Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 6/13 uku. 4
  • Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Utoaji Mbalimbali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Namna Mbalimbali ya Kuanzisha Mazungumuzo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2013
km 6/13 uku. 4

Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo

Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza ya Mwezi wa 7

“Kwa kawaida kila mutu anapenda kuishi maisha marefu na yenye furaha. Kwa hiyo, tungependa kujua maoni yako juu ya ulizo hili: Unawaza kama siku fulani ufundi wa wanadamu katika mambo ya sayansi na ya kiganga utatusaidia tuishi milele? [Acha mutu ajibu.] Ona yale ambayo gazeti hili linasema.” Umuonyeshe ukurasa wa mwisho wa Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 7, na muzungumuzie habari iliyo chini ya ulizo la kwanza na hata andiko moja iliyo hapo. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo linalofuata.

Tangazo: Kwenye mukutano kwa ajili ya mahubiri wa tarehe 6 Mwezi wa 7, mutafanya onyesho mukitumia pendekezo lililo hapa juu.

Munara wa Mulinzi 01/07/13

“Watu wengi tunaozungumuza nao wana dini yao. Lakini wengine wanasema kwamba hawatumainie hata dini moja. Wewe unawaza nini kuhusu dini? [Acha mutu ajibu.] Yesu alitutolea kanuni fulani ili kutusaidia kujua ikiwa dini fulani ni ya kweli ao ya uongo. [Soma Luka 6:44a.] Gazeti hili linazungumuzia matunda fulani mabaya ambayo dini imetokeza. Linajibu pia ulizo hili, Je, kuna dini fulani tunayoweza kutumainia?”

Amuka! Mwezi wa 7

“Tunawatembelea majirani ili kuzungumuzia tatizo linalohangaisha watu. Tatizo hilo ni ukosefu wa haki. Watu fulani wanapiganisha ukosefu wa haki kwa kufanya maandamano ya kuupinga. Unawaza watu wanaofanya hivyo wanafikia kubadilisha mambo? [Acha mutu ajibu.] Ona jambo ambalo, kulingana na Biblia, litabadilisha kabisa mambo duniani. [Soma Mathayo 6:9, 10.] Gazeti hili linajibu ulizo, je, kufanya maandamano ya kupinga ndiko kutamaliza tatizo la ukosefu wa haki?”

Habari Njema Inayotoka kwa Mungu!

“Tunatembelea familia yenu ili kuzungumuzia wazo moja la Biblia lenye kutia moyo. Watu wengi ambao tumeongea nao wanajiuliza sababu gani Mungu mwenye upendo anaruhusu mateso mengi duniani. Unawaza kwamba Mungu alipoumba alikusudia mateso duniani?” Acha mutu ajibu. Kisha fungua somo la 5, na musome na kuzungumuzia fungu mbili za kwanza na maandiko yenye neno “soma.” Umutolee broshua, na upange kumurudilia ili muzungumuzie ulizo linalofuata lililo katika maandishi meusi mazito.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine