Programu ya Juma Tokea Tarehe 26 Mwezi wa 9
JUMA TOKEA TAREHE 26 MWEZI WA 9
Wimbo 101 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
bt sura ya 10 fu. 1-9, kisanduku kwenye uku. 79 (Dak. 25)
□ Shule ya Huduma ya Kiteokrasi:
Usomaji wa Biblia: Zaburi 142-150 (Dak. 10)
Na. 1: Zaburi 144:1–145:4 (Isipite dak. 4)
Na. 2: Je, Ufalme wa Mungu Ulianza Kutawala Katika Karne ya Kwanza?—rs uku. 318 fu. 2-4 (Dak. 5)
Na. 3: Kwa Nini Tunapaswa Kuepuka “Matendo ya Kupendelea”?—Yak. 2:1-4 (Dak. 5)
□ Mukutano wa Utumishi:
Wimbo 56
Dak. 10: Matangazo. Zungumuzia habari yenye kichwa “Njia Moja ya Kutumia Broshua Biblia Ina Ujumbe Gani?” Kwa kutumia utoaji unaopendekezwa kwenye ukurasa wa 4, mufanye onyesho kuhusu jinsi ya kuanzisha funzo la Biblia Siku ya Posho, tarehe 1 mwezi wa 10. Tia wote moyo washiriki katika mahubiri siku hiyo.
Dak. 10: Kisanduku cha Maulizo. Mazungumuzo. Tia ndani maelezo ya Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 3, 2005, ukurasa wa 6.
Dak. 15: Tujitayarishe Kutolea Watu Magazeti Katika Mwezi wa 10. Mazungumuzo. Kwa muda wa dakika moja ao mbili, zungumuzia habari fulani zinazoweza kupendeza sana watu katika eneo lenu. Kisha, onyesha jinsi habari mbili ao tatu zinaweza kutumiwa ili kutolea mutu gazeti. Zungumuzia habari moja moja. Fanya hivyo kwa kuomba wasikilizaji wapendekeze maulizo yanayoamusha kupendezwa ambayo wanaweza kuuliza watu na kisha uwaombe wapendekeze maandiko wanayoweza kusoma. Kwa kuwa Amkeni! ya mwezi wa 10 ni Amkeni! ya pekee, omba wasikilizaji waeleze ni watu gani wanaoweza kupendezwa na Amkeni! hiyo na jinsi tunavyoweza kufanya ili kuitolea watu wengi zaidi. Mufanye onyesho kuhusu jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa. Ikiwa hamujapata magazeti ya mwezi wa 10, mutumie magazeti ambayo kutaniko lilipata hivi karibuni.
Wimbo 41 na Sala