Matangazo
◼ Katika Mwezi wa 8: Tutatolea watu broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32: Biblia−Ina Ujumbe Gani?, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, ao Uhai−Ulitokana na Muumbaji? Unapowarudilia watu, uwaonyeshe kitabu Biblia Inafundisha, ao ikiwa inafaa kulingana na mahitaji ya musikilizaji, umuonyeshe broshua Umusikilize Mungu ao Umusikilize Mungu ili Uishi Milele, na jaribu kuanzisha funzo la Biblia. Mwezi wa 9 na wa 10: Tutawatolea watu Munara wa Mulinzi na Amkeni! Unapowarudilia watu, uwaonyeshe kitabu Biblia Inafundisha, ao ikiwa inafaa kulingana na mahitaji ya musikilizaji, umuonyeshe broshua Umusikilize Mungu ao Umusikilize Mungu ili Uishi Milele, na jaribu kuanzisha funzo la Biblia.
◼ Kuanzia mwezi wa 9, mwangalizi wa muzunguko atatoa hotuba yenye kichwa “Kutembea Pamoja na Mungu Kunaleta Baraka Sasa na Hata Milele.”
◼ Mwangalizi wa kikundi cha mahubiri ana daraka la kusaidia kukusanya ripoti za mahubiri za wahubiri na mapainia walio katika kikundi chake cha mahubiri. Wahubiri wanaweza kumusaidia mwangalizi wa kikundi kwa kutoa ripoti zao za mahubiri bila kukawia. Hilo litasaidia Beteli ikusanye kwa wakati ripoti zote za makutaniko mwishoni mwa kila mwezi. Ni lazima kufanya hivyo hasa katika Mwezi wa 7 na wa 8 ili tuwe na ripoti sahihi ya utumishi wa shambani ya mwaka. (Ona Tengenezo sura ya 5 uku. 45).