Matangazo
◼ Mwezi wa 2: Tutatolea watu kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Mwezi wa 3: Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Mujikaze sana kuanzisha mafunzo ya Biblia munapohubiria mutu. Ikiwa mutu amekwisha kupata kitabu hicho na anakataa kujifunza Biblia, muhubiri anaweza kumutolea gazeti fulani la zamani ao broshua yoyote inayozungumuzia mambo yenye kumupendeza.
◼ Hotuba ya pekee itatolewa Siku ya Posho ao Siku ya Yenga kisha Ukumbusho, ni yenye kichwa “Je, Unafikiri Kwamba Mwisho Ungali Mbali Sana?”
◼ Ikiwa mutu anapanga kusafiri katika inchi fulani ambayo haipatikani kwenye ripoti ya mwaka wa utumishi ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote, ao ikiwa haipatikani kwenye adresi ya inchi zinazopatikana kwenye ukurasa wa mwisho wa Kitabu cha Mwaka cha hivi karibuni, anaweza kuandikia biro ya tawi ya inchi yake ili ajue mipango ya kuchukua. Hilo litamusaidia kuepuka hatari fulani ao kujua maagizo fulani ya kipekee anayopaswa kufuata. Labda kazi yetu imekatazwa na serikali katika inchi hiyo. (Math. 10:16) Katika inchi fulani labda si jambo la hekima kuonana na Mashahidi wa mahali hapo ao na makutaniko. Kwa hiyo, biro ya tawi inaweza kukujulisha lile unaloweza kufanya ili kuhubiri katika inchi kama hizo ao vitabu gani unapaswa kubeba. Kufuata mashauri ya biro ya tawi kunaweza kukusaidia uepuke matatizo, na pia uepuke kuletea ndugu magumu.—1 Kor. 14:33, 40.
◼ Katika kitabu ks10-SW ukurasa wa 112, wazee wa kutaniko wavute mahali panapoandikwa w99 1/11 uku. 28-29 na waandike km 6/05 Cn uku. 5.
◼ Kwa sababu ya matukio fulani ya pekee ambayo yanatazamiwa katika mwezi wa 4 na wa 5, kuanzia tarehe 9 mupaka tarehe 20 mwezi wa 4, 2012 na kuanzia tarehe 21 mwezi wa 5 mupaka tarehe 1 mwezi wa 6, 2012, watu hawaruhusiwi kutembelea Beteli, makutaniko pia hayaruhusiwi.
◼ Mwandishi wa kutaniko na mwangalizi wa utumishi wanapaswa kuchunguza utendaji wa mapainia wa kawaida katikati ya mwaka wa utumishi. Wazee watasaidia painia yeyote aliye na tatizo la kueneza saa.