Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 12/12 uku. 7
  • Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 12/12 uku. 7

Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi

Maulizo yanayofuata yatatumiwa kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi katika juma tokea tarehe 31 Mwezi wa 12, 2012. Tarehe ambayo kila jambo litazungumuziwa inaonyeshwa pia ili kusaidia watu kutafuta majibu katika vitabu wanapotayarisha masomo ya huduma ya kila juma.

1. Unabii ulio katika andiko la Yoeli 2:1-10, 28 kuhusu shambulio la wadudu umetimizwa kwa njia gani? [Juma tokea tarehe 5 Mwezi wa 11, w07 1/10 uku. 13 fu. 1]

2. Andiko la Amosi 8:11 linatimizwa kwa nani, na ni ulizo gani tunalopaswa kujiuliza kwa kuwa tuna chakula kingi cha kiroho? [Juma tokea tarehe 12 Mwezi wa 11, jd uku. 60-61 fu. 9]

3. Ni nini kilichowafanya Waedomu wawe na kiburi cha moyo, na kwa kweli ni jambo gani ambalo hatupaswe kusahau? (Oba. 3, 4) [Juma tokea tarehe 19 Mwezi wa 11, w07 1/11 uku. 13 fu. 6]

4. Ni katika njia gani Yehova alijuta juu ya musiba ambao alisema ataleta juu ya watu wa Ninawi? (Yona 3:8, 10) [Juma tokea tarehe 19 Mwezi wa 11, w07 1/11 uku. 14 fu. 13]

5. Namna gani kutembea katika jina la Mungu kunatia nguvu uhusiano wetu pamoja naye? (Mika 4:5) [Juma tokea tarehe 26 Mwezi wa 11, jd uku. 88 fu. 12]

6. Kutimizwa kwa unabii unaopatikana katika andiko la Nahumu 2:6-10 kunatutolea uhakikisho gani? [Juma tokea tarehe 3 Mwezi wa 12, w07 15/11 uku. 9 fu. 2; w88-F 15/2 uku. 28 fu. 7]

7. Andiko la Hagai 1:6 linamaanisha nini, na tunajifunza jambo gani ambalo tunapaswa kuchukua kwa uzito? [Juma tokea tarehe 10 Mwezi wa 12, w06 15/4 uku. 22 fu. 12-15]

8. Namna gani tunaweza kutumikisha shauri lenye kufaa lililo katika andiko la Zekaria 7:10 linalosema kwamba ‘tusipangiane jambo lolote baya’ mioyoni mwetu? [Juma tokea tarehe 17 Mwezi wa 12, jd uku. 113 fu. 6; w07 1/12 uku. 11 fu. 2]

9. Sababu gani maneno yaliyo katika andiko la Zekaria 4:6, 7 yanafariji waabudu wa Yehova leo? [Juma tokea tarehe 17 Mwezi wa 12, w07 1/12 uku. 10 fu. 7]

10. Tunapofikiria mawazo yaliyo katika andiko la Malaki 3:16, sababu gani hatupaswe hata kidogo kuregeza azimio letu la kulinda uaminifu wetu kwa Mungu? [Juma tokea tarehe 31 Mwezi wa 12, w07 15/12 uku. 29 fu. 3]

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine