Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/04/10
“Waandishi fulani wanasema kwamba Yesu hakukufa kama Biblia inavyosema, lakini alioa na kuzaa watoto. Je, umekwisha kusikia hivyo? [Acha mutu ajibu.] Ni jambo la maana kujua kweli. [Soma Yohana 17:3.] Habari hii inatoa sababu za kuamini yale ambayo Biblia inasema kumhusu Yesu.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 26.
Amkeni! Mwezi wa 4
Soma Zaburi 37:9-11. Kisha uliza: “Wewe unafikiri ulimwengu utakuwa namna gani wakati mambo haya yatatimia? [Acha mutu ajibu.] Habari hii inazungumzia unabii huo wenye kutia moyo na inaeleza kwa nini kuna uovu mwingi sana duniani leo.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 20.
Mnara wa Mlinzi 01/05/10
“Je, umekwisha kujiuliza kwa nini Mungu anaruhusu kuteseka? [Acha mutu ajibu.] Ona jinsi mwandishi mmoja wa Biblia anatokeza ulizo moja ambalo watu wengi wamejiuliza. [Soma Zaburi 10:1.] Gazeti hili linazungumzia yale ambayo Biblia inasema kuhusu kwa nini Mungu anaruhusu kuteseka na yale anayofanya ili kumaliza mateso.”
Amkeni! Mwezi wa 5
“Watu wengi wanataka kuacha kuvuta tumbaku lakini wanaona kwamba ni vigumu sana kuacha. Je, unamjua mutu fulani ambaye angetaka kuacha kuvuta tumbaku? [Acha mutu ajibu.] Watu fulani wameona kuwa jambo lenye faida kutegemea msaada wa marafiki na watu wa familia. [Soma Mhubiri 4:12a.] Gazeti hili linatoa mashauri fulani yenye kufaa ya kumsaidia mutu aache kuvuta tumbaku.”