Utoaji Mbalimbali
Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 10
“Katika siku hizi ngumu, sisi wote tunapatwa na matatizo yanayoleta mikazo katika familia. Unafikiri tunaweza kupata wapi mashauri yenye kutegemeka ili kutusaidia tufanye maisha ya familia yawe yenye furaha?” Acha mutu ajibu. Kisha umuonyeshe Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1 mwezi wa 10, na muzungumuzie habari ya kichwa kidogo kimoja kati ya vichwa vidogo vilivyo kwenye ukurasa wa 16 na 17 na andiko moja hivi kati ya maandiko yanayoonyeshwa. Umutolee mutu gazeti, na ufanye mupango wa kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo moja kati ya maulizo mengine.
Mnara wa Mlinzi 01/10/11
Umuonyeshe mutu jalada la gazeti, kisha umuulize, “Unaweza kujisikia namna gani ikiwa unajua kwamba umefundishwa mambo ya uongo kumuhusu Mungu? [Acha mutu ajibu.] Ona yale Yesu alisema kuhusu jinsi ya kutofautisha mafundisho ya kweli na ya uongo. [Soma Yohana 17:17.] Kwa hiyo, Biblia pekee ndiyo inayotufundisha kweli kumuhusu Mungu. Gazeti hili linazungumuzia mafundisho tano ya uongo ambayo watu wamefundishwa kumuhusu Mungu na kisha utaona yale ambayo Biblia inafundisha.”
Amkeni! Mwezi wa 10
“Leo, tunatembelea watu wote na tuna habari inayoweza kufaidi familia. Unafikiri ni tatizo gani kubwa zaidi ambalo wazazi wanapambana nalo leo katika kulea watoto? [Acha mutu ajibu.] Wazazi wengi wanategemea Biblia ili kupata mashauri. Kwa mufano, maneno haya yanawasaidia sana wanapowaadibisha watoto wao. [Soma Waefeso 4:31.] Gazeti hili linaonyesha jinsi mashauri ya Biblia yanavyoweza kuwasaidia wazazi kuwalea vizuri watoto wao tangu utoto mupaka wanapokuwa vijana.”