Matangazo
◼ Mwezi wa 6: Tutatolea watu kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Mujikaze sana ili kuanzisha mafunzo ya Biblia munapowahubiria watu kwa mara ya kwanza. Ikiwa mutu amekwisha kupata kitabu hicho na anakataa kujifunza Biblia, muhubiri anaweza kumutolea gazeti fulani la zamani ao broshua yoyote inayozungumuzia mambo yenye kumupendeza. Mwezi wa 7 na wa 8: Tutatolea watu broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32: Je, Kweli Mungu Anatujali?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele? Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, na Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! Unaporudilia mutu, umuonyeshe kitabu Biblia Inafundisha ao ikiwa inafaa, na kulingana na mahitaji yake, umuonyeshe broshua Umusikilize Mungu ao Umusikilize Mungu ili Uishi Milele, na ujaribu kuanzisha funzo la Biblia.
◼ Video Toute la communauté des frères itachunguzwa kwenye Mukutano wa Utumishi wa wakati ujao. Ikiwa unahitaji video hiyo, unaweza kufanya ombi kupitia kutaniko.