Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/03/11
“Watu wana mawazo yenye kupingana kuhusu Yesu. Wamoja wanasema kwamba Yesu ni mwana wa Mungu, wengine wanasema kwamba yeye ni mutu muzuri tu, wewe unafikiri nini?” Acha mutu ajibu. Kisha msome pamoja habari iliyo chini ya ulizo moja lenye maandiko mazito meusi kwenye ukurasa wa 16-17 na andiko moja kati ya maandiko yanayotajwa. Tolea mutu gazeti, na ufanye mipango ya kurudi ili kuchunguza jibu la ulizo linalofuata.
Amkeni! Mwezi wa 3
Unapokutana na kijana, onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 26. Onyesha kichwa kidogo cha kwanza na uulize, “Kulingana na wewe, maneno yanayoandikwa hapa ni ya kweli ao ya uongo? [Acha mutu ajibu. Kisha soma 2 Wakorintho 7:1.] Habari hii inazungumzia yale unayohitaji kujua kuhusu kuvuta tumbako, pia jinsi mutu anavyoweza kuachana na tabia hiyo.”
Mnara wa Mlinzi 01/04/11
“Watu wengi wanashikilia mafundisho yenye kutofautiana kuhusu Yesu. Unafikiri kwamba ni jambo la maana kujua ukweli kuhusu Yesu? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Yohana 17:3.] Gazeti hili linaeleza yale Biblia inasema kuhusu Yesu—alitoka wapi, yale aliyotimiza katika maisha yake, na kwa nini alikufa.”
Amkeni! Mwezi wa 4
“Je, unakubali kwamba kufiwa na mutu tunayemupenda ni moja kati ya hali mbaya sana ambazo zinampata mutu katika maisha? [Acha mutu ajibu.] Wengi waliofiwa walisaidiwa na shauri hili. [Soma Zaburi 55:22.] Gazeti hili linazungumzia njia fulani zinazofaa za kupambana na huzuni, kutia ndani jinsi ya kumutupia Mungu muzigo wetu.”