Programu ya Juma Tokea Tarehe 29 Mwezi wa 8
JUMA TOKEA TAREHE 29 MWEZI WA 8
Wimbo 33 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
bt sura ya 8 fu. 17-24 kisanduku kwenye uku. 67 (Dak. 25)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Zaburi 110-118 (Dak. 10)
Kujikumbusha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi (Dak. 20)
□ Mkutano wa Utumishi:
Wimbo 128
Dak. 10: Matangazo. Kwa kutumia utoaji wenye kupendekezwa ulio kwenye ukurasa huu, mufanye onyesho kuhusu jinsi funzo la Biblia linavyoweza kuanzishwa Siku ya Posho ya kwanza ya mwezi wa 9. Tia wote moyo kuhubiri siku hiyo ili kuanzisha funzo. Zungumzia habari “Tolea Watu Magazeti ya Zamani ao Broshua Yoyote Inayozungumzia Habari Zinazowapendeza.” Itolewe kama hotuba.
Dak. 15: Wenye Bidii, Ijapokuwa Wamezeeka. Mazungumzo yenye kutegemea Kitabu cha Mwaka cha 2011, ukurasa wa 61, fungu la 1-2; ukurasa wa 67, fungu la 1, na ukurasa wa 135, fungu la 2, mpaka ukurasa wa 136, fungu la 1. Omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu mambo wanayojifunza kutokana na habari hizo.
Dak. 10: Tujitayarishe Kutolea Watu Magazeti Katika Mwezi wa 9. Mazungumzo. Kwa muda wa dakika moja ao mbili, zungumzia habari fulani zilizo katika magazeti hayo. Kisha chagua habari mbili ao tatu, na omba wasikilizaji wapendekeze maulizo na maandiko ambayo wanaweza kutumia wanapotolea watu magazeti hayo. Mufanye onyesho kuhusu jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa.
Wimbo 122 na Sala