Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Trakte Habari ya Ufalme Na. 38
“Ulimwenguni pote tunawatolea watu trakte hii iliyo na ujumbe wa maana. Chukua yako.”
Tangazo: Ili kutolea watu wa eneo trakte hiyo, ni vizuri tuseme maneno machache. Hata hivyo, wakati fulani, musikilizaji anaweza kupendezwa kabisa na ujumbe na kutaka mazungumuzo yaendelee. Ikiwa ni hivyo, unaweza kumuuliza maoni yake kuhusu ulizo lililo kwenye ukurasa wa kwanza wa trakte, kisha unaweza kumusomea jibu la Biblia lililo ndani na kuzungumuzia habari moja kati ya habari zilizo katika trakte ikiwa wakati unaruhusu. Mbele ya kuachana naye, umuonyeshe ulizo lililo chini ya sehemu “Pengine Unajiuliza,” na ufanye mipango ya kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo hilo.
Munara wa Mulinzi 01/11/13
“Kwa maoni yako, watu wamesema uongo mukubwa gani kumuhusu Mungu? [Acha mutu ajibu.] Kulingana na Biblia, Mungu anataka watu wamupende na kumutumainia. [Soma Isaya 41:13.] Gazeti hili linafunua mambo matatu ya uongo yanayosemwa kumuhusu Mungu ambayo yamefanya iwe vigumu kwa watu kumukaribia.”
Amuka! Mwezi wa 11
“Tunawatembelea watu ili kuzungumuza nao kwa muda mufupi kuhusu kanuni za mwenendo safi. Watu wengi wanaogopa kwamba kanuni hizo haziheshimiwe tena. Unawaza kwamba watu wamepuuza kanuni za jamii za mwenendo safi? [Acha mutu ajibu.] Biblia ilitabiri kwamba katika siku za mwisho watu watakuwa na mwenendo na tabia mbaya. [Soma 2 Timotheo 3:1-5.] Gazeti hili linaeleza sababu gani tunaweza kutegemea kanuni za mwenendo safi zinazopatikana katika Biblia.”