Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 7/13 uku. 7
  • Majibu kwa Maulizo Yenu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Majibu kwa Maulizo Yenu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mazungumuzo ya Kumalizia Pamoya na Wale Wenye Watabatizwa
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Wahubiri wa Habari Njema
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Nyongeza
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Ubatizo Ni Hatua Inayomuongoza Mutu Kwenye Uhusiano Muzuri Pamoja na Mungu
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2013
km 7/13 uku. 7

Majibu kwa Maulizo Yenu

◼ Mbele muhubiri akubaliwe kubatizwa, ni lazima awe amehuzuria mikutano na kuhubiri kwa muda gani?

Kubatizwa ndio uamuzi wa maana zaidi ambao mutu anafanya. Ndiyo sababu, mbele mutu akubaliwe kubatizwa, anapaswa kuelewa vizuri yale ambayo Mungu anataka afanye. Tena, anapaswa kuwa amekwisha kuonyesha kwamba ameazimia kuishi kulingana na mapenzi ya Mungu.

Wakristo wameamuriwa wasiache kukusanyika pamoja; kwa hiyo wazee wanapaswa kuhakikisha kwamba muhubiri asiyebatizwa anahuzuria kwa ukawaida mikutano ya kutaniko. (Ebr. 10:24, 25) Kwa kawaida ni vizuri pia awe mwenye kutoa maelezo kwenye mikutano. Ni vizuri pia awe amejiandikisha kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi, hata ikiwa si jambo linaloombwa ili kubatizwa.

Pia, kwa kuwa Wakristo wamepewa daraka la kuhubiri habari njema na kufanya wanafunzi, muhubiri anapaswa kuhubiri kwa ukawaida mbele ya kubatizwa. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Anapaswa kuwa amehubiri kwa miezi mingapi ili abatizwe? Kwa kawaida, anapaswa kuwa amehubiri muda wa kutosha ili aonyeshe kwamba ameazimia kabisa kuhubiri kwa ukawaida na kwa bidii mwezi baada ya mwezi. (Zab. 78:37) Lakini, si lazima kuwe kumepita muda murefu sana tangu aanze kuhubiri mupaka akubaliwe kubatizwa; miezi michache inaweza kutosha. Anapaswa kuripoti saa ngapi kila mwezi? Hakuna sheria kamili kuhusu jambo hilo. Wazee wanapaswa kuchunguza hali ya kila muhubiri na kumuelewa kulingana na hali yake.—Luka 21:1-4.

Wazee (ao watumishi wa huduma katika makutaniko ambamo kuna wazee wachache sana) wanaokutana na muhubiri ambaye anataka kubatizwa wanapaswa kukumbuka kwamba kila mutu iko tofauti na mwengine, na wanapaswa kutumia hekima wanapoamua ikiwa anastahili kubatizwa ao hapana. Watachunguza ikiwa kwa kweli anataka kuwa Shahidi wa Yehova na ikiwa ameonyesha kwamba anapendezwa na pendeleo la kujiunga na tengenezo la Yehova na kuhubiri habari njema. Wazee wanaelewa kwamba bado hajakomaa kiroho ao hajakuwa na ufundi kama wahubiri waliobatizwa wenye uzoefu. Ikiwa wazee wanaona kwamba muhubiri hastahili kubatizwa, wanapaswa kumujulisha kwa upole sababu zinazotegemea Maandiko zinazowachochea waamue kwamba hastahili kubatizwa, na kufanya mipango ili apokee musaada wa kiroho.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine