Utoaji Mbalimbali
Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 7
“Wengi wamerudilia-rudilia maneno haya yaliyo katika Sala ya Bwana: ‘Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.’ Unafikiri Ufalme huo ni nini? [Acha mutu ajibu.] Andiko hili la Biblia linatupatia jibu.” Soma Danieli 2:44. Kisha umuonyeshe mutu Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1 mwezi wa 7 na usome na kuzungumzia habari iliyo chini ya kichwa kidogo cha kwanza kwenye ukurasa wa 16. Umtolee mutu gazeti na ufanye mpango wa kumrudilia ili kujibu ulizo linalofuata.
Mnara wa Mlinzi 01/07/11
“Kwa kuwa maisha ni mafupi na ni yenye kujaa na matatizo, watu wengi wanajiuliza kusudi la maisha ni nini. Je, umekwisha kufikiria jambo hilo? [Acha mutu ajibu.] Biblia inaahidi kwamba maisha hayataendelea kuwa mafupi ao yenye kujaa na matatizo. [Soma Ufunuo 21:4.] Gazeti hili linazungumzia kusudi la Mungu kwa dunia na linaonyesha mambo fulani tunayoweza kufanya ili tuwe na kusudi maishani hata sasa.”
Amkeni! Mwezi wa 7
Taja tukio fulani lenye kuhuzunisha linalozungumziwa katika eneo lenu. Kisha useme hivi: “Unafikiri ni kwa nini Mungu anaruhusu mambo kama hayo yatendeke? [Acha mutu ajibu.] Kulingana na Biblia, Mungu anasikilia watu wanaoteseka huruma. [Soma Kutoka 3:7.] Pia Biblia inatuonyesha kwa nini Mungu anaruhusu watu wateseke na inaonyesha kwamba hivi karibuni atamaliza mateso milele. Gazeti hili linaeleza mambo hayo.”