Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi
Maulizo yanayofuata yatatumiwa kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi katika juma tokea tarehe 25 mwezi wa 6, 2012. Tarehe ambayo kila jambo litazunguziwa inaonyeshwa pia ili kusaidia watu kutafuta majibu katika vitabu wanapotayarisha masomo ya huduma ya kila juma.
1. Tunaweza kujifunza nini juu ya namna Yehova alivyomutegemeza Yeremia wakati wa magumu? (Yer. 37:21) [Tokea tarehe 7 mwezi wa 5, w97 15/9 uku. 3 fu. 4–uku. 4 fu. 1]
2. Namna gani Wakristo walio na tumaini la kuishi milele duniani wanaiga mufano muzuri wa Ebed-meleki? (Yer. 38:8-13) [Tokea tarehe 7 mwezi wa 5, su uku. 179 fu. 9]
3. Kwa kuwa Yehova alitumia walinzi wa Nebukadneza ili kulinda Yeremia na Baruku, je, ni jambo lenye kufaa leo Wakristo watafute ulinzi wa polisi wenye silaha? (Yer. 39:11-14) [Tokea tarehe 14 mwezi wa 5, w84 1/8 uku. 24]
4. “Makuu” ambayo labda Baruku alikuwa akijitafutia yalikuwa mambo gani, na tunajifunza nini kutokana na namna alivyokubali shauri la Yehova? (Yer. 45:5) [Tokea tarehe 21 mwezi wa 5, w06 15/8 uku. 18 fu. 2; uku. 19 fu. 6]
5. Alipozungumuza juu ya kuazibu Edomu kwa haki, sababu gani Yehova alionyesha kama alikuwa tofauti na “wakusanya-zabibu” na “wezi”? (Yer. 49:9, 10) [Tokea tarehe 28 mwezi wa 5, w77-F 1/11 uku. 666 fu. 1–uku. 667 fu. 1]
6. Ni mambo gani ya maana ambayo tunaweza kujifunza kutokana na yale yaliyomupata mufalme Sedekia kwa kuwa ‘alimuasi mufalme wa Babiloni’? (Yer. 52:3, 7-11) [Tokea tarehe 4 mwezi wa 6, w88 9/15 uku. 17 fu. 8; w81-F 1/7 uku. 13 fu. 3-4; uku. 14 fu. 6]
7. “Kiti cha miguu” cha Yehova ni nini na “kibanda” chake ni nini? (Omb. 2:1, 6) [Tokea tarehe 11 mwezi wa 6, w07 1/6 uku. 9 fu. 2]
8. Yeremia alimaanisha nini aliposema kama Yehova ‘atakumbuka na kuinama’ juu yake na sababu gani maneno hayo ni ya maana kwetu? (Omb. 3:20) [Tokea tarehe 18 mwezi wa 6, w07 1/6 uku. 11 fu. 3]
9. Sababu gani ni vizuri mutu ajifunze kuchukua nira ya mateso, ni kusema, kuvumilia mateso wakati wa ujana? (Omb. 3:27) [Tokea tarehe 18 mwezi wa 6, w07 1/6 uku. 11 fu. 5; w87 15/2 uku. 24 fu. 1]
10. Namna gani mufano wa Ezekieli unatusaidia kusema na watu bila woga hata ikiwa wengine hawapendezwi na ujumbe wetu? (Eze. 3:8, 9) [Tokea tarehe 25 mwezi wa 6, w08 15/7 uku. 8 fu. 6-7]