Matangazo
◼ Vichapo vya kutolea watu katika Mwezi wa 4 na wa 5: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo watu wanapendezwa, tuwatolee trakti Je, Ungependa Kujua Kweli? na tujikaze sana ili kuanzisha mafunzo ya Biblia. Tunapowarudilia wale waliohuzuria Ukumbusho ao matukio mengine ya kiteokrasi lakini hawajiunge kabisa na kutaniko, tuwe na kusudi la kuanzisha mafunzo katika kitabu Biblia Inafundisha. Mwezi wa 6: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Mujikaze kuanzisha mafunzo ya Biblia munapomuhubiria mutu kwa mara ya kwanza. Ikiwa mutu amekwisha kupata kitabu hicho na anakataa kujifunza Biblia, muhubiri anaweza kumutolea gazeti fulani la zamani ao broshua yoyote inayozungumuzia mambo yenye kumupendeza.
◼ Programu ya mikutano ya juma linalotangulia juma la mukusanyiko wa wilaya inaweza kubadilishwa ili kurudilia mashauri na mambo ya kukumbuka ya mukusanyiko wa wilaya. Mwezi moja ao miezi miwili kisha mukusanyiko wenu, munaweza kutumia sehemu ya mahitaji ya kutaniko lenu ili kurudilia habari za mukusanyiko ambazo wahubiri waliona kuwa zenye kusaidia katika mahubiri.
◼ Ikiwa utasafiri na unapanga kuhuzuria mukusanyiko wa wilaya katika inchi nyingine, unaweza kupata habari juu ya jambo hilo kwenye adresi yetu ya internet jw.org. Fungua consultation na kisha fungua Assemblée.