Matangazo
◼ Mwezi wa 12: Tutatolea watu trakte Je, Ungependa Kujua Kweli?, Kila Namna ya Kuteseka Itakwisha Karibuni!, Yehova—Yeye Ni Nani?, ao Yesu Kristo—Yeye Ni Nani? Ikiwa mutu anapendezwa, umuonyeshe namna funzo la Biblia linafanywa kwa kutumia kitabu Biblia Inafundisha, ao broshua Umusikilize Mungu ao Umusikilize Mungu ili Uishi Milele. Mwezi wa 1 na wa 2: Tutawatolea watu broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32: Je! Kweli Mungu Anatujali?, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, ao Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! Unapowarudilia watu, uwaonyeshe kitabu Biblia Inafundisha, ao ikiwa inafaa, kulingana na mahitaji ya musikilizaji, umuonyeshe broshua Umusikilize Mungu ao Umusikilize Mungu ili Uishi Milele, na jaribu kuanzisha funzo la Biblia.
◼ Ukumbusho wa mwaka wa 2014 utafanywa Siku ya Kwanza tarehe 14 Mwezi wa 4.
◼ Wahubiri watakaofanya upainia musaidizi katika Mwezi wa 3, 2013 wataamua ikiwa watahubiri kwa saa 30 ao 50 mwezi huo. Pia, ikiwa mwangalizi wa muzunguko anatembelea kutaniko katika mwezi wa 3, wahubiri wote wanaofanya upainia musaidizi watahuzuria tangu mwanzo mupaka mwisho mukutano ambao mwangalizi wa muzunguko atafanya pamoja na mapainia wa kawaida.
◼ Ikiwa katika eneo lenu watu hawatumie sana Internete, muzee mwenye uzoefu anaweza kutoa habari yenye kichwa Jinsi ya Kufanya Utafiti, iliyo katika kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, ukurasa wa 33 mupaka 38. Ikiwezekana katika luga yenu, mufanye maonyesho mawili. Kwanza, munapozungumuzia kichwa kidogo Kutumia Biblia, Kitabu Chetu Kikuu cha Utafiti, mufanye onyesho kuhusu familia inayotumia marejeo (références marginales) yaliyo katika Biblia ili kupata habari zaidi kuhusu andiko moja la Biblia ao maandiko mawili. Kisha, munapozungumuzia kichwa kidogo Kujifunza Kutumia Vifaa Vingine vya Utafiti, mufanye onyesho kuhusu familia inayotumia fahirisi ya maandiko (Index biblique) ya kitabu Index des publications Watch Tower ili kupata vichapo vinavyotoa maelezo kuhusu andiko fulani wanalochunguza katika ibada ya familia.