Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/07/09
“Je, unafikiri kwamba inawezekana kupata amani ya moyoni katika nyakati hizi zenye taabu? [Acha mutu ajibu.] Ona yale ambayo Biblia inasema katika andiko la Wafilipi 4:6, 7. [Soma.] Habari hii inaeleza jinsi tunavyoweza kupata amani ambayo Mungu anatoa.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 10.
Amkeni! Mwezi wa 7
“Wengi kati yetu wanaonyesha shukrani kwa ajili ya mambo ambayo wazazi wetu wametufundisha. Je, unafikiri kwamba ni kukosa heshima kwa wazazi ikiwa tunachunguza mafundisho ya kidini tuliyofundishwa tangu utotoni? [Acha mutu ajibu. Kisha soma 1 Yohana 4:1.] Habari hii inatusaidia kujua ikiwa ni vibaya kubadili dini yetu.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 28.
Mnara wa Mlinzi 01/08/09
“Watu fulani wanasema kwamba dini zote ni barabara tofauti tofauti zinazoongoza watu kwa Mungu mmoja. Je, unafikiri kwamba dini zote ni nzuri? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Mathayo 7:13, 14.] Gazeti hili linazungumzia mambo matatu ambayo, kulingana na Biblia, dini nzuri inapaswa kuunga mkono.”
Amkeni! Mwezi wa 8
“Sisi wote tumekwisha kutendewa isivyo haki kwa sababu ya ubaguzi. Unafikiri Mungu anaona ubaguzi namna gani? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Matendo 10:34, 35.] Biblia inaweza kutusaidia tuvumilie tunapotendewa kwa ubaguzi. Inatusaidia pia kuondoa moyoni mwetu wazo lolote la ubaguzi ambalo tunaweza kuwa nalo. Gazeti hili linaeleza jambo hilo.”