Njia Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 4
“Ubatizo unafanywa na Wakristo wengi. Unawaza ubatizo ni wa lazima? [Acha mutu ajibu.] Habari hii inaeleza mambo fulani yenye kupendeza.” Umuonyeshe musikilizaji wako Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1 mwezi wa 4, na muzungumuzie habari iliyo chini ya kichwa kidogo kwenye ukurasa wa 16 na umusomee hata andiko moja kati ya maandiko yanayoonyeshwa. Umutolee mutu magazeti na ufanye mupango wa kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo linalofuata.
Mnara wa Mlinzi 01/04/12
“Watu wana mawazo mengi juu ya Yesu. Wamoja wanawaza Yesu alikuwa Masiya aliyeahidiwa. Wengine wanawaza alikuwa tu mutu muzuri. Na wengine wanawaza Yesu hakuwahi kuishi. Wewe unawaza namna gani? [Acha mutu ajibu.] Biblia inasema kama ni jambo la lazima kujua ukweli juu ya Yesu. [Soma Yohana 17:3.] Gazeti hili linaonyesha majibu ya Biblia kwa maulizo fulani ambayo watu wanauliza sana juu ya Yesu.”
Amkeni! Mwezi wa 4
“Tunatembelea watu na tuna habari inayoweza kusaidia familia. Leo, familia zinapatwa na matatizo mengi, sivyo? [Acha mutu ajibu.] Tazama mahali ambapo familia nyingi zimepata mashauri yaliyowasaidia. [Soma Zaburi 119:105.] Gazeti hili linazungumuzia familia ambazo baba na mama wameoana kila mumoja anakuja na watoto wake aliozaa na mume ao na muke mwingine, na hata hivyo familia hizo zimeweza kutatua matatizo yao kwa kufuata kanuni za Biblia.”