Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza ya Mwezi wa 10
“Tunawatembelea majirani wetu kwa muda mufupi. Kati ya wale ambao tumezungumuza nao, wengi wanasema kwamba hali ngumu zaidi ambayo wamepambana nayo maishani ni kifo cha mutu ambaye walimupenda. Wewe pia unaweza kusema hivyo? [Acha mutu ajibu.] Kuna habari yenye kutia moyo ambayo nilipenda kukuonyeshe.” Umuonyeshe ukurasa wa mwisho wa Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 10, na muzungumuzie habari iliyo chini ya ulizo la kwanza na hata andiko moja. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo linalofuata.
Munara wa Mulinzi 01/10/13
“Tunawatembelea watu kwa muda mufupi ili kuwatia moyo wasome Biblia. Tunajua kwamba watu fulani wanapendezwa na Biblia; lakini wengine hawapendezwe nayo. Wewe pia unapendezwa na Biblia ao hapana? [Acha mutu ajibu.] Biblia inasema jambo hili la maana. [Soma 1 Wathesalonike 2:13.] Niko hakika utakubaliana nami kwamba ikiwa Biblia ni kitabu cha Mungu, basi ni lazima tuisome. Gazeti hili linazungumuzia kwa kifupi habari zilizo katika Biblia na sababu gani tunapaswa kupendezwa nayo.”
Amuka! Mwezi wa 10
“Ningetaka kujua maoni yako juu ya ulizo hili: Je, mutu anaweza kutosheka maishani hata ikiwa hana vitu vingi vya kimwili? [Acha mutu ajibu.] Ona yale ambayo Biblia inasema. [Soma 1 Timotheo 6:8.] Gazeti hili linaonyesha namna tunavyoweza kuwa na maoni yenye kusawazika juu ya vitu vya kimwili na linazungumuzia mambo matatu ya lazima ambayo feza haziwezi kununua.”