Kujikumbusha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maulizo yanayofuata yatatumiwa kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi katika juma tokea tarehe 29 mwezi wa 8, 2011.
1. Namna gani fazili zenye upendo za Mungu ni “bora kuliko uzima”? (Zab. 63:3) [w01 10/15 uku. 15 fu. 17]
2. Zaburi ya 70 inaonyesha nini kumhusu Daudi? [w08 9/15 uku. 4 fu. 4]
3. Zaburi 75:5 inatuonya tuepuke nini? [w06 7/15 uku. 11 fu. 2]
4. Tunaweza kumtazamia Yehova asikilize sala zetu wakati gani? (Zab. 79:9) [w06 7/15 uku. 12 fu. 5]
5. ‘Mambo yaliyofichwa’ yanayozungumziwa kwenye Zaburi 90:7, 8 ni nini? [w01 11/15 uku. 12-13 fu. 14-16]
6. Kama inavyoonyeshwa katika Zaburi 92:12-15, watu wenye kuzeeka wana daraka gani la maana katika kutaniko? [w04 5/15 uku. 13-14 fu. 15-18]
7. Je, maneno yaliyo katika Zaburi 102:25-27, yanapinga kusudi la Mungu la milele kwa dunia? (Mwa. 1:28) [w08 4/1 uku. 12 fu. 1]
8. Katika Zaburi 106:7, tunajifunza nini kuhusiana na ufahamu? [w95 9/1 uku. 19 fu. 4–uku. 20 fu. 2]
9. Kulingana na Zaburi 110:1, 4, Yehova ameapa namna gani kuhusu Mzao aliyeahidiwa, ao Masihi, na hilo litaletea wanadamu wote baraka gani? [cl uku. 194 fu. 13]
10. Mtunga–zaburi alipata matokeo gani kwa kutafakari kuhusu faida alizopata kwa kumtumikia Mungu? (Zab. 116:12, 14) [w09 7/15 uku. 29 fu. 4-5]