Utoaji Mbalimbali
Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 5
“Je, umekwisha kujiuliza kwa nini Mungu anaruhusu uovu na kuteseka? [Acha mutu ajibu.] Nilipenda kukuonyesha jambo fulani lenye kupendeza kuhusu ulizo hilo.” Musome pamoja habari iliyo chini ya kichwa kidogo kwenye ukurasa wa 16 wa Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1 mwezi wa 5 na andiko moja kati ya maandiko yaliyo katika habari hiyo. Umtolee gazeti na upange kumrudilia ili kujibu ulizo linalofuata.
Mnara wa Mlinzi 01/05/11
Soma Zaburi 37:10, 11. Kisha sema: “Je, unafikiri kwamba tutaona utimizo wa ahadi hii hivi karibuni? [Acha mutu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia mambo sita yaliyotabiriwa katika Biblia ambayo tunaona utimizo wake leo na ambayo yanaonyesha kweli kwamba ahadi hiyo itatimia karibuni.”
Amkeni! Mwezi wa 5
“Watu fulani wanasema kwamba wanadamu ni wanyama waliogeuka-geuka mpaka wakawa wanadamu. Wewe unawaza nini? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Zaburi 139:14.] Kwa kweli, mtunga-zaburi hakuwa na ujuzi mwingi kuhusu mwili wa mwanadamu kama leo. Gazeti hili linazungumzia mambo tunayojua sasa, na pia yale yanayotufanya tuwe tofauti na wanyama.”