Programu ya Juma Tokea Tarehe 11 mwezi wa 3
JUMA TOKEA TAREHE 11 MWEZI WA 3
Wimbo 68 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jr sura ya 6 fu. 13-18, kisanduku kwenye uku. 74 (Dak. 30)
□ Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi:
Usomaji wa Biblia: Marko 13-16 (Dak. 10)
Na. 1: Marko 14:22-42 (Isipite dak. 4)
Na. 2: Ukumbusho una Maana Gani?—rs uku. 336 fu. 6–uku. 337 fu. 2 (Dak. 5)
Na. 3: Mukate na Divai Vinavyotumiwa Kwenye Ukumbusho Vinamaanisha Nini?—rs uku. 337 fu. 3–uku. 338 fu. 1 (Dak. 5)
□ Mukutano wa Utumishi:
Wimbo 109
Dak. 10: Maandiko Yanayofuata Yanatufundisha Nini? Mazungumuzo. Musome Mathayo 10:7-10 na Luka 10:1-4. Muzungumuzie namna habari hizo zinavyoweza kutusaidia katika mahubiri.
Dak. 10: Njia za Kupanua Utumishi Wako—Sehemu ya 1. Mazungumuzo yanayotegemea kitabu Tengenezo, ukurasa wa 111, fungu la 1, mupaka ukurasa wa 112, fungu la 2. Uulize maulizo muhubiri mumoja ao wawili ambao wamehamia katika eneo lingine ao ambao wamejifunza luga nyingine ili kupanua utumishi wao. Walikutana na matatizo gani na walifanya nini ili kupambana nayo? Namna gani familia yao ao ndugu na dada wa kutaniko waliwasaidia? Walipata baraka gani?
Dak. 10: “Tujitayarishe kwa Furaha kwa Ajili ya Ukumbusho.” Maulizo na majibu. Zungumuzia mipango ya kutaniko lenu kwa ajili ya Ukumbusho na toa maelezo kuhusu namna kampanye ya kuwaalika watu kwenye Ukumbusho inavyoendelea.
Wimbo 8 na Sala