Matangazo
◼ Mwezi wa 9 na wa 10: Tutawatolea watu Munara wa mulinzi na Amkeni! Unapowarudilia watu, uwaonyeshe kitabu Biblia Inafundisha, ao ikiwa inafaa kulingana na mahitaji ya musikilizaji, umuonyeshe broshua Umusikilize Mungu ao Umusikilize Mungu ili Uishi Milele, na jaribu kuanzisha funzo la Biblia.
◼ Hotuba ya pekee ya watu wote kwa ajili ya kipindi cha Ukumbusho wa mwaka wa 2013 itatolewa juma linaloanza tarehe 1 Mwezi wa 4. Kichwa cha hotuba hiyo kitajulishwa baadaye. Makutaniko yatakayokuwa na ziara ya mwangalizi wa muzunguko ao na mukusanyiko juma hilo yatapanga hotuba ya pekee juma linalofuata. Hakuna kutaniko linaloruhusiwa kutoa hotuba hiyo ya pekee mbele ya tarehe 1 Mwezi wa 4.