Matangazo
◼ Mwezi wa 11 na wa 12: Tutatolea watu broshua Je, Ungependa Kujua Kweli?, Kila Namna ya Kuteseka Itakwisha Karibuni!, Yehova—Yeye Ni Nani?, ao Yesu Kristo—Yeye Ni Nani? Ikiwa mutu anapendezwa, umuonyeshe namna funzo la Biblia linafanywa kwa kutumia kitabu Biblia Inafundisha, ao broshua Umusikilize Mungu ao Umusikilize Mungu ili Uishi Milele. Mwezi wa 1 na wa 2: Tutawatolea watu broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32: Je! Kweli Mungu Anatujali?, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa..., ao Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! Unapowarudilia watu, uwaonyeshe kitabu Biblia Inafundisha, ao ikiwa inafaa, kulingana na mahitaji ya musikilizaji, umuonyeshe broshua Umusikilize Mungu ao Umusikilize Mungu ili Uishi Milele, na jaribu kuanzisha funzo la Biblia.
◼ Siku ya Posho, tarehe 24 Mwezi wa 11, 2012, kwenye Beteli kutakuwa kazi zinazohusu tu wanabeteli. Kwa hiyo, tunawaomba musipange kutembelea Beteli ao kutembelea wanabeteli siku hiyo.
◼ Siku ya Posho tarehe 8 Mwezi wa 12 kutakuwa usafishaji mukubwa wa Beteli. Kwa hiyo, tunawaomba musipange kutembelea Beteli ao kutembelea wanabeteli siku hiyo.
◼ Tafazali, muhakikishe kama andiko mupya la mwaka linaonyeshwa katika Jumba la Ufalme tangu tarehe 1 Mwezi wa 1, mwaka wa 2013. Tunawakumbusha kama si lazima kuandika maneno “Andiko la Mwaka.” Inatosha kuandika tu maneno ya andiko hilo na kitabu cha Biblia ambamo yanatoka kama inavyokubaliwa na Baraza Linaloongoza.