Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/02/09
“Je, unafikiri kwamba Mungu anasikiliza sala zote? [Acha mutu ajibu.] Ona yale ambayo Yesu alisema kuhusu jambo hilo. [Soma Mathayo 6:7.] Habari hii yenye kupendeza inatoa majibu ya Biblia kwa maulizo mane ambayo watu wanauliza mara nyingi.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 16.
Amkeni! Mwezi wa 2
“Watu wengi wanaamini kwamba kila jambo linalotupata maishani limekwisha kupangwa na Mungu. Unafikiri namna gani? [Acha mutu ajibu.] Kulingana na andiko hili tunaweza kuchukua uamuzi. [Soma Kumbukumbu la Torati 30:19.] Habari hii inatoa maelezo kuhusu yale Biblia inasema kuhusiana na fundisho la kwamba Mungu amekwisha kupanga kila jambo linalotupata maishani.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 12.
Mnara wa Mlinzi 01/03/09
“Je, unafikiri kwamba kila jambo linalotupata maishani limekwisha kupangwa na Mungu? [Acha mutu ajibu.] Ona yale ambayo Biblia inasema kuhusu jambo hilo. [Soma Mhubiri 9:11.] Gazeti hili linaeleza kwamba, ijapokuwa Mungu amepanga wakati mzuri ajabu kwa ajili ya dunia, anaruhusu kila mmoja wetu achague njia atakayoifuata maishani.”
Amkeni! Mwezi wa 3
“Watu wengi leo wanateseka kwa sababu ya kukosa feza, zaidi sana wakati huu ambapo mambo ya uchumi (économie) yanaharibika. Je, unakubaliana na jambo hilo? [Acha mutu ajibu.] Ona shauri hili lenye kufaa. [Soma 1 Timotheo 6:8, 10.] Gazeti hili linazungumzia kanuni fulani za Biblia zinazotusaidia kutumia feza zetu kwa hekima ili tupate amani ya akilini.”