Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza ya Mwezi wa 10
“Tunawatembelea watu ili kuzungumuza nao kwa dakika chache kuhusu Guvernema nzuri. Unawaza kwamba kuna guvernema ambayo inaweza kumaliza matatizo makubwa kama vile kutendea watu kwa ukali ao kuwaua na ukosefu wa haki?” Acha mutu ajibu. Mukumbushe musikilizaji kwamba katika Sala ya Baba yetu, Yesu aliwafundisha wafuasi wake wasali ili guvernema hiyo, ni kusema Ufalme wa Mungu, ukuje. Muonyeshe ukurasa wa mwishowa Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 10, na muzungumuzie habari iliyo chini ya ulizo la kwanza na hata andiko moja. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili muzungumuzie ulizo linalofuata.
Munara wa Mulinzi 01/10
“Tunazungumuza na watu kwa dakika chache kuhusu maneno haya ya sala inayojulikana sana ambayo Yesu aliwafundisha wanafunzi wake. [Soma Matayo 6:9, 10.] Unajua Ufalme wa Mungu ni nini, na sababu gani Yesu alizungumuzia sana Ufalme huo katika mafundisho yake? [Acha mutu ajibu.] Gazeti hili linaonyesha mambo ambayo Biblia inasema kuhusu Ufalme wa Mungu na pia kuhusu baraka nyingi nzuri ambazo Ufalme huo utaleta katika dunia.”
Amuka! Mwezi wa 10
“Tunawatembelea watu kwa dakika chache tu ili kuwasaidia wapate jibu la ulizo hili. [Onyesha ukurasa wa kwanza wa gazeti] Unafikiri kwamba ili mutu afanikiwe kabisa katika maisha ni lazima tu akuwe tajiri? [Acha mutu ajibu.] Ona mambo ambayo Biblia inasema juu ya vitu vya kimwili. [Soma Luka 12:15.] Kulingana na Biblia, kila mutu anaweza kupata mafanikio ya kweli. Gazeti hili linaeleza namna gani hilo linawezekana.”