la Biblia la nyumbani.

16 Tuendelee Kusaidia Wale Waliohudhuria: Katika majuma yanayofuata Ukumbusho, wale waliohudhuria wanaweza kuhitaji msaada zaidi. Hilo linahusu wale ambao walihudhuria mikutano kwa ukawaida hapo zamani lakini sasa hawashirikiane tena sana na kutaniko. Wazee watakuwa tayari kuona kwamba watu kama hao hawasahauliwe, wakitafuta kujua kwa nini walisimamisha kufanya maendeleo ya kiroho. Mfanye waone uharaka wa wakati. (1 Pet. 4:7) Tusaidie wote waone faida ya kutii himizo la Kimaandiko la kukusanyika pamoja kwa ukawaida na watu wa Mungu—Ebr. 10:24, 25.

17 Kazi za Yehova ni za ajabu mno kwa sisi kuzielewa kikamili hata ikiwa tunaishi milele. (Ayu. 42:2, 3; Mhu. 3:11) Kwa hiyo, hatutakosa kamwe mambo ya kutuchochea tumsifu. Kwenye majira haya ya Ukumbusho tunaweza kuonyesha shukrani kwa kazi za ajabu za Yehova kwa kufanya jitihada ya pekee ya kuongeza ushirika wetu katika huduma.

[Maulizo ya Funzo]

1. Ni kazi gani fulani za ajabu za Yehova ambazo unathamini hasa?

2. Tunafaidikaje sisi binafsi na kufanya utumishi wa painia msaidizi?

3. Wengine wamewezaje kuwa mapainia wasaidizi ijapokuwa hali zao ngumu?

4. Ni mambo gani tunayoweza kufikiria tunapofanya programu ili kuwa mapainia wasaidizi?

5. Vijana wanaweza kujiwekea miradi gani mnamo Machi, Aprili, na Mei?

6. Tunawezaje kusaidia wanafunzi wa Biblia wawe wahubiri wa habari njema?

7. Wahubiri wasio kawaida na wasiotenda wanawezaje kusaidiwa?

8, 9. Wazee wanaweza kufanya nini ili kuchochea shauku kwa ajili ya utendaji wa pekee?

10. Familia zinawezaje kujitayarisha ili kuongeza utendaji wao?

11. (a) Ni mambo gani ya ajabu sana ambayo dhabihu ya Yesu ilitimiza? (b) Ni wakati na mahali gani ambako Ukumbusho utaazimishwa katika eneo letu?

12. Jinsi gani kuhudhuria mwadhimisho wa Mlo wa Jioni wa Bwana kunavyoweza kuwafaidi wale wanaopendezwa?

13, 14. Ni nani tunaopaswa kualika kwenye Ukumbusho, na jinsi gani?

15. Tunawezaje kuonyesha ukaribishaji jioni hiyo ya Ukumbusho?

16. Ni nini kinachoweza kufanywa ili kusaidia wale waliohudhuria Ukumbusho wafanye maendeleo ya Kiroho?

17. Kwa nini tunapaswa kuendelea kusema kuhusu kazi za ajabu za Yehova?

[Kisanduku Kwenye Ukurasa wa 5]

Je, Unaweza Kuwa Painia Msaidizi kwa Kutumia Moja ya Programu Hizi?

Machi Siku Siku Siku Siku Siku Siku Siku Mwezi

ya ya ya ya ya ya ya

Yenga Kwanza*Pili*Tatu*Nne Tano Posho Jumla

Kila

Siku 2 1 1 1 1 1 5 51

Siku

Mbili 0 5 0 5 0 0 0 50

Miisho-

Juma tu 5 0 0 0 0 0 8 52

Miisho-

Juma na

Siku

mbili

za

Juma 2 0 0 2 0 2 6 50

Aprili Siku Siku Siku Siku Siku Siku Siku Mwezi

ya ya ya ya ya ya ya

Yenga Kwanza Pili Tatu Nne* Tano* Posho Jumla

Kila

Siku 2 1 1 1 1 1 5 50

Siku

Mbili 0 0 0 0 5 5 0 50

Miisho-

Juma tu 5 0 0 0 0 0 8 52

Miisho-

Juma na

Siku

Mbili

za

Juma 2 0 0 2 0 2 6 50

Mei Siku Siku Siku Siku Siku Siku Siku Mwezi

ya ya ya ya ya ya ya

Yenga*Kwanza*Pili Tatu Nne Tano Posho* Jumla

Kila

Siku 2 1 1 1 1 1 4 51

Siku

Mbili 0 5 0 0 0 0 5 50

Miisho-

Juma tu 3 0 0 0 0 0 7 50

Miisho-

Juma na

Siku

Mbili

za

Juma 2 0 0 2 0 2 5 51

* Tano katika mwezi

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine