Tangazeni Mahali Pote Sifa Bora za Yehova
1 “Ee Yehova, ukuu ni wako na nguvu na uzuri na utukufu na heshima; kwa maana kila kitu mbinguni na duniani ni chako.” (1 Nya. 29:11) Upendo na shukrani kwa Yehova vinatuchochea tufanye nini? Vinatuchochea ‘tutangaze mahali pote sifa bora zake yeye aliyetuita sisi kutoka katika giza kuingia katika nuru yake ya ajabu.’ (1 Pet. 2:9) Hatuwezi kuacha kuwaelezea wengine kuhusu mambo yanayomhusu Mungu wetu mkuu! Tutakuwa na nafasi kubwa za kutangaza sifa za Yehova mwezi wa 3, mwezi wa 4, na mwezi wa 5.
2 Kampanye ya Pekee Kuhusu Ukumbusho: Siku ya Kwanza, terehe 2 mwezi wa 4, tutakazia sifa bora za Yehova kwa kufanya ukumbusho wa Chakula cha Jioni cha Bwana. Vikaratasi vya mwaliko wa pekee kuhusu tukio hili la maana vitagawanywa ulimwenguni pote kuanzia tarehe 17 mwezi wa 3 mpaka tarehe 2 mwezi wa 4. Sisi wote tunatiwa moyo kushiriki kabisa katika kampanye hiyo. Huo utakuwa wakati mzuri kwa wapya kuanza kutangaza habari njema ikiwa wanatimiza matakwa. Ikiwa una mafunzo ya Biblia au watoto ambao wanatimiza matakwa, zungumza jambo hilo na wazee.
3 Kampanye hii itakuwa sawa na ile tuliyofanya kuhusu Mkusanyiko wa Wilaya wenye kichwa “Ukombozi Unakaribia!” Makutaniko yatatumiwa vikaratasi vya kutosha ili kualika watu hivi kwamba kila mhubiri anaweza kupokea vikaratasi 50 na kila painia anaweza kupokea vikaratasi 150. Uwe na maneno mafupi wakati unapomwalika mtu, labda unaweza kusema hvi: “Huu ni mwaliko wako kwenye tukio la maana linalokaribia katika mwaka huu. Utakaribishwa kwa furaha. Habari zaidi kuhusu tukio hilo inapatikana kwenye karatasi hii ya mwaliko.” Hata hivyo, ikiwa mwenye nyumba ana maulizo, chukua nafasi ya kumjibu. Habari inayopatikana katika kitabu Biblia Inafundisha kwenye nyongeza kuhusu Chakula cha Bwana cha Jioni kuanzia kwenye ukurasa wa 206, inaweza kusaidia kujibu maulizo yake. Siku za Posho na Siku za Yenga, tutatolea watu magazeti mapya pamoja na kikaratasi cha mwaliko wa pekee. Uwe mwangalifu ili kutambua kila mtu anayependezwa, na fanya mpango ili kumrudilia.
4 Inapowezekana, inafaa kumpatia mkononi kila mtu tunayemkuta nyumbani kikaratasi hicho cha mwaliko wa pekee. Kwa hiyo, andika wale ambao haukukuta nyumbani na ufanye mpango ili kuwarudilia tena wakati mwingine. Makutaniko ambayo yanabaki na sehemu kubwa ya vikaratasi vya mwaliko yanaweza kuyatolea wale ambao hawakukutwa nyumbani juma la mwisho mbele ya Ukumbusho, jambo hilo lifanywe tu juma hilo la mwisho. Usikose kuwapatia vikakaratasi vya mwaliko, watu ambao unarudilia kwa kawaida, watu unaojifunza nao Biblia, watu wa jamaa, wafanyakazi wenzako, majirani, na watu wengine unaowafahamu.
5 Kufanya Kazi ya Upainia Msaidizi: Je, unaweza kutangaza zaidi sifa bora za Yehova kwa kuwa painia msaidizi mwezi wa 3, wa 4 na wa 5? Labda hilo litaomba ufanye mabadiliko fulani katika programu yako ya kila siku. (Efe. 5:15-17) Uwe hakika kwamba kujikaza ili kufanya mengi zaidi katika kazi ya Yehova kutakuletea furaha na pia baraka ya Yehova. (Met. 10:22) Kwa kuwa kipindi cha ukumbusho kinakaribia, sasa huu ndio wakati wa kuanza kufanya mipango.—Met. 21:5.
6 Dada mmoja mwenye umri wa miaka 90 alifurahia pendeleo la kuwa painia msaidizi mwaka uliopita. Alisema hivi: “Ijapokuwa ninapenda sana kazi ya kulima na nilitaka kuanza kupanda, nilitambua kwamba nilihitaji kupanga mambo ya kuweka pa nafasi ya kwanza. Nikiwa na tamaa ya kuweka faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza, niliamua kufanya upainia msaidizi mwezi wa 3.” Je, dada huyo alibarikiwa kwa kufanya hivyo? Anasema, “Ninajisikia sana kuwa karibu na kutaniko na hilo limenifanya kuwa karibu na Yehova.” Je, tunaweza kuchunguza mambo tunayopaswa kutia pa nafasi ya kwanza na kufanya mabadiliko ya namna hiyo ikiwa yanahitajiwa?
7 Painia msaidizi anaombwa kutimiza saa 50. Hilo si jambo gumu kama unavyofikiri. Fikiria katika sala kazi mbalimbali unazofanya kila siku, fanya programu, na kisha uiandike mahali unapoandika programu ya utendaji wako mbalimbali wa kitheokrasi. Wewe mwenyewe unajua hali zako vizuri zaidi. Ikiwa afya yako si nzuri na ikiwa unakosa nguvu, labda unaweza kuhubiri saa mbili kila siku. Ikiwa una kazi ya kimwili inayokuchukua wakati wote au ikiwa unakwenda masomoni, unaweza kufanya upainia msaidizi kwa kuhubiri jioni au Siku za Posho na Siku za Yenga.
8 Wengi wamefanya iwezekane kwamba washiriki wote wa familia wafanye kazi ya upainia msaidizi. Katika miaka iliyopita ndugu mmoja na mke wake walisita kuwa mapainia wasaidizi kwa sababu waliona kwamba hali zao hazingewaruhusu. Walifanya nini kuhusu jambo hilo? “Tulimwomba Yehova atusaidie tutimize jambo ambalo kwa muda mrefu tulitaka kufanya pamoja.” Kupanga mambo vizuri kuliwasaidia wafikie jambo walilokusudia. Waliongeza hivi: “Lilikuwa jambo bora sana. Tulibarikiwa sana. Tunawapendekeza kwamba mujaribu nanyi pia. Ikiwa sisi tuliweza kufanya hivyo, ninyi pia mnaweza kufanya hivyo.”
9 Wakati wa funzo lenu la familia linalokuja, mnaweza kutumia wakati fulani ili kuchunguza namna ninyi wote katika familia mnaweza kuongeza saa mnazotumia katika kazi ya kuhubiri katika miezi inayokuja. Hata ikiwa huenda isiwezekane kwamba ninyi wote katika familia mufanye kazi ya upainia msaidizi, labda mtu mmoja anaweza kufanya hivyo ikiwa wengine wanamsaidia na kumuunga mkono. Ikiwa sivyo, ikiwezekana, washiriki wa familia yenu wanaweza kujitilia miradi ya kuongeza saa watakazopitisha katika mahubiri katika miezi hii ya utendaji wa pekee.
10 Musaidiane: Bidii inaweza kuwaambukiza wengine. Sema kuhusu tamaa yako ya kufanya upainia. Hilo linaweza kutia wengine moyo kufanya hivyo. Zaidi ya hilo, wale ambao wamefanya upainia wakati uliopita wanaweza kukutolea mapendekezo yatakayokusaidia upange mambo yako na kufanya programu ili kufikia kusudi lako. (Met. 15:22) Ikiwa unaweza kufanya upainia msaidizi, kwa nini usialike mhubiri mwengine, labda ndugu au dada mwengine aliye katika hali kama zako, ili akuunge mkono katika utendaji huu wenye kupendeza?
11 Wazee wengi wamefanya mipango ya lazima ili kushiriki katika aina hii ya utumishi. (Ebr. 13:7) Wazee wanapofanya hivyo makutaniko yanatiwa moyo! Kwa mazungumzo yao wazee wanachochea pia hamu hiyo kwa wengine. Maneno machache yenye kutia moyo au mapendekezo fulani yenye kufaa huenda ndilo jambo tu linalohitajiwa ili kuchochea watu fulani wafanye kazi ya upainia msaidizi. Mwangalizi wa utumishi anaweza kupanga mikutano mingine kwa ajili ya kazi ya kuhubiri ili wote wapate nafasi ya kuhubiri pamoja na wengine, hata kisha kazi au kisha kutoka masomoni. Mipango hiyo inapaswa kutangazwa kwa ukawaida. Atahakikisha pia kwamba eneo la kuhubiri limetayarishwa vya kutosha na pia kwamba kuna vitabu vya kutosha.
12 Ijapokuwa huenda hali zisikuruhusu ufanye kazi ya upainia msaidizi, unaweza kuwatia moyo wale walioomba kufanya kazi ya upainia msaidizi, na unaweza kusali kwa ajili yao. (Met. 25:11; Kol. 4:12) Unaweza kufanya mipango ili kuhubiri nao siku fulani ingine katika juma au kupitisha saa nyingi katika mahubiri kuliko ilivyo kawaida yako.
13 Tunapenda Kufikia Hesabu ya Mapainia Wasaidizi 22,750 Katika Mwezi wa 4: Katika mwaka wa 2000, Congo-Brazzaville ilifikia hesabu kubwa ya mapainia wasaidizi 556, na katika mwaka wa 1997 Congo-Kinshasa ilifikia hesabu kubwa ya mapainia wasaidizi 8,260. Kwa hiyo, mradi wa kufikia katika mwezi wa 4 ujao ni wa mapainia wasaidizi 750 katika Congo-Brazzaville na mapainia wasaidizi 22,000 katika Congo-Kinshasa. Ikiwa katika kila kutaniko mhubiri mmoja kati ya wahubiri sita atafanya kazi ya upainia msaidizi, tunaweza kufikia mradi huo. Kwa kweli, makutaniko mengine yatakuwa hata na wahubiri zaidi ambao hali zao zitawaruhusu wafanye kazi ya upainia msaidizi. Ni kweli kwamba makutaniko mengi yatafikia mradi huo kwa urahisi. Kufanya hivyo kutasisimua kabisa kutaniko lenu na kutaleta matokeo mazuri ya kazi ya kuhubiri katika eneo lenu.
14 Kwa nini mwezi wa 4 ni mwezi mzuri ili kufanya kazi ya upainia msaidizi? Ukumbusho utafanywa mwanzoni mwa mwezi, hilo litatutolea nafasi kubwa ya kutembelea wale watakaohuzuria. Tutatolea watu magazeti, tukiwa na kusudi la kuwaachia kitabu Biblia Inafundisha tutakapowarudilia na kuanzisha hivyo mafunzo ya Biblia. Kwa hiyo, kufanya kazi ya upainia msaidizi katika mwezi wa 4 kutatutolea nafasi nyingi za kuanzisha mafunzo ya Biblia. Zaidi ya hilo, mwezi wa 4 una Siku za Yenga tano na sikukuu ya ulimwengu, hilo litafanya iwe rahisi sana kwa wale wanaofanya kazi ya kimwili na wale wanaosoma wawe mapainia wasaidizi.
15 Kila kipindi cha Ukumbusho kinachopita kinapunguza sana siku zinazobaki za mwisho wa ulimwengu huu. Wakati unaobaki wa kuelezea wengine mambo yanayomhusu Mungu wetu mkuu umepunguka. (1 Kor. 7:29) Kipindi hiki cha Ukumbusho kitakapokuwa kimepita, nafasi bora ambazo tulipewa ili kumsifu Baba wetu wa mbinguni zitakuwa zimepita kwa milele, yaani, hazitarudi tena hata kidogo. Na tujitayarishe sasa kufanya yote tuwezayo mwezi wa 3, wa 4, na wa 5 ili kutangaza mahali pote sifa bora za Yehova!
[Maulizo ya Funzo]
1. Ni nini kinachotuchochea kutangaza mahali pote sifa bora za Yehova?
2. Ni kampanye gani ya pekee inayopangwa kuhusu Ukumbusho, na ni nani anayepaswa kushiriki katika kampanye hiyo?
3. Tunaweza kusema nini ili kualika watu kwenye Ukumbusho?
4. Vikaratasi vya mwaliko wa pekee kuhusu Ukumbusho vitagawanywa namna gani?
5. Kwa nini tunapaswa kuanza tangu sasa kufanya mipango ili kufanya kazi ya upainia msaidizi?
6. Tunaweza kujifunza nini kutokana na mfano wa dada mwenye umri wa miaka 90, aliyefanya upainia msaidizi mwaka uliopita?
7. Je, ni jambo gumu kutumika kama painia msaidizi?
8. Ni nini iliyosaidia ndugu mmoja na mke wake kufanya kazi ya upainia msaidizi?
9. Munaweza kufanya nini wakati wa funzo lenu la jamaa linalokuja ili kujitayarisha kwa ajili ya miezi inayokuja ya utendaji wa pekee?
10. Kwa nini tunapaswa kuwaelezea wengine kuhusu tamaa yetu ya kufanya upainia msaidizi katika kipindi hiki cha Ukumbusho?
11. Namna gani wazee wanaweza kuchochea hamu ya kufanya kazi ya upainia msaidizi katika miezi inayokuja?
12. Unaweza kufanya nini ikiwa hali hazikuruhusu kufanya kazi ya upainia msaidizi?
13. Congo-Brazzaville na Congo-Kinshasa zimetiliwa mradi gani, na kutaniko lenu linaweza kufanya nini ili kufikia mradi huo?
14. Kwa nini mwezi wa 4 ni mwezi mzuri sana ili kufanya upainia msaidizi?
15. Kwa nini tunapaswa kutambua uhitaji wa kutenda kwa haraka kadiri kipindi hiki cha Ukumbusho kinavyokaribia?
[Kisanduku kwenye ukurasa wa 4]
Je, Tunaweza Kufikia Mapainia Wasaidizi 22,750 Mwezi wa 4?
[Kisanduku kwenye ukurasa wa 4]
◼ Chunguza mambo unayopaswa kutia pa nafasi ya kwanza
◼ Mzungumze miradi yenu katika familia
◼ Elezea wengine mipango yako