Matangazo
◼ Kichapo cha kutolea watu katika mwezi wa 8: Broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 inaweza kutumiwa: Endeleeni Kukesha!, Jambo Gani Hutufikia Tunapokufa?, Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Kuishi Milele Duniani Katika Furaha!, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Roho za Wafu—Je, Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Mwezi wa 9: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Tujikaze sana ili kuanzisha mafunzo ya Biblia tunapomhubiria mutu kwa mara ya kwanza.
◼ Tafazali, tunawakumbusha tena kwamba moja kati ya madaraka ya mwangalizi wa kikundi cha mahubiri ni kusaidia kukusanya ripoti za utumishi za wahubiri na mapainia wa kikundi chake. Hilo litasaidia Betheli kukusanya pa wakati ripoti za makutaniko yote mwisho wa kila mwezi. Ni lazima kufanya hivyo katika mwezi wa 8 na wa 9 ili ripoti zote ziwe tayari na kutiwa katika ripoti ya utumishi wa shambani ya mwaka. (Ona kitabu Tengenezo sura ya 5 uku. 45).
◼ Tunapenda kuwajulisha kwamba kikundi kinachotegemea kutaniko fulani, kinapaswa kutuma ripoti ya utumishi kwa kutaniko hilo wala si kuituma mara moja kwenye Betheli. Ripoti hiyo itaongezwa kwenye ripoti ya kutaniko wanalotegemea na itatumwa yote pamoja kwenye Betheli.
◼ Programu za video Mashahidi wa Yehova—Imani Yenye Matendo, Sehemu ya 1: Kutoka Gizani na pia Maajabu ya Uumbaji Yanafunua Utukufu wa Mungu, zitachunguzwa kwenye Mikutano ya Utumishi inayokuja. Ikihitajiwa, mufanye ombi kupitia kutaniko haraka iwezekanavyo ili kupata video hizo.