Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/11/09
“Inaonekana kwamba familia zinaendelea kupatwa na mikazo. Unafikiri familia zinaweza kufaidika namna gani ikiwa watu wa familia wanajikaza kuwa na maoni kama ya Yesu? [Soma Mathayo 20:28. Kisha acha mutu ajibu.] Habari hii inazungumzia mambo 5 ambayo watu wa familia mbalimbali wanaweza kujifunza kutokana na mfano wa Yesu.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 16.
Amkeni! Mwezi wa 11
“Je, unaona kwamba dini inawachochea watu kuwa na upendo na amani ao inawachochea wachukiane na kutendeana kwa jeuri? [Acha mutu ajibu.] Inaonekana kwamba watu wengi hawatii maneno haya ya Yesu. [Soma Mathayo 5:44, 45.] Habari hii inajibu ulizo, Je, inawezekana mutu awapende maadui wake?” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi 01/12/09
“Je, unafikiri kwamba siku fulani Mungu atamaliza mateso duniani? [Acha mutu ajibu.] Ona ahadi hii ya Biblia inayotutolea sababu ya kuwa na tumaini. [Soma andiko moja kati ya maandiko yaliyo katika kisanduku kwenye ukurasa wa 7.] Gazeti hili linaonyesha maoni ya Biblia kuhusu jinsi gani na wakati gani Mungu atamaliza mateso yote.”
Amkeni! Mwezi wa 12
“Watu fulani wanaamini kwamba ulimwengu uliumbwa, wengine wanafikiri kwamba ulijitokeza wenyewe na hauna kusudi lolote. Wewe unafikiri nini? [Acha mutu ajibu.] Ona jinsi Biblia inavyosema. [Soma Waebrania 3:4.] Gazeti hili linatoa maelezo yanayofaa kuhusu jinsi ulimwengu ulivyoanza na kusudi lake.”