Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/02/10
“Karibu kila mutu ana dini yake. Je, unafikiri Mungu anakubali tumwabudu kupitia dini yoyote? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Mathayo 15:9.] Habari hii inazungumzia mambo mane ambayo Yesu alionyesha yanayotambulisha dini ya kweli.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 16.
Amkeni! Mwezi wa 2
“Watu fulani wanaamini kwamba kuna Muumba, lakini wengine wanafikiri kwamba jambo hilo halipatani na sayansi na si sawa. Wewe unafikiri namna gani? [Acha mutu ajibu.] Kulingana na Biblia, imani ya kweli inategemea mambo yaliyo wazi. [Soma Waebrania 11:1.] Gazeti hili linazungumzia mambo fulani yanayohakikisha kwamba kuna Muumba.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 22.
Mnara wa Mlinzi 01/03/10
“Je, unaiona Biblia kuwa Neno la Mungu ao kuwa kitabu kizuri tu? [Acha mutu ajibu.] Ona yale ambayo Biblia yenyewe inasema. [Soma 2 Timotheo 3:16, 17.] Gazeti hili linazungumzia namna ya kufanya uamuzi mzuri kuhusu jambo hilo na kwa nini ni jambo la maana kufanya hivyo.”
Amkeni! Mwezi wa 3
“Kama vile watu wengi, labda unafurahia uzuri wa vitu vinavyotuzunguka. Je, unakubali kwamba vitu vinavyotuzunguka vinaonyesha pia kwamba kuna Muumba mwenye hekima? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Zaburi 104:24.] Gazeti hili lina mifano ya vitu fulani vyenye kupendeza vinavyotuzunguka na linazungumzia kile ambacho vitu hivyo vinatufundisha.”