Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/04/09
“Watu fulani wanaamini kwamba Mungu amekwisha kupanga mambo yote, wengine wanafikiri kwamba tunajichagulia wenyewe. Unafikiri nini? [Acha mutu ajibu.] Ona maelezo haya kupendeza. [Soma Mhubiri 9:11.] Habari hii inazungumzia jibu la Biblia kuhusu ulizo, ‘Je, Mungu amekwisha kupanga kila jambo’” Onyesha habari iliyo kwenye ukurasa wa 26.
Amkeni! Mwezi wa 4
“Ndoa nyingi zinavunjwa kwa sababu ya uzinifu. Je, unafikiri kwamba kutii shauri la andiko hili kunaweza kusaidia ndoa zisivunjike? [Soma Mathayo 5:28. Kisha acha mutu ajibu.] Habari hii inatumia Biblia ili kusaidia watu waliooana waepuke mtego wa kukosa uaminifu katika ndoa.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 28.
Mnara wa Mlinzi 01/05/09
“Unafikiri ni nini kinachoweza kufanya mutu aone kuwa vigumu kumwamini Mungu? [Acha mutu ajibu.] Kulingana na andiko hili, imani ni ya maana. [Soma Waebrania 11:6.] Gazeti hili linazungumzia hatua ine tunazoweza kuchukua ili kutia nguvu imani yetu.”
Amkeni! Mwezi wa 5
“Leo, watu wengi zaidi wanatumia vibaya dawa walizoandikiwa na mganga. Unafikiri ni kwa sababu gani? [Acha mutu ajibu.] Biblia inataja sababu moja kubwa, zaidi sana kuhusu watoto. [Soma Methali 13:20.] Gazeti hili linazungumzia jinsi unavyoweza kujilinda na hatari hiyo, wewe mwenyewe na familia yako.”