Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/01/09
“Kwa kuwa watu wanaharibu hewa, maji, na misitu, je, unafikiri kwamba Mungu hatafanya jambo lolote? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Ufunuo 11:18.] Habari hii inatoa sababu zilizo katika Biblia zinazotupatia tumaini kuhusu wakati ujao wa dunia.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 18.
Amkeni! Mwezi wa 1
“Watu wengi wanapopatwa na magumu, wanafikiri kwamba ni malipizi kutoka kwa Mungu. Je, umekwisha kufikiri hivyo? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Yakobo 1:13.] Habari hii inaeleza chanzo cha magumu yetu, na kwa nini tunaweza kuwa hakika kwamba magumu tunayopata yatakwisha karibuni.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 28.
Mnara wa Mlinzi 01/02/09
“Je, unafikiri kwamba dini zote zinakubaliwa na Mungu? [Acha mutu ajibu.] Ona wazo la Yesu katika andiko hili. [Soma Mathayo 15:8, 9.] Habari hii inaonyesha ikiwa Mungu anakubali dini zote ao hapana.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 9.
Amkeni! Mwezi wa 2
“Vitu vyote vinavyotuzunguka vinaonyesha kwamba dunia ilifanywa ili iwezekane mutu aishi duniani. Je, unafikiri kwamba vitu vilijitokeza ao viliumbwa? [Acha mutu ajibu.] Watu wengi wanakubaliana na mawazo yaliyo katika andiko hili. [Soma Zaburi 104:24.] Gazeti hili linazungumzia uhakikisho wa sayansi na wa Biblia kwamba kuna Muumbaji.”