Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/12/09
“Wakati huu wa mwaka, watu wengi wanachora ao kutengeneza vifaa vya michezo kuhusu kuzaliwa kwa Yesu ili kuonyesha jinsi habari hii ya Biblia ilivyotendeka. [Soma Mathayo 2:1, 11.] Je, umeona tofauti kati ya yale Biblia inasema yalitendeka na yale ambayo watu wanaonyesha mara nyingi? [Acha mutu ajibu.] Habari hii inazungumzia mambo yaliyotendeka kabisa.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 31.
Amkeni Mwezi wa 12
“Ningependa kujua maoni yako kuhusu jambo fulani ambalo Yesu alisema. [Soma Mathayo 5:3.] Kwa kuwa kuna dini nyingi, je, unafikiri kwamba tunaweza kuchagua dini yoyote ili kutosheleza mahitaji yetu ya kiroho? [Acha mutu ajibu.] Habari hii inaonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusu jinsi ya kutosheleza kabisa mahitaji yetu ya kiroho.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 12.
Mnara wa Mlinzi 01/01/10
“Dini zina maoni tofauti kuhusu kunywa pombe. Unafikiri Mungu anamwona namna gani mutu anayekunywa pombe? [Acha mutu ajibu.] Ijapokuwa Biblia inaonyesha kwamba Yesu aligeuza maji kuwa divai, inasema pia hivi. [Soma Methali 23:20a.] Gazeti hili linaonyesha maoni yenye kusawazika ya Biblia.”
Amkeni! Mwezi wa 1
“Katika nyakati hizi ngumu, watu wanalemewa na kazi nyingi na wanajisikia wenye kuchoshwa sana. Je, wewe pia umekwisha kujisikia hivyo? [Acha mutu ajibu.] Ona shauri hili lenye kufaa. [Soma Mhubiri 4:6.] Gazeti hili linazungumzia jinsi tunavyoweza kuwa na usawaziko kati ya kazi, madaraka ya familia, na mambo ya kujifurahisha. Linatoa pia mapendekezo kwa ajili ya wale wanaotafuta kazi.”