Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 7
“Katika miaka ya karibuni, watu wamezungumuzia sana kuhusu malaika. Je, unawaza kama malaika wako kabisa? [Acha mutu ajibu.] Ona yale ambayo gazeti hili linasema.” Umupatie musikilizaji Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 mwezi wa 7, na muchunguze pamoja habari iliyo chini ya kichwa kidogo cha kwanza kwenye ukurasa wa 16 na andiko moja kati ya maandiko yaliyo hapo. Umutolee gazeti, na upange kurudia ili muzungumuzie ulizo linalofuata.
Mnara wa Mlinzi 07/01/12
Soma Zaburi 65:2. Kisha sema: “Watu wengi wanakubaliana na jambo hilo, wanakubali kama Mungu ni ‘Musikiaji wa sala,’ na wanasali kila siku. Lakini wengine wanajiuliza, ‘Ikiwa Mungu iko, sababu gani ulimwengu unajaa matatizo mengi?’ Unafikiri nini? Je, kuna Mungu anayesikia sala zetu? [Acha mutu ajibu.] Gazeti hili linazungumuzia maoni ya Biblia kuhusu ulizo hili: ‘Sababu gani Musikiaji wa sala anawaacha watu wateseke?’”
Amkeni! Mwezi wa 7
“Ikiwa ungekuwa na uwezo wa kubadilisha mambo, ni jambo gani kuhusu ulimwengu wetu wewe ungebadilisha? [Acha mutu ajibu.] Biblia inaonyesha sababu gani wanadamu wana mipaka kuhusu mambo wanayoweza kufanya. [Soma Yeremia 10:23.] Gazeti hili linaonyesha mambo ambayo Mungu anakusudia kubadilisha.”