Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/05/10
“Unafikiri ulimwengu ungekuwa namna gani ikiwa kila mutu angefuata maneno haya ya Yesu? [Soma Mathayo 7:12. Kisha acha mutu ajibu.] Habari hii inazungumzia mafundisho fulani ya Yesu ili kuonyesha kabisa maana ya kuwa Mkristo.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 16.
Amkeni! Mwezi wa 5
“Je, unafikiri kwamba matatizo ya kupata feza tuliyo nayo sasa yatakwisha karibuni? [Acha mutu ajibu.] Watu wengi hawajui jinsi Biblia inavyoweza kutusaidia katika nyakati zilizo ngumu kama hizi. [Soma andiko moja kati ya maandiko yaliyo katika habari.] Habari hii inaonyesha jinsi mashauri ya Biblia yanavyoweza kutusaidia tunapopambana na matatizo ya kupata feza.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 18.
Mnara wa Mlinzi 01/06/10
“Tofauti na miaka iliyopita, kanisa nyingi leo hazizungumzii zambi. Je, unafikiri zambi ni jambo la zamani, ao ni jambo tunalopaswa kuhangaikia? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Waroma 5:12.] Gazeti hili linazungumzia yale ambayo Biblia inasema kuhusu zambi.”
Amkeni! Mwezi wa 6
“Inaonekana kwamba mahangaiko ya maisha yanaendelea kuongezeka. Je, wewe pia unaona hivyo? [Acha mutu ajibu.] Watu wengi wanafikiri kwamba maneno haya yanaeleza sababu moja inayofanya kuwe na mahangaiko mengi. [Soma 2 Timotheo 3:1.] Gazeti hili linazungumzia matokeo mabaya yanayotokana na mahangaiko. Linatoa pia mapendekezo fulani kuhusu jinsi tunavyoweza kuepuka kuwa na mahangaiko zaidi .”