Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/08/09
“Watu wengi wanafikiri kwamba watu wazuri wote wataenda mbinguni. Je, wewe pia unaamini hivyo? [Acha mutu ajibu.] Ona jinsi andiko hili linavyosema kuhusu dunia. [Soma Zaburi 37:11, 29.] Habari hii inazungumzia mambo ambayo Yesu alifundisha kuhusu tumaini la wanadamu la wakati ujao hapa duniani.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 22.
Amkeni! Mwezi wa 8
“Kifo cha mzazi kinaleta huzuni nyingi sana. Je, unakubaliana na wazo hilo? [Acha mutu ajibu.] Watu wengi wamekwisha kufarijiwa na andiko kama hili. [Soma Ufunuo 21:4.] Habari hii inaeleza jinsi watu wanavyoweza kushinda hali ya kuwa na huzuni nyingi, zaidi sana vijana.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi 01/09/09
“Watu fulani wanasema kwamba ukiwa mwaminifu kwa Mungu, yeye atakubariki kwa kukupa mali, na kwamba umasikini unaonyesha kwamba mutu hakubaliwe na Mungu. Unafikiri nini? [Acha mutu ajibu.] Lakini inapendeza kujua kwamba Yesu hakuwa tajiri. [Soma Luka 9:58.] Gazeti hili linazungumzia aina ya baraka ambazo watumishi wa Mungu wanaweza kutazamia.”
Amkeni! Mwezi wa 9
“Je, unafikiri vijana wa leo wanapambana na magumu mengi kupita vijana wa miaka iliyopita? [Acha mutu ajibu.] Watu wengi wanakubali kwamba andiko hili linaeleza waziwazi hali ya wakati wetu. [Soma 2 Timotheo 3:1.] Gazeti hili linazungumzia kanuni za Biblia zenye kufaa zinazoweza kuwasaidia wazazi na vijana washindane na magumu wanayopambana nayo.”